CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,781
- 6,139
Aisha alikuwa binti mzuri Wa uso na umbo ..Aisha alijulikana kwa ukarimu wake na upole..
Siku moja Aisha akiwa na wasichana wenzake walitekwa na kuozeshwa kwa wanaume kinguvu...
Aisha aliishi utumwani kwa tabu akifanyishwa kazi za kila namna..
Wanasema hakuna marefu yasiyo na ncha hatimaye...mwaka 1961 ndugu zake aisha walijitutumua na kumkomboa ndugu yao na Inasadikika hakuna damu iliyomwagika na ndio maana Aisha hakuwa na DOA lolote katika mwili wake....
Aisha alirudi katika ardhi yake akapata mume ambaye hakumtesa Aisha ...alimpenda sana...pamoja na kumlea Aisha mume huyu alikuwa na malengo ya kuunganisha ndugu wote ili wasitekwe tena..Aisha alimpenda mume wake lakini Mungu alimpenda zaidi....akamchukua...
Hata hivyo Aisha aliachiwa Mali nyingi sana na mume wake....na alipewa angalizo kuwa wapo wanaume wakware watakaojitokeza ili wamrithi si kwamba wanampenda yeye Bali Mali zake!..
Hatimaye kweli wanaume wakajitokeza...kila mmoja akatoa Sera zake ...hatimaye akajitokeza Juma! Juma akakubalika machoni pa Aisha na ndugu zake....kwanza Juma alikuwa ni ukoo ule ule Wa mume Wa zamani Wa Aisha kwahiyo Aisha alidhani ataendeleza mazuri ya mumewe kipenzi! hatimaye Juma akapewa mke kwa sherehe kubwa....kipato huleta majivuno...Juma akabadili hati miliki zote zisome jina lake...nyumba,mashamba, viwanja vyote Juma akajimilikisha!!
Na mbaya zaidi juma akaanza tabia nyingine mbaya kabisa ya kumpiga mkewe kila anapodai haki yake!.. Juma akageuka nyang'au Mkubwa... kwa amani kabisa Aisha akaamua kutengana na Juma pamoja na wingi Wa miaka yote walioishi pamoja! hapo sasa akajitokeza mwanaume mwingine akadai yeye atamtunza vizuri Aisha kwa manufaa ya watoto Wa Aisha ..ikiwemo kuwasomesha mpaka watakapochoka wenyewe....kidogo Aisha alivutiwa nae...na kila alipokuja usiku Aisha alimuandalia chakula kizuri sana.
..hatimaye minong'ono ikaanza na kumfikia Juma... Juma akaanza vitisho kwa Aisha alidai kama Aisha akiolewa na bwana mwingine nyumba haitakalika..na Juma akaanza tabia ya kupita kwa ndugu zake Aisha akawashawishi kwa zawadi na bakshishi...kumbuka Juma ana mali nyingi..basi pole pole ndugu zake Aisha wakamshawishi eti arudiane na mumewe kwani amebadilika siku hizi! eti asisikilize porojo..
Kwa uchungu siku hiyo yule bwana mwingine baada ya kupewa mkanda mzima na Aisha alimwambia maneno machache tu..
"Aisha nakupenda sana kumbuka Juma anakulaghai...ni miaka mingapi umeishi nae ? zaidi ya 30 na amekufanyia mangapi Leo hii anakushawishi kwa vijizawadi hivi u akubal? Aisha Mimi nakuacha lakini Ipo siku utanikumbuka...
kweli Aisha akarudiana na Juma!! mwanzoni Juma alionyesha kweli sio Juma yule amebadilika kabisa huku akichapa kazi kwa bidii..
Aisha alifurahi na kuanza kumdhihaki yule bwana kuwa kumbe "angejichanganya" hata hivyo yule bwana alimjibu Aisha huku akitabasamu...
"Aisha Mimi nimekua nimecheza na Juma tangu utotoni utotoni ninamjua Juma vizuri...Juma ni yule yule hajabadilika na hatabadilika..."
mwisho
Siku moja Aisha akiwa na wasichana wenzake walitekwa na kuozeshwa kwa wanaume kinguvu...
Aisha aliishi utumwani kwa tabu akifanyishwa kazi za kila namna..
Wanasema hakuna marefu yasiyo na ncha hatimaye...mwaka 1961 ndugu zake aisha walijitutumua na kumkomboa ndugu yao na Inasadikika hakuna damu iliyomwagika na ndio maana Aisha hakuwa na DOA lolote katika mwili wake....
Aisha alirudi katika ardhi yake akapata mume ambaye hakumtesa Aisha ...alimpenda sana...pamoja na kumlea Aisha mume huyu alikuwa na malengo ya kuunganisha ndugu wote ili wasitekwe tena..Aisha alimpenda mume wake lakini Mungu alimpenda zaidi....akamchukua...
Hata hivyo Aisha aliachiwa Mali nyingi sana na mume wake....na alipewa angalizo kuwa wapo wanaume wakware watakaojitokeza ili wamrithi si kwamba wanampenda yeye Bali Mali zake!..
Hatimaye kweli wanaume wakajitokeza...kila mmoja akatoa Sera zake ...hatimaye akajitokeza Juma! Juma akakubalika machoni pa Aisha na ndugu zake....kwanza Juma alikuwa ni ukoo ule ule Wa mume Wa zamani Wa Aisha kwahiyo Aisha alidhani ataendeleza mazuri ya mumewe kipenzi! hatimaye Juma akapewa mke kwa sherehe kubwa....kipato huleta majivuno...Juma akabadili hati miliki zote zisome jina lake...nyumba,mashamba, viwanja vyote Juma akajimilikisha!!
Na mbaya zaidi juma akaanza tabia nyingine mbaya kabisa ya kumpiga mkewe kila anapodai haki yake!.. Juma akageuka nyang'au Mkubwa... kwa amani kabisa Aisha akaamua kutengana na Juma pamoja na wingi Wa miaka yote walioishi pamoja! hapo sasa akajitokeza mwanaume mwingine akadai yeye atamtunza vizuri Aisha kwa manufaa ya watoto Wa Aisha ..ikiwemo kuwasomesha mpaka watakapochoka wenyewe....kidogo Aisha alivutiwa nae...na kila alipokuja usiku Aisha alimuandalia chakula kizuri sana.
..hatimaye minong'ono ikaanza na kumfikia Juma... Juma akaanza vitisho kwa Aisha alidai kama Aisha akiolewa na bwana mwingine nyumba haitakalika..na Juma akaanza tabia ya kupita kwa ndugu zake Aisha akawashawishi kwa zawadi na bakshishi...kumbuka Juma ana mali nyingi..basi pole pole ndugu zake Aisha wakamshawishi eti arudiane na mumewe kwani amebadilika siku hizi! eti asisikilize porojo..
Kwa uchungu siku hiyo yule bwana mwingine baada ya kupewa mkanda mzima na Aisha alimwambia maneno machache tu..
"Aisha nakupenda sana kumbuka Juma anakulaghai...ni miaka mingapi umeishi nae ? zaidi ya 30 na amekufanyia mangapi Leo hii anakushawishi kwa vijizawadi hivi u akubal? Aisha Mimi nakuacha lakini Ipo siku utanikumbuka...
kweli Aisha akarudiana na Juma!! mwanzoni Juma alionyesha kweli sio Juma yule amebadilika kabisa huku akichapa kazi kwa bidii..
Aisha alifurahi na kuanza kumdhihaki yule bwana kuwa kumbe "angejichanganya" hata hivyo yule bwana alimjibu Aisha huku akitabasamu...
"Aisha Mimi nimekua nimecheza na Juma tangu utotoni utotoni ninamjua Juma vizuri...Juma ni yule yule hajabadilika na hatabadilika..."
mwisho