Simulizi: Penzi Kitunguu

Simulizi: Penzi Kitunguu

kibangubangu

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2018
Posts
272
Reaction score
353
ProductMarketingAdMaker_19012025_135722.png


SEHEMU YA 1

Danieli aliingia bila hodi,nyumbani kwa mpenzi wake alichokiona mbele ya macho yake aliamua kuyafumba, huku mwanaume aliyembele yake akiokota nguo zake kwa haraka zilizotapakaa sakafuni ili kujifunika.


Kabla hajafumbua macho,alisikia sauti ya mwanaume huyo aliyeonekana kumfahamu ikimwambia “Nisamehe kaka pole sana jamani” alisema mwanaume huyo huku akitoka nje ya chumba hicho kwa kasi ya ajabu.


Kitandani alikua amebakia msichana mrembo,akiusitili mwili wake kwa shuka lililolowa jasho la purukushani za tendo la uzinifu.


Hakuweza kukutana na macho ya mpenzi wake ambaye alikua mbele yake...Daniel kifua chake kilikuwa kinawaka moto na koo lake lilikuwa likiganda kwa maumivu ya mwanaume harisi yenye hasira zisizo elezeka...


Alikuwa amefadhaika kihisia,hata hivyo, alivuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu,akamwita
Graceeeeeeeeee.........!!!!!!!!!????

Grace hakujibu kitu huku akijikunja pale kitandani kama,chatu aliyekamata windo au kamba ifungayo mzigo,akifunika uso wake ulio jaa woga na aiibu kwa mikono yake inayo tetemeka ila yenye kucha ndefu za urembo.

"Grace"......... aliita tena ulinifanyia nini nikakusamehe? Unawezaje kunifanyia tena? Je, hii ni laana au kitu gani? Je, Musa si X wako,imekuaje unaruhusu tena anakuchezea heshima yako na yangu?!,na kudharirisha kimapenzi?”


"EEEEEhhhh Mungu nisaidie nisichanganyikiwe"
Daniel alisali asipoteze akili.


Grace akafungua kinywa chake kwa sauti ya chini na woga akasema "Sama.....Samahani mpenzi wangu"

Midomo ya Daniel ilitetemeka na kilio kilimtoka huku akimtizama mpenzi wake kwa uchungu,"Unasema samahani???!", alifoka
kwasira kali na chuki zilianza kumwagika kwenye mishipa yake,kama sumu ya nyoka koboko ingiapo katika mishipa ya kiumbe hai..

Daniel akashika kiti cha plastiki kilichokuwa karibu na T.V na kukibamiza ukutani. Kiti kilivunjika vipande vipande na kikitoa sauti za midondoko ya vipande vyake katika sakafu.

Samahani Daniel tafadhali…..” Grace alilia huku akimsogelea Daniel lakini jinsi Daniel alivyokuwa akimtazama Grace kama chui akaamua kurudi nyuma.

Uliomba msamaha mara ya kwanza,na ya pilli na sasa unataka msamaha tena...?!"

Grace akanyamaza na kukaa mwisho wa pembe ya kitanda huku macho yake yakiwa yamemtoka kwa kuchanganyikiwa.

"Pole sana Danie tafadhali..." Alilia kwa kwikwi.

“Tatizo lako ni nini hasa Grace”? Kwa nini unapenda kuniumiza sana? Hivi mimi kukupenda ni hatia!???Huu ni mwaka wa tatu wa uhusiano wetu!

Na umeamua leo unisaliti siku ya kumbukumbu ya uchumba wetu unajua leo nilikuja kwa kustukiza,unajua nilikua nakuja kukufanyia kitu gani msaliti wewe? ”

Dani aliingiza mkono mfukoni mwake na kutoa kisanduku…. Tazama… nimesema tazama juu!” Akamwita Grace!

Grace Alishtuka alipoona kisanduku cha pete… midomo yake ilitetemeka…..

Akasema “Daniel….. Tafadhali nisamehe mara hii ya mwisho, ninaahidi haitatokea tena” aliomba msamaha huku akitokwa na machozi.Daniel alicheka kwa uchungu na kusema "kwani mimi ni mjinga, siyo?"

Grace alisimama kwa woga, shuka likidondoka na kudhihirisha mwili wake kuwa ulikua upo uchi huku akimkimbilia na kumrukia Daniel na kumng'ang'ania kama gundi.

Grace alipomkumbatia akasema "Daniel...Si unanipenda...au... hunipendi akimtizama machoni....

Daniel huku akitabasamu kwa hasira, aliinamisha kichwa chake upande wa kushoto na kurudisha macho yake kulia kuelekea kwake.Akamwambia kwa kumnong'oneza Grace sikioni na kusisitizia kila neno alilosema.......


“Usiponiondolea mwili wako huu wa uasherati katika mwili wangu ulioukumbatia sasa hivi Grace, haki ya Mungu naapa.......ninamalizana na wewe nitakacho kufanya,hakuna mbwa yoyote duniani hapa atakayeweza kukutizama hata mara moja,hata hao wajinga unaolala nao hawatataka kuwa na chochote kuhusu wewe".

Alitishwa na maneno ya Daniel yaliyomtoka huku akijaa sura ya kutisha aliyomwonesha Grace.

Grace kwa haraka alijitenga naye mara moja bila kujaribu kuufunika mwili wake;

Akajificha kwenye kona ya chumba, akilia huku uso wake akiuziba kwa viganja vyake vilivyo bakiza jasho na manukato ya mwanaume aliiyefumaniwa naye.

Daniel akalirudisha kisanduku kile cha pete mfukoni na kupiga hatua chache kuelekea alipokuwa amejikunyata Grace.

Mwangalie wewe mwanamke...Nakuchukia Grace...unaniadhibu kwa mapenzi yangu kwako.

Daniel Alifungua mlango na kuondoka huku akiubamiza mlango kwa nguvu nyuma yake.


Grace alitoka alijikongoja na kuinuka akajifuta uso kwa mikono yake; alitembea polepole kwenye chumba, akasimama kwenye sanduku la mbao lililokuwa likining'inia ukutani.

Sanduku liliandikwa “First Aid” ilikuwa imeandikwa kwa ufasaha.Akaifungua na kutumbukiza mkono wake wa kulia.Akachukua kikopo kidogo cha dawa.

Haraka akakifungua na kukipeleka mdomoni. Alinyanyua kidevu chake huku vilivyomo ndani ya kikopo vikiingia mdomoni.


Harufu ya kidonge ilimkera, akafumba macho; akameza mate....


ITAENDELEA.......

*Script writing
*Story writing
 
SEHEMU YA PILI.

Katika sehemu ya kwanza tumeona siku ya kumbukumbu ya uchumba imegeuka kua siku ya maumivu ya mapenzi baada ya Daniel kumfumania mpenzi wake Grace akimsaliti na mpenzi wake wa zamani(x)....

Daniel kaondoka kwa hasira,wakati Grace kaparamia box la huduma ya kwanza na kumeza dawa zilizopo.

**************************

Zilikua ni dawa za kupunguza maumivu ya kichwa,ambacho kilikua kinagonga kama ngoma za mdundiko kila akifikilia na kukumbuka tukio la kufumaniwa na mpenzi wake hali yake inazidi kua mbaya.

Jasho likazidi mkumtiririka,akaamua kupiga hatua chache hadi kwenye kioo chake kilichosimama, akatulia akijitazama kwenye kwenye kioo hakupenda kujitizama,akatoka na kuelekea bafuni,akajimwagia
maji ya baridi mwilini,alihema huku mawazo mengi yakizidi kumpita kichwani.

Hakuamini amesahau vipi kama siku hiyo ni siku yao ya kumbukumbu ya uchumba wake na Daniel,kama angejua asinge fanya ujinga kama huo tena chumbani kwake,kwenye nyumba aliyopangiwa na mpenzi wake.

Alifunga bomba la maji ya kuoga, akanyoosha mkono kuchukua taulo, akatoka bafuni...

Mawazo yakazidi kumuandama,Mama yangu anampenda sana Daniel siku zote, na yeye ndiye alikuwa sababu kuu ya mimi kua naye,lakini mimi simpendi Daniel(Grace alijisemea moyoni)Isingekua mama ningemuacha kijana wa watu.

Alichomeka kifaa cha kukaushia nywele, akabonyeza kitufe, na kusogeza kifaa cha kukaushia nywele karibu na nywele zake zilizolowa maji, na kuruhusu upepo wa joto uingie kukausha nywele zake.

Grace alikua ni msichana mrembo,nywele zake ndefu na raini na pua yake iliyochongoka, kope nyeusi zilizo jaa na uso uliopangiliwa kikamilifu ukipambwa na macho makubwa na angavu,vyote vikisindikizwa na shepu moja matata,watoto wa mjini wanasema kiuno kijiko shepu sinia...

Rangi yake iliyokataa kua nyeusi au nyeupe ilimfanya kila mwanaume achanganyikiwe akimuona.

Grace alijiandaa kwenda nyumbani kwa mama yake ili akamueleze kilichotokea kabla Daniel hajafika nyumbani kwao.

Upande alipo Daniel*

Spika zilikuwa zikipiga kwa nguvu zote huku DJ akiendelea kufurahisha watu;akifanya kile alichoweza kufanya.

Mikono mingi iliinuliwa juu, huku mashabiki wakicheza kwa mdundo mzito.


Watu walijaa tele nafasi ilikua hakuna, viuno vya mashabiki vikiwa bize kuonyesha msisitizo wa kusakana ngoma kali za Dj mitaa ya Tabata.


Taa nyororo za zilimulika kwenye sakafu ya dansi ya kioo,kila mtu alikua na mpenzi wake walikumbatiana miili yao na kucheza,vinywaji vya kila aina vilipamba meza za Club moja maarufu mitaa hiyo.

Danieli alikua katulia,ameshika chupa ya mvinyo,lakini hakuonekana kufurahia mazingira yale,ni kama mwili upo pale ila akili ipo sehemu nyingine...


Alikua eneo ambalo watu wana furahia na kusheherekea wakati yeye alikua ni mwenye huzuni.

Daniel akajiwazia "Kwa kweli sipaswi kuwa hapa". Lilikuwa wazo baya kuja hapa; nahitaji kurudi nyumbani.


Akaanza kujipenyeza katika kundi la watu ili aende zake nyumbani,ghafla pembeni anamuona rafiki yake kipenzi Patric,rafiki yake kichaa asiyejua kupenda anapenda leo anaacha kesho,Daniel hupenda kumuita kijana mtukutu na kichaa.


Amemkuta akiwa ameketi kwenye kona ya ukumbi .Kulikua na kama chupa kumi za bia na mvinyo wa bei ghali zilikuwa juu ya meza mbele yake, alikuwa amezungukwa na wanawake wawili.

Daniel akajisemea kimoyomoyo hivi ni nani mwingine angeweza kumsahaulisha huzuni na maumivu yake ikiwa si kwa rafiki yake huyo kichaa Patric!


Daniel akasogea na kumgusa bega,Patric akageuka na kumuona rafiki yake Daniel,akainuka na kumkumbatia kwa bashasha kubwa,japo alishangaa kumuona kijana mstaarabu maeneo ya watu kama yeye ambao rafiki yake hupenda kuwaita vichaa.


"Ladies, meet my guy, my best friend, the one and only Doctor Daniel" Alimtambulisha kwa fahari kwa wanawake ambao wote walionekana kufurahi kumuona.

“Daniel, hawa ni wapenzi wangu.” Mmoja ya mwanamke alionesha kufurahia utambulisho,mwanamke ambaye kope zake zilikuwa zimejaa sana, pua iliyochongoka na midomo miwili yenye mvuto, nywele zake zilitambaa kama magugu ya baharini.


Daniel aliitikia kwa kichwa huku akitabasamu, “Halo warembo mnaendeleaje?” "Sisi tupo poa karibu shemu"walirudisha salamu yake kwa tabasamu naye akaketi.


"Oya leo umepatwa na nini hadi upo chimbo hizi?" Patric alimuuliza Daniel huku, akimpa chupa ya bia ambayo aliishika mkononi.

"Vipi au ile pisi imekuzingua tena?" aliuliza Patric.."Ndiyo yule mjinga kazingua,kama alichofanya mwanzo akafanya tena." Alijibu, akiinua chupa kwenye midomo yake na kupiga mafundo kadhaa.

"Kama vile ulivyosema,kipindi kile nilivyo mfumania,kuwa nisimsamehe atachepuka tena,mimi sikukusikiliza,kafanya tena leo ."

“Dah siwezi kufurahia mateso yako ila rafiki yangu unanichekesha sana,sasa kama nilisha kwambia na ukadhani nakudanganya unashangaa nini, pole sana.” Patric alijibu huku akiinamisha kichwa chini, “Huyo demu si mwaminifu, yule msichana ni kahaba kabisa.”

Huwezi jua kwanini wanaume wapole kama nyinyi huishia na makahaba namna hiyo.Daniel alimkazia macho rafiki yake akiwa amekaa kwenye kiti akinywa kilevi taratibu.

"Hii ndio maana kujidanganya ni bora zaidi..." Patric aliendelea "Kila mtu anajua mimi ni mjinga,ndiyo mimi ni mjinga ila nina furaha na maisha yangu.

Unaniumiza sana rafiki yangu,kila siku unafumania demu huyo huyo na bado unamrudia,ni nini sasa hii?

Sina sababu ya kuumia moyoni kwa sababu moyo wangu hauhusiki na mateso yako lakini wewe ni rafiki yangu ntafanyaje.


“Chukua kwa mfano, hawa warembo wawili, ni pisi zangu za kunipa furaha tu,ila zinajua kabisa mimi ni mwongo na wao ni waongo,hatupendani ila tunafurahiana.

"Ndiyo hizi ni pisi zangu za starehe wanifuata tu kwa sababu ya pesa zangu na mara nitakapomalizana nao, naachana nao na sitawakumbuka na wao hawata nikumbuka."


Daniel akaona mpenzi wa mmoja wa Patric akimpiga Patric shavuni,Daniel aliangua kicheko, alicheka kwa rafiki yake ambaye alikuwa kapigwa kofi na mwanamke Patric aliweka mkono kwenye shavu lake kupoza maumivu,japo hakuonekana kujali huku akiwasha sigara.

"Angalau huyu mwanamke kapiga shavu langu , na siyo moyo wangu." Patric alisema, akiweka sigara iliyowaka katikati ya midomo yake.

"Umewahi kuniahidi kwamba akikosea wakati huu hauta msamehe ," Patric aliendelea kuongea na Daniel.

"Umempa nafasi nyingi sana, naelewa unampenda lakini anakuchukulia kama mjinga, najua ni mrembo na kila kitu, lakini , jamani nakuhakikishia hata badilika, yeye ni demu wa mjini unajua anataka umaarufu na pesa, umaarufu pesa za haraka kuwa na wewe kwake haitoshi tafadhali sita kwambia hii tena,mwache huyo demu aende zake"

Daniel alihema,aliona rafiki yake alikuwa sahihi kwa kila jambo,ameshamsamehe mara nyingi sana kwa sababu alimpenda kwa dhati,hakuweza hata kueleza asilimia anazompenda.

Je, unawezaje kumpenda mtu ambaye anaendelea kukuumiza?Ni mwanamke mrembo kuliko wote ambaye hajawahi kumuona na alikuwa akifikiri kwamba angebadilika.

GRACE na DANIEL**
Walikutana hospitalini na Grace alikuwa mgonjwa sana na karibia kufa, alipata ajali ambayo karibu ikatishe maisha yake miezi miwili,alilazwa pale hospitalini kwao,alimpa kipaumbele na kuwatelekeza wagonjwa wengine wote kwa ajili yake.

Daniel alikaribia kufukuzwa kazi lakini alinusurika, alipambana kuhusu afya ya Grace na baadaye alifumbua macho na kumwita "Daktari"!

Mama yake Grace alimshukuru sana baada ya kuokoa maisha ya mwanae,alimkaribisha nyumbani kwao na ndipo mapenzi yake na Grace yalipo anzia.

Nyumbani kwa mama Grace

Mama Daniel kanifumania tena!
"Wewe nini!"?Mama alipigwa na mshangao..

Grace alishusha pumzi yake huku mama akimpiga jicho la hasira,"Ina maana Daniel alikukamata unachepuka? Ndani ya nyumba aliyokupangishia?"

Mama ake Grace akapiga hatua nyingine zaidi huku uso wake ukiwa hauamini maneno ya binti yake huku akiendelea. "Unamaanisha amekukuta kitandani mnafanya ngono wote wawili. Wewe Binti yangu ni wapi ulipoteza yako akili?” alisimama mbele yake.

"Nimefanya makosa mama, najua" Alijibu kwa kujitetea. "Sikujua angekuja wakati huo,mbali na hilo, Musa alikuja tu kunisalimia sikuweza kumfukuza,bahati mbaya tukajikuta tunafanya".

Aliona sura ya kukata tamaa na mshtuko uliokuwa umetanda usoni mwa mama yake, ndipo alipogundua kuwa alilitaja jina Musa.

Akajuta papo hapo, hakupaswa kufanya vile,aliuma kucha huku mama yake akija kwa utulivu na kukaa pembeni yake. , akiwa amekaza, uso ulielekea upande wake.

“Umesema Musàaaaaaaaa?” Mama yake aliuliza kimya kimya, lakini hakutoa sauti huku akiuma mdomo wa chini.

“Unamaanisha yule yule Musa aliyekuwa akiendesha gari usiku ule mliopata ajari karibu upoteze maisha yako ikiwa si kwa ajili ya daktari huyu aliyekuhudumia na Mungu angekua umefumba macho kaburini mwanangu...

Inakuajee umerudiana na X-wako inakuaje mwanangu....?

Grace akainuka kwa hasira kutoka kwenye kiti akasema "Ndiyo mama! Nilikuwa na Musa sawa? Alikuwa kapendeza sana katoka ulaya na pia alinipa vitu vya thamani na aliomba msamaha; ilibidi nimsamehe,na alisema amefungua kampuni ya urembo, hivyo atanisaidia sana katika kazi zangu za urembo mama"

“Unajua nilisikia upotovu na uhuni wako tangu ulipoenda chuo cha wanamitindo, ujue kama sivyo kwa huyu Daniel ungeweza kuwa umekufa na kazi yako ingeenda wapi?Mama Grace aliongea kwa hasira.

Mambo haya ya uanamitindo yamekugeuza kuwa kahaba,unachofanya ni uasherati kwa jina la umaarufu na pesa! Kumbuka, Daniel." aliiii.....

“Mamaaaaaaaaaaaa!” Grace alipiga kelele huku kifua chake kikipanda na kushuka, nimekusikiliza vya kutosha, “Kama unajua Daniel ni mkamilifu kwa nini usiende kuolewa nae! kila ninachofanya mama nafanya kwa sababu nilijifunza kwako! Grace aliongea kwa hasira.

"Ulinitoa nyumbani kwa baba yangu kwa vile alikuwa masikini na wewe ulitaka pesa!, Kwa hiyo tafadhali, natafuta pesa sawa mama?

Ulifikiri nilikusamehe!Kuniondoa kwa baba yangu..????

Usinilazimishe kuwa naye!Sitaki mwanaume masikini kama yeye!Kazi yake ya udaktari haina pesa ya kunitosha mimi.Kama yeye ni mkamilifu sana nenda mkaoane!" wewe si huna mume sasa,ulimkimbia baba yangu sababu ni maskini olewa na huyo Daniel wako unaemuona tajiri......

Mama yake Grace akabaki mdomo wazi,akamuita "Grace mwanangu......!!!!

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 3.

“Unajua mimi mama ako ninakutakia mema.” Sauti yake ilikuwa ya baridi ka na ya upole

"Nilifanya makosa kuhusu baba yako; kama ningeweza kurudisha siku nyuma, ningerudisha, binti yangu. Niliruhusu pesa kuchukua kitu bora ambacho nisingeweza kukupa ambacho ni familia kamili na yenye furaha.

Niliichukua furaha ya kuwa na familia iliyotimia najua unaweza usinisamehe kamwe. Ninaweza kukusihi tu usifanye kosa lile nililofanya.”

Grace bado hakujibu na hakuwa akimtazama mama yake.

"Unaweza kuwa na furaha yote unayotaka wewe ni mwanamke mtu mzima na uko huru kufanya kile kinachokufurahisha."

"...hata hivyo, kuwa na hekima sana na
tafadhali, tuna hoteli unaweza kwenda huko kufanya starehe zako,ila kamwe isifanyie katika mazingira ambayo Daniel atakukuta, usimdhuru kwa starehe zako amekuwa mtu mzuri kwako."

Grace alitabasamu,anaona kama mama yake kaongea pointi ambayo ni bora kuliko hata mazungumzo yao ya awali.

Swala la kufanya starehe na kuburudika hiyo kwake ilikuwa ni haki ya kutosha, ingawa haikuhitaji ridhaa ya mama yake alitaka yeye alitaka amani.

“Kwa hiyo tunamrudishaje Daniel mama?” Aliuliza...

"Nadhani nina wazo ya namna ya kumrudisha" mama yake alijibu "Lakini itakuwa wakati nitakaporudi kutoka kwa matembezi yangu. Naenda kwenye "date"

Grace alicheka, akionekana kushangaa sana.
"Mama una mchumba? Nilidhani hakuna wanaume wa kukupenda tena kwa umri wako."

Wote wawili walicheka.

“Sawa mama ngoja nikusaidie kuvaa nguo”

*DANIEL

Ilikuwa ni dakika chache baada ya saa mbili asubuhi. Ilikuwa asubuhi nzuri ya Jumapili na ilikuwa siku yake ya mapumziko. Bado alikuwa kitandani,hakujua ni nini angefanya kwa siku nzima na hakuwa tayari kujiumiza kufikiria juu ya yalio mtokea wiki mbili zilizopita alipo mfumania mpenzi wake.

Kama ingekuwa ni maamuzi yake angeweza kubaki kufanya kazi hospitalini lakini Prisca hakumruhusu.

"Unahitaji kulala,kupumzika na kufanya maamuzi mapya Daniel." Alikuwa amemwambia jana usiku. “Hujajipa mapumziko na unaweka nguvu zako zote katika kazi yako. Unahitaji kufanyia kazi mambo yako pia. Ikiwa utataka kuachana naye, unahitaji kumwita na kumwambia, kisha unaweza kuendelea na maisha yako.

Mimi na Patric tupo kukusaidia kulivuka hili si unajua..?”Hakika, Daniel alijua kwamba walikuwa marafiki pekee aliokuwa nao. Yeye na Prisca walikuwa wakifanya kazi katika hospitali moja.

Daniel alipata wazo la katembelee kaburi la shangazi yake, sababu mara atumiapo wakati kwenye kaburi lake kwa kawaida humletea amani isiyoelezeka.Aliwaza akitoka kaburini baadae angeweza kwenda ubalozini na kuhitimisha mipango yote inayohitajika kwa ajili ya safari yake ya nje ya nchi.

Wakati anawaza hayo Mlango uligongwa ghafla ukakatiza mawazo yake...

Alishangaa; alidhani yupo peke yake nyumbani. Inaweza kuwa nani? Ni bora isiwe Grace. Nani mwingine alikuwa na ufunguo wake wa nyumba? Je, inaweza kuwa mwizi?

Hodi ikasikika tena...

Mara moja akasimama, hakuweza kuvaa shati akabaki na boxer.

Mlango uligongwa tena, laini kwa sasa kwa nguvu zaidi,akausogelea mlango na kufungua...miwani mikubwa iliyofunika macho ya kupendeza ili mtazama,nywele zilizofunikwa kwa kitambaa kinachobana juu.

"Wewe ni nani?"

"Mimi ni Rahma, msaidizi wa kazi wa nyumba yako, pamoja na Grace"

Lo! ni wewe kweli bila shaka.

"Ninaomba radhi Rahma, hatujaonana kwa muda" ... alitaka kuuliza shida ilikuwa nini ya yeye kuja pale ...Ila Rahma akasema

"Grace amepata ajali, nimeambiwa niue nikuambie na mama yake wameenda hospitali!

"Moyo wa Daniel ulistuka kwa nguvu. "Mungu wangu. Ngoja nivae nguo.


HOSPITALI**

"Oooh Mungu Asante.."Rahma anahema na kushukuru "Asante Mungu"! Kwa kufika hospitali salama,maana ulikuwa ni muujiza mwingine badala ya mgonjwa kuwa mmoja tu pale hospitalini na wao pia wangekua majeruhi au maiti kwa jinsi Daniel alivyokuwa akiendesha gari kama kichaa kabisa!

Daniel alisimamisha gari ghafla na kufungua mlango,kukimbilia katika jengo la hospitali,wakati huo Rahma akibaki kwenye gari.

Wakati Rahma anataka kufungua mlango wa gari kushuka mara ghafla akakumbuka alitakiwa kumtaarifu mama mzazi wa Grace Bi Mbaga.

Lilikua ni agizo la mama ake Grace kuwa wakisha fika tu eneo la kupaki magari amtaarifu.

“Mungu wangu” Alimtazama Daniel akitoweka kwa mbali ndani ya jengo la hospitali huku yeye akiwa amebaki ndani ya gari akaichukua simu.

Akapiga simu ila network ilikua inasumbua,simu zinagoma kutoka,aliigonga goonga simu kwa nguvu kwenye kiganja cha mkono wake wa kulia,kuishawishi ikamate mawasiliano, na bahati mbaya akasababisha kuvunja kioo cha simu na wino wa kioo cha simu ukaanza kuvuja.

Aliogopa,alijitahidi kupiga tena kwa Bi.Mbaga kabla kioo hakiujajifunika kabisaa kwa wino..

Simu ikaita na kupokelewa " Rahma? Upo njiani..?”Mama Grace alihoji.... “Tumesha fika mama na Daniel kaingia katika jengo la hospitali mama.....

"Mjinga! Kwa nini hukunipigia simu mkiwa njiani kabla hamjafika kama nilivyokuagiza? mpumbavu!"

Simu ikakatwa.
****************************

Daniel aliingia kwa kasi hadi kwa muhudumu wa mapokezi "Habari za mchana, tafadhali umepokea binti anaitwa Miss Grace Mbaga aliletwa hapa"

Alimkodolea macho, yupo "Chumba 20A. Kwa upande wako wa kushoto tafadhali, alinyoosha kidole. "Asante" alitembea kuelekea uelekeo aliokuwa ameelekeza Macho yake yalitazama kwenye mlango huku akipita kila mmoja. “19A... 19C..... D... 20A...,” akasukuma mlango.

Jozi nne za macho zilikutana na macho yake alipokuwa akiingia. Bi Mbaga na Grace wote walikuwa wameketi karibu na kitanda,huku kuna Daktari alikuwa na upara pembeni yao, Daniel akasikia maneno machache kama "alikaribia kufa" "aliumia sana" "alitaka kujiua..."

Mama yake Grace alipo muona Daniel alimsogelea na kumkumbatia kwa huzuni,akasema mwenzako alitaka kujiua,tafadhali usiruhusu ex mjinga aingie kati kati yenu, Unajua mimi binafsi nakupenda kama mwanangu na najua wewe ni kitu bora katika maisha yake.

ITAENDELEA

kusoma epsode za mbele zaidi jiunge na group letu la hadithi na vitabu whatsup...kule hadithi ipo mbele zaidi

 
Back
Top Bottom