AK Mastori
Member
- Jul 26, 2024
- 5
- 6
SURA YA 1 - SAPRAIZ YA NGUVU
likua maajira ya saa tatu usiku kwenye jengo la gorofa la hostel ya wanaume katika chuo kikuu cha Mbezi Beach.
“Bilal, nenda gorofa ya kwanza chumba namba mia moja na nne uniletee laptop yangu!”
Kijana mwenye kiduku aliamrisha baada ya kufungua mlango wa chumba cha wakina Bilal na kutupa shilingi elfu moja sakafuni kabla ya kugeuka na kuanza kuondoka.
“Nimesahau, pia ukishuka ninunulie maji kutoka super market ya hapo chini.”
Yule kijana mwenye kiduku aligeuka na kutoa elfu moja nyengine na kuirusha chini kwa ajili ya Bilal kumnunulia maji.
“We kiduku! Kwanini mnapenda sana kumtuma tuma Bilal awafanyie vitu vyenu? Mda wote mnakuwaga na kazi ya kumnyanyasa tu.”
Rafiki wa kutoka chumbani kwa wakina Bilal waliuliza kwasababu walikua wamechoshwa na rafiki yao kutumwa tumwa.
“Hahaha! Bilal anaishi chumbani kwenu na wala hamjamsoma tu hadi leo? Huyu mtu ukimpa buku mbili tu unaweza kumuamrisha ata kula kinyesi,” Kiduku alijibu kwa dharau huku akiondoka na kucheka.
Sura ya Bilal ilibadilika kwa hasira na aibu huku akijitahidi kuyapotezea yale aliyoyatamka Kiduku. Baada ya hapo, aliinama kuokota zile pesa zilizorushwa na Kiduku huku akijiwazia, "Hapa nimeshatengeneza buku na inatosha kabisa kula wali maharage kutoka kwa mama ntilie wa site ya ujenzi iliopo jirani na chuo, silali na njaa tena leo, asante Mungu."
“Bilal..usiende! Kama hauna pesa za kutosha tutakuazima, na wala huna haja ya kuturudishia.” Kiongozi wa chumba chao alishindwa kujizuia na kujikuta akimwambia hivyo Bilal ili asidhalilike. Bilal alitikisa kichwa chake kabla ya kutabasamu na kusema, “Asante, lakini usijali ni sawa tu..”
Kisha Bilal akageuka na kuanza kutoka nje ya chumba chao. Mda huu, wavulana wote wa chumbani kwake walimuangalia Bilal akiwa anaenda huku wakitikisa vichwa vyao kwa kumhurumia.
Bilal hakuwa akifurahia kutumwa tumwa na wanafunzi wengine na alitamani na yeye kufurahia maisha ya chuo kama wenzake. “Ingependeza kama na mimi ningekua nasoma bila ya kuwa na hofu ya vitu vyengine.” Aliwaza.
Lakini kiuhalisia, Bilal alikuwa maskini sana. Ingawa wale vijana wa chumbani kwake walikua wakiishi nae vizuri kulingana na hali yake, hakutaka wamhurumie. Alikuwa anahofia kwamba itafika siku watamchoka tu na maisha yake ya chuo yatazidi kuzorota.
Ukiacha na hawa aliokuwa akiishi nao chumba kimoja, Bilal hakuwa na marafiki wengine wa karibu chuoni hapo isipokua wachache sana waliokua wakisoma kozi moja, kwani wanafunzi wengi walikua ni watoto wa kitajiri. Kilikuwa ni chuo cha gharama kuliko vyote katika wilaya hio, na yeye alikua akisoma kwa ufadhili tu kwasababu ya ufaulu wake mzuri.
“Bilal, nimemskia Kiduku akisema unashuka kwenda chini, si ndio?”
Mara hii, kijana mtanashati alievaa vizuri alikuwa akizungumza huku akitoka kutoka kwenye chumba cha jirani na Bilal.
Jina lake lilikua ni Daniel Mushi na alikua ni kiongozi wa chumba cha wakina Kiduku. Alikua ni kijana anaependwa na wanafunzi wa kike kwa sababu licha ya uzuri wake, Daniel pia alikua ni mtoto wa kitajiri. Hata hivyo, Daniel alikua akimdharau sana Bilal kwa kuwa alihisi ni kijana anaetia aibu tu kutokana na hali yake ya kimaisha.
Bilal hakuelewa kwanini huyu kijana anaemdharau hivi anamuongelesha, hivyo akatikisa kichwa kuitikia, “Ndio, naelekea chini.”
Daniel alitabasamu kabla ya kumpatia Bilal boksi lilijojaa vitu.
“Nina rafiki yangu mmoja yupo kwenye vimbweta vya mapumziko vya jirani na jengo la sheria, mpelekee hili. Utamkuta kavaa jinzi jeusi na tishet ya bluu bahari. Hii hapa buku tatu kwa ajili yako.”
Daniel alikua anapenda kuchezea wasichana na vimbweta hivyo ndio alikua anapenda kukutana nao. Pia alikua na marafiki wengi ambao ilikua ndio tabia yao hii.
Bilal hakuwaza sana kuhusu hili na alikubali kwa kuwa alikua kashazoea kutumwa tumwa.
Alichukua hilo boksi na shilingi elfu tatu akaanza kushuka ngazi. Alivyogeuka tu, alihisi kumsikia Daniel akicheka kwa mbali..
Bilal alishuka ngazi kwenda kuchukua laptop na kumnunulia maji Kiduku kabla ya kuanza safari ya kimbwetani kupeleka boksi alilokabidhiwa na Daniel.
Vimbweta vya mapumziko vya jirani na jengo la sheria vilikua maarufu kwa wapenzi wa chuoni hapo kukutana maajira ya usiku. Walivipa jina lililokua maarufu la vimbweta vya mahaba.
Bilal alivyofika vimbwetani hapo akaona mtu alievaa jinzi jeusi kwa mbali akiwa na binti wa kike. Walikua wamekaa chini kwenye bustani, eneo linalomulikwa vizuri na mwanga wa mwezi, wakipiga stori na kucheka pamoja. Bilal akaanza kuwafuata.
Alipowakaribia, Bilal alishtuka sana baada ya kuona sura ya mwanaume na mwanamke hao waliokuwa wamekaa hapo.
Ilikua ni kama kapigwa na shoti ya umeme.
Alikua ni Sheila!
Macho ya Bilal yakawa mekundu ghafla na boksi alilobeba likadondoka chini.
Sheila alikua ni mpenzi wa Bilal walioachana siku tatu tu zilizopita, tena ilikua ni Sheila alietaka wavunje uhusiano wao.
Wakati wanaachana, Sheila alimwambia anataka tu kuwa mwenyewe kwa muda ili atafakari mambo, lakini imekua siku tatu tu na tayari alikua na mwanaume mwengine, tena kwenye vimbweta vya mahaba!
Wawili hao nao walivyomuona Bilal anawafuata sura zao zilibadilika ghafla.
“Bilal..unafanya nini hapa? Wewe, wewe...usinielewe vibaya. Nipo na John kwasababu...”
Sheila alianza kupanik hapo hapo, akiwa anajiskia aibu kwa mazingira aliokutwa. Aliinamisha kichwa haraka na kuangalia chini kwa kutojua namna ya kumkabili Bilal.
Kijana John Rugemalila, ambae pia alikua ni mtoto wa kitajiri, alitupia macho kwenye boksi lilodondoshwa na Bilal kabla ya kuanza kucheka kwa nguvu.
“Duh! Kweli Daniel anajua kuwafanya watu wapumbavu. Nilimuomba aniletee hivi vitu na sikutegemea atakutuma wewe uvilete. Hii inafurahisha, inafurahishsa sana!”
Bilal alijua kuwa John, ambae ni mtoto wa kitajiri, ni rafiki wa karibu wa Daniel. Familia yao inamiliki migahawa mingi na alikua akitumia gari aina ya BMW 3 series chuoni. Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kukunja tu ngumi zake kwa hasira wakati akiskiliza maneno ya John.
Ilikuwa wazi kwamba Daniel alimfanyia hivi maksudi. Zaidi ya hayo, Bilal alianza kuhisi na kuamini kuwa Daniel alihusika katika yeye kuachana na Sheila, haswa baada ya kuona rafiki wa karibu wa Daniel yuko na Sheila siku chache tu baada ya mahusiano yao kuvunjika.
“Sheila, najua huna hisia na mimi lakini huna haja ya kuwa na mvulana wa namna hii baada ya mahusiano yetu kuvunjika. Unajua ni wanawake wangapi kawabadili huyu kabla ya wewe?” Bilal aliongea kwa sauti.
Alimpenda sana huyu dada, sana.
Shelia aliudhika na kauli ya Bilal iliotaka kumtia hofu na wasiwasi. “Bilal, unadhani wewe ni nani? Nani kakupa haki ya kunifundisha nini cha kufanya na kutofanya? Nimeshaachana na wewe na sasa naweza kuwa na mtu yoyote ninaetaka kuwa nae!”
“Pia...” Sheila alikua kashajawa na hasira mda huu. Akamtazama Bilal kabla ya kuendelea kumuuliza, “Kwani umekuja hapa maksudi? Embu potea”
‘Kofi!’
Baada ya kumaliza kuzungumza, Sheila alimsogelea Bilal na kumpiga kofi kali shavu la upande wa kulia.
John alicheka zaidi baada ya kuyaona haya. Kisha akamshika kiuno Sheila huku akiendelea kucheka na kuzungumza. “Hahaha. Sheila, kwanini unamfukuza huyu kapuku? Muache tu abaki atutazame tunavyofurahi!”
Sheila akatabasamu kiuchokozi. “John, nishapoteza hamu yote baada ya kumuona huyu mpuuzi hapa! Labda wakati mwengine...”
Baada ya hapo, Sheila akautoa mkono wa John kutoka kiunoni kwake.
Bilal hajui hata aliwezaje kutembea kutoka kwenye vimbweta hivyo. Akili yake ilikua kama imeganda na haifanyi kazi wakati huo.
“Kila kitu ni pesa tu. Nisingekua katika hali hii kama ningekua tajiri.“ Alijiwazia.
“Hahaha…”
Baada ya kufika hostel kwake, Bilal alisalimiwa na vicheko vya wanafunzi wenzake kwenye korido.
Daniel alikua kashika tumbo lake huku akicheka kwa nguvu zaidi. Ilikua dhahiri kwamba aliwaelezelea wanafunzi wenzake kuhusu tukio lote kwani yeye ndio aliolipanga.
“Hahaha. Bilal, uliona nini ulivyoenda kupeleka boksi uliloagizwa na Daniel?” Kiduku alimuuliza akiwa na tabasamu usoni mwake.
“Dah! Umepoteza demu mwenye umbo zuri sana mzee” Daniel aliendelea kuchochea huku akicheka.
Bilal alikunja ngumi kwa hasira na macho yake yalikua mekundu karibu kudondosha chozi. Alitamani amuue Daniel mda huo huo na yeye ajiue ili asiwe kwenye aibu hii tena.
“Kwanini? Kwanini unanifanyia hivi lakini Daniel? Nimekukosea nini?” Bilal alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye hasira.
Daniel aliendelea kucheka kabla ya kumjibu, “Sikia we mpuuzi, mimi sikuogopi kabisa. Hujui katika maskini wote wa darasani kwetu wewe ndio wa kutupa? Sheila ni msichana mrembo na ni hasara mtu kama yule kuwa kwenye mahusiano na mwanaume wa aina yako. Shukuru tu nimekutoa kwenye ramani na sasa anafurahia maisha na kijana anayeweza kumhudumia. Alafu nimekumbuka, hivi unajua John ameweza kumpata Sheila ndani ya nusu siku tu wakati wewe umehangaika karibu mwaka mzima kabla ya yeye kukukubalia? Tafuta pesa mzee.”
Kila mtu aliekuwepo alikua anamcheka Bilal mda huu na hamna aliejali hisia wala utu wake kabisa.
Bilal akaanza kumkimbilia Daniel kwa ajili ya kumpiga baada ya hasira kumzidia. Matokeo yake, yeye ndio alioishia kupigwa na marafiki wa Daniel na hakuweza hata kumgusa.
Wakati fujo hizi zikiendelea kukua, watu wa hostel hio walishaanza kujaa eneo hilo. Marafiki wanaokaa na Bilal chumba kimoja pia wakafika na baada ya kuona mwenzao anapigwa wakakimbilia kuamuru ugomvi na kumrudisha mwenzao chumbani kwao.
Bilal alifunika uso wake na shuka yake ya kujifunikia huku akiendelea kulia akiwa kitandani kwake.
“Kwanini? Kwanini mimi tu ndio wa kuonewa na kuvunjiwa heshima? Kwanini? Kwani sina hisia hata kama mimi maskini? Kwahio maskini ndio hatutakiwi kuwa na hisia? Yani mimi moyoni mwao sio mtu kabisa, kwanini unaniweka katika hali hii Mungu? Dua zangu huzisikii? Huoni ninavyodhalilika?”
Bilal aliendelea kusononeka moyoni na kushindwa kuzuia machozi kuendelea kububujika kutoka machoni mwake. Alishindwa kabisa kupoteza mawazo ya yaliyomtokea usiku huo.
Hajui hata ni muda gani alipitiwa na usingizi akiwa kajikunyata chini ya shuka yake akilia.
Bialal alilala usingizi mzito sana usiku huo, huenda kwasababu ni kutokana na kuchoka na mawazo na vilio vya yote yaliyomkuta.
Alipoamka asubuhi iliofuatia, hakukuwa na mtu chumbani kwao. Bilal alijua kiongozi wa chumba chao hakutaka aamshwe ili apumzike baada ya matukio aliyoyapitia usiku uliopita. Baada ya kushika simu yake, alishtushwa kuona kuwa kuna simu nyingi zimeingia na meseji ambazo hakuzijibu.
Kilichomshangaza zaidi, simu na meseji zote zilikua zikitoka kwenye namba za kigeni.
Kwakua hakuwa na salio kwenye simu yake, alishindwa kuipigia ile namba iliokuwa imepiga mara nyingi. Hivyo akaanza kupitia meseji zilizokua zimeingia.
Alishtushwa kuona meseji kutoka benki ya CRDB ikimtaarifu kuwa kiasi cha shilingi za kitanzania milioni arubaini na laki nne kimewekwa kwenye akaunti yake.
Kabla hajamaliza kustaajabu akapokea simu kutoka benki hio ikimtaka afike katika tawi la karibu kwa ajili ya mahojiano. Aliamka haraka haraka na kuvaa tishet na jinzi aliokua kavaa jana yake na kutoka mbio. Alisahau hata kuoga na kupiga mswaki.
Akiwa njiani, bado alikua haelewi nani anaweza kukosea na kuweka kiwango chote hicho kwenye akaunti yake. Mawazo na maswali yalijaa kichwani mwake na yote yalikosa majibu. Wakati akiendelea kuwaza, simu yake ikaita tena. Kuangalia ilikua ni ile namba ya kigeni. Aliipokea kwa haraka kabla haijakata, baada ya kupokea aliskia sauti ya kike ambayo haikuwa ngeni kwake ikimuongelesha.
“Bilal, assalamu alaikum. Ni mimi dada yako Aisha!”
“Dada! Waalaikumu salaam. Vipi mpo salama?” Bilal alishindwa kuzuia furaha ya kusikia sauti ya dada yake na kujikuta akitokwa na chozi. “Mama yupo wapi? Mpo wapi? Mbona hamjanitafuta miaka yote hii?” Maswali mfululizo yalitoka kinywani mwa Bilal.
Ilikuwa ni mwaka wa pili tangu mama na dada yake waondoke nchini kwenda katika falme za kiarabu kutafuta maisha bora. Wakati wanaondoka, familia yao ilikua katika hali duni sana. Mama yake alimnunulia simu ndogo ya kiswaswadu kwa ajili ya kuwasiliana nae lakini kwa bahati mbaya aliibiwa na kushindwa kurejesha laini kwani haikusajiliwa kwa jina lake na hakuwa na kitambulisho cha taifa muda huo, ingawa kwa sasa alikua ameshapata simu janja kutoka kwenye posho za chuoni na pesa anayotengeneza kwa kufanya shughuli za kutumwa. Pia, laini ya mama yake ilifungiwa baada ya kukaa kwa muda bila ya kutumika huko nje ya nchi. Hivyo hakuwa na taarifa zozote za ndugu zake.
“Embu punguza maswali kwa kasi basi mdogo wangu, nitakujibu vipi haraka hivyo? Nimekumiss dada yako.” Aisha alimjibu huku akiwa na furaha kuweza kuongea na mdogo wake kwa mara nyengine.
“Kiukweli huwezi kuamini nitakachokwambia, lakini mdogo wangu dua zetu za miaka yote zimejibiwa. Tumefanikiwa kukutana na baba yetu mzazi Bilal. Baba yuko hai. Na taarifa kubwa itakayokusapraiz ni kwamba baba anatokea kwenye familia yenye utajiri mkubwa sana huku Abu Dhabi. Wana uwekezaji kwenye makampuni makubwa duniani kote. Ni stori ndefu sana kuielezea kwa sasa lakini jua tu wewe ni kijana tajiri sana huko, sidhani kama kuna kijana anaekufikia kwa utajiri huko. Sasa mdogo wangu mimi naingia kwenye kikao huku, tutaongea vizuri nikipata nafasi.”
Bilal alishtuka na maelezo haya. Upande mmoja alitamani kuamini lakini kuzingatia na maisha waliyokulia na changamoto walizopitia alihisi dada yake anamtania tu.
“Dada acha masihara yako bwana. Kweli unataka tupoteze muda na salio kuongea hadithi za abunuasi wakati tuna mambo ya msingi chungu nzima ya kuongelea?”
Bilal alimjibu.
“Sikutanii Bilal. Kwanza nimetuma pesa ya matumizi kwenye akaunti yako kiasi cha dola elfu kumi na tano. Kwa kiwango cha kubadilisha fedha cha huko utakua umepokea kwenye shilingi milioni arubaini. Benki watazuia hio pesa kwa ajili ya kujiridhisha kuwa hutakatishi fedha hivyo kuna maelezo na vithibitisho nimekutumia kwa whatsapp uwaelezee ili uweze kutumia hio pesa. Naingia kwenye kikao sasa, tutaongea baadae.”
Bilal hakuamini alichosikia. “Kwa hio hizi pesa ni zangu?” alijiwazia. Kuhamaki alikua kashafika kwenye tawi la benki ya CRDB. Baada ya kuingia kuhojiwa na kutoa maelezo ya pesa ile, benki ilijiridhisha na kuondoa zuio kwenye akaunti yake.
Alivyotoka, akaingia kwenye atm kujiridhisha. Akajiaribu kutoa laki nne iliotoka bila ya changamoto yoyote. Aliruka ruka pale kwenye atm kufurahia hadi watu wakamshangaa. Ndipo aliporudi hostel za chuo na kwenda moja kwa moja chumbani kwao. Akajitupa juu ya kitanda huku akitazama juu na kusema kimoyo moyo:
“Mimi Bilal Hassan, mtoto niliyekulia kwenye umaskini..leo hii ni tajiri? Asante Mungu kwa kujibu dua zangu!”
Sura ya pili itaendelea
Whatsapp: 0746260961
likua maajira ya saa tatu usiku kwenye jengo la gorofa la hostel ya wanaume katika chuo kikuu cha Mbezi Beach.
“Bilal, nenda gorofa ya kwanza chumba namba mia moja na nne uniletee laptop yangu!”
Kijana mwenye kiduku aliamrisha baada ya kufungua mlango wa chumba cha wakina Bilal na kutupa shilingi elfu moja sakafuni kabla ya kugeuka na kuanza kuondoka.
“Nimesahau, pia ukishuka ninunulie maji kutoka super market ya hapo chini.”
Yule kijana mwenye kiduku aligeuka na kutoa elfu moja nyengine na kuirusha chini kwa ajili ya Bilal kumnunulia maji.
“We kiduku! Kwanini mnapenda sana kumtuma tuma Bilal awafanyie vitu vyenu? Mda wote mnakuwaga na kazi ya kumnyanyasa tu.”
Rafiki wa kutoka chumbani kwa wakina Bilal waliuliza kwasababu walikua wamechoshwa na rafiki yao kutumwa tumwa.
“Hahaha! Bilal anaishi chumbani kwenu na wala hamjamsoma tu hadi leo? Huyu mtu ukimpa buku mbili tu unaweza kumuamrisha ata kula kinyesi,” Kiduku alijibu kwa dharau huku akiondoka na kucheka.
Sura ya Bilal ilibadilika kwa hasira na aibu huku akijitahidi kuyapotezea yale aliyoyatamka Kiduku. Baada ya hapo, aliinama kuokota zile pesa zilizorushwa na Kiduku huku akijiwazia, "Hapa nimeshatengeneza buku na inatosha kabisa kula wali maharage kutoka kwa mama ntilie wa site ya ujenzi iliopo jirani na chuo, silali na njaa tena leo, asante Mungu."
“Bilal..usiende! Kama hauna pesa za kutosha tutakuazima, na wala huna haja ya kuturudishia.” Kiongozi wa chumba chao alishindwa kujizuia na kujikuta akimwambia hivyo Bilal ili asidhalilike. Bilal alitikisa kichwa chake kabla ya kutabasamu na kusema, “Asante, lakini usijali ni sawa tu..”
Kisha Bilal akageuka na kuanza kutoka nje ya chumba chao. Mda huu, wavulana wote wa chumbani kwake walimuangalia Bilal akiwa anaenda huku wakitikisa vichwa vyao kwa kumhurumia.
Bilal hakuwa akifurahia kutumwa tumwa na wanafunzi wengine na alitamani na yeye kufurahia maisha ya chuo kama wenzake. “Ingependeza kama na mimi ningekua nasoma bila ya kuwa na hofu ya vitu vyengine.” Aliwaza.
Lakini kiuhalisia, Bilal alikuwa maskini sana. Ingawa wale vijana wa chumbani kwake walikua wakiishi nae vizuri kulingana na hali yake, hakutaka wamhurumie. Alikuwa anahofia kwamba itafika siku watamchoka tu na maisha yake ya chuo yatazidi kuzorota.
Ukiacha na hawa aliokuwa akiishi nao chumba kimoja, Bilal hakuwa na marafiki wengine wa karibu chuoni hapo isipokua wachache sana waliokua wakisoma kozi moja, kwani wanafunzi wengi walikua ni watoto wa kitajiri. Kilikuwa ni chuo cha gharama kuliko vyote katika wilaya hio, na yeye alikua akisoma kwa ufadhili tu kwasababu ya ufaulu wake mzuri.
“Bilal, nimemskia Kiduku akisema unashuka kwenda chini, si ndio?”
Mara hii, kijana mtanashati alievaa vizuri alikuwa akizungumza huku akitoka kutoka kwenye chumba cha jirani na Bilal.
Jina lake lilikua ni Daniel Mushi na alikua ni kiongozi wa chumba cha wakina Kiduku. Alikua ni kijana anaependwa na wanafunzi wa kike kwa sababu licha ya uzuri wake, Daniel pia alikua ni mtoto wa kitajiri. Hata hivyo, Daniel alikua akimdharau sana Bilal kwa kuwa alihisi ni kijana anaetia aibu tu kutokana na hali yake ya kimaisha.
Bilal hakuelewa kwanini huyu kijana anaemdharau hivi anamuongelesha, hivyo akatikisa kichwa kuitikia, “Ndio, naelekea chini.”
Daniel alitabasamu kabla ya kumpatia Bilal boksi lilijojaa vitu.
“Nina rafiki yangu mmoja yupo kwenye vimbweta vya mapumziko vya jirani na jengo la sheria, mpelekee hili. Utamkuta kavaa jinzi jeusi na tishet ya bluu bahari. Hii hapa buku tatu kwa ajili yako.”
Daniel alikua anapenda kuchezea wasichana na vimbweta hivyo ndio alikua anapenda kukutana nao. Pia alikua na marafiki wengi ambao ilikua ndio tabia yao hii.
Bilal hakuwaza sana kuhusu hili na alikubali kwa kuwa alikua kashazoea kutumwa tumwa.
Alichukua hilo boksi na shilingi elfu tatu akaanza kushuka ngazi. Alivyogeuka tu, alihisi kumsikia Daniel akicheka kwa mbali..
Bilal alishuka ngazi kwenda kuchukua laptop na kumnunulia maji Kiduku kabla ya kuanza safari ya kimbwetani kupeleka boksi alilokabidhiwa na Daniel.
Vimbweta vya mapumziko vya jirani na jengo la sheria vilikua maarufu kwa wapenzi wa chuoni hapo kukutana maajira ya usiku. Walivipa jina lililokua maarufu la vimbweta vya mahaba.
Bilal alivyofika vimbwetani hapo akaona mtu alievaa jinzi jeusi kwa mbali akiwa na binti wa kike. Walikua wamekaa chini kwenye bustani, eneo linalomulikwa vizuri na mwanga wa mwezi, wakipiga stori na kucheka pamoja. Bilal akaanza kuwafuata.
Alipowakaribia, Bilal alishtuka sana baada ya kuona sura ya mwanaume na mwanamke hao waliokuwa wamekaa hapo.
Ilikua ni kama kapigwa na shoti ya umeme.
Alikua ni Sheila!
Macho ya Bilal yakawa mekundu ghafla na boksi alilobeba likadondoka chini.
Sheila alikua ni mpenzi wa Bilal walioachana siku tatu tu zilizopita, tena ilikua ni Sheila alietaka wavunje uhusiano wao.
Wakati wanaachana, Sheila alimwambia anataka tu kuwa mwenyewe kwa muda ili atafakari mambo, lakini imekua siku tatu tu na tayari alikua na mwanaume mwengine, tena kwenye vimbweta vya mahaba!
Wawili hao nao walivyomuona Bilal anawafuata sura zao zilibadilika ghafla.
“Bilal..unafanya nini hapa? Wewe, wewe...usinielewe vibaya. Nipo na John kwasababu...”
Sheila alianza kupanik hapo hapo, akiwa anajiskia aibu kwa mazingira aliokutwa. Aliinamisha kichwa haraka na kuangalia chini kwa kutojua namna ya kumkabili Bilal.
Kijana John Rugemalila, ambae pia alikua ni mtoto wa kitajiri, alitupia macho kwenye boksi lilodondoshwa na Bilal kabla ya kuanza kucheka kwa nguvu.
“Duh! Kweli Daniel anajua kuwafanya watu wapumbavu. Nilimuomba aniletee hivi vitu na sikutegemea atakutuma wewe uvilete. Hii inafurahisha, inafurahishsa sana!”
Bilal alijua kuwa John, ambae ni mtoto wa kitajiri, ni rafiki wa karibu wa Daniel. Familia yao inamiliki migahawa mingi na alikua akitumia gari aina ya BMW 3 series chuoni. Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kukunja tu ngumi zake kwa hasira wakati akiskiliza maneno ya John.
Ilikuwa wazi kwamba Daniel alimfanyia hivi maksudi. Zaidi ya hayo, Bilal alianza kuhisi na kuamini kuwa Daniel alihusika katika yeye kuachana na Sheila, haswa baada ya kuona rafiki wa karibu wa Daniel yuko na Sheila siku chache tu baada ya mahusiano yao kuvunjika.
“Sheila, najua huna hisia na mimi lakini huna haja ya kuwa na mvulana wa namna hii baada ya mahusiano yetu kuvunjika. Unajua ni wanawake wangapi kawabadili huyu kabla ya wewe?” Bilal aliongea kwa sauti.
Alimpenda sana huyu dada, sana.
Shelia aliudhika na kauli ya Bilal iliotaka kumtia hofu na wasiwasi. “Bilal, unadhani wewe ni nani? Nani kakupa haki ya kunifundisha nini cha kufanya na kutofanya? Nimeshaachana na wewe na sasa naweza kuwa na mtu yoyote ninaetaka kuwa nae!”
“Pia...” Sheila alikua kashajawa na hasira mda huu. Akamtazama Bilal kabla ya kuendelea kumuuliza, “Kwani umekuja hapa maksudi? Embu potea”
‘Kofi!’
Baada ya kumaliza kuzungumza, Sheila alimsogelea Bilal na kumpiga kofi kali shavu la upande wa kulia.
John alicheka zaidi baada ya kuyaona haya. Kisha akamshika kiuno Sheila huku akiendelea kucheka na kuzungumza. “Hahaha. Sheila, kwanini unamfukuza huyu kapuku? Muache tu abaki atutazame tunavyofurahi!”
Sheila akatabasamu kiuchokozi. “John, nishapoteza hamu yote baada ya kumuona huyu mpuuzi hapa! Labda wakati mwengine...”
Baada ya hapo, Sheila akautoa mkono wa John kutoka kiunoni kwake.
Bilal hajui hata aliwezaje kutembea kutoka kwenye vimbweta hivyo. Akili yake ilikua kama imeganda na haifanyi kazi wakati huo.
“Kila kitu ni pesa tu. Nisingekua katika hali hii kama ningekua tajiri.“ Alijiwazia.
“Hahaha…”
Baada ya kufika hostel kwake, Bilal alisalimiwa na vicheko vya wanafunzi wenzake kwenye korido.
Daniel alikua kashika tumbo lake huku akicheka kwa nguvu zaidi. Ilikua dhahiri kwamba aliwaelezelea wanafunzi wenzake kuhusu tukio lote kwani yeye ndio aliolipanga.
“Hahaha. Bilal, uliona nini ulivyoenda kupeleka boksi uliloagizwa na Daniel?” Kiduku alimuuliza akiwa na tabasamu usoni mwake.
“Dah! Umepoteza demu mwenye umbo zuri sana mzee” Daniel aliendelea kuchochea huku akicheka.
Bilal alikunja ngumi kwa hasira na macho yake yalikua mekundu karibu kudondosha chozi. Alitamani amuue Daniel mda huo huo na yeye ajiue ili asiwe kwenye aibu hii tena.
“Kwanini? Kwanini unanifanyia hivi lakini Daniel? Nimekukosea nini?” Bilal alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye hasira.
Daniel aliendelea kucheka kabla ya kumjibu, “Sikia we mpuuzi, mimi sikuogopi kabisa. Hujui katika maskini wote wa darasani kwetu wewe ndio wa kutupa? Sheila ni msichana mrembo na ni hasara mtu kama yule kuwa kwenye mahusiano na mwanaume wa aina yako. Shukuru tu nimekutoa kwenye ramani na sasa anafurahia maisha na kijana anayeweza kumhudumia. Alafu nimekumbuka, hivi unajua John ameweza kumpata Sheila ndani ya nusu siku tu wakati wewe umehangaika karibu mwaka mzima kabla ya yeye kukukubalia? Tafuta pesa mzee.”
Kila mtu aliekuwepo alikua anamcheka Bilal mda huu na hamna aliejali hisia wala utu wake kabisa.
Bilal akaanza kumkimbilia Daniel kwa ajili ya kumpiga baada ya hasira kumzidia. Matokeo yake, yeye ndio alioishia kupigwa na marafiki wa Daniel na hakuweza hata kumgusa.
Wakati fujo hizi zikiendelea kukua, watu wa hostel hio walishaanza kujaa eneo hilo. Marafiki wanaokaa na Bilal chumba kimoja pia wakafika na baada ya kuona mwenzao anapigwa wakakimbilia kuamuru ugomvi na kumrudisha mwenzao chumbani kwao.
Bilal alifunika uso wake na shuka yake ya kujifunikia huku akiendelea kulia akiwa kitandani kwake.
“Kwanini? Kwanini mimi tu ndio wa kuonewa na kuvunjiwa heshima? Kwanini? Kwani sina hisia hata kama mimi maskini? Kwahio maskini ndio hatutakiwi kuwa na hisia? Yani mimi moyoni mwao sio mtu kabisa, kwanini unaniweka katika hali hii Mungu? Dua zangu huzisikii? Huoni ninavyodhalilika?”
Bilal aliendelea kusononeka moyoni na kushindwa kuzuia machozi kuendelea kububujika kutoka machoni mwake. Alishindwa kabisa kupoteza mawazo ya yaliyomtokea usiku huo.
Hajui hata ni muda gani alipitiwa na usingizi akiwa kajikunyata chini ya shuka yake akilia.
Bialal alilala usingizi mzito sana usiku huo, huenda kwasababu ni kutokana na kuchoka na mawazo na vilio vya yote yaliyomkuta.
Alipoamka asubuhi iliofuatia, hakukuwa na mtu chumbani kwao. Bilal alijua kiongozi wa chumba chao hakutaka aamshwe ili apumzike baada ya matukio aliyoyapitia usiku uliopita. Baada ya kushika simu yake, alishtushwa kuona kuwa kuna simu nyingi zimeingia na meseji ambazo hakuzijibu.
Kilichomshangaza zaidi, simu na meseji zote zilikua zikitoka kwenye namba za kigeni.
Kwakua hakuwa na salio kwenye simu yake, alishindwa kuipigia ile namba iliokuwa imepiga mara nyingi. Hivyo akaanza kupitia meseji zilizokua zimeingia.
Alishtushwa kuona meseji kutoka benki ya CRDB ikimtaarifu kuwa kiasi cha shilingi za kitanzania milioni arubaini na laki nne kimewekwa kwenye akaunti yake.
Kabla hajamaliza kustaajabu akapokea simu kutoka benki hio ikimtaka afike katika tawi la karibu kwa ajili ya mahojiano. Aliamka haraka haraka na kuvaa tishet na jinzi aliokua kavaa jana yake na kutoka mbio. Alisahau hata kuoga na kupiga mswaki.
Akiwa njiani, bado alikua haelewi nani anaweza kukosea na kuweka kiwango chote hicho kwenye akaunti yake. Mawazo na maswali yalijaa kichwani mwake na yote yalikosa majibu. Wakati akiendelea kuwaza, simu yake ikaita tena. Kuangalia ilikua ni ile namba ya kigeni. Aliipokea kwa haraka kabla haijakata, baada ya kupokea aliskia sauti ya kike ambayo haikuwa ngeni kwake ikimuongelesha.
“Bilal, assalamu alaikum. Ni mimi dada yako Aisha!”
“Dada! Waalaikumu salaam. Vipi mpo salama?” Bilal alishindwa kuzuia furaha ya kusikia sauti ya dada yake na kujikuta akitokwa na chozi. “Mama yupo wapi? Mpo wapi? Mbona hamjanitafuta miaka yote hii?” Maswali mfululizo yalitoka kinywani mwa Bilal.
Ilikuwa ni mwaka wa pili tangu mama na dada yake waondoke nchini kwenda katika falme za kiarabu kutafuta maisha bora. Wakati wanaondoka, familia yao ilikua katika hali duni sana. Mama yake alimnunulia simu ndogo ya kiswaswadu kwa ajili ya kuwasiliana nae lakini kwa bahati mbaya aliibiwa na kushindwa kurejesha laini kwani haikusajiliwa kwa jina lake na hakuwa na kitambulisho cha taifa muda huo, ingawa kwa sasa alikua ameshapata simu janja kutoka kwenye posho za chuoni na pesa anayotengeneza kwa kufanya shughuli za kutumwa. Pia, laini ya mama yake ilifungiwa baada ya kukaa kwa muda bila ya kutumika huko nje ya nchi. Hivyo hakuwa na taarifa zozote za ndugu zake.
“Embu punguza maswali kwa kasi basi mdogo wangu, nitakujibu vipi haraka hivyo? Nimekumiss dada yako.” Aisha alimjibu huku akiwa na furaha kuweza kuongea na mdogo wake kwa mara nyengine.
“Kiukweli huwezi kuamini nitakachokwambia, lakini mdogo wangu dua zetu za miaka yote zimejibiwa. Tumefanikiwa kukutana na baba yetu mzazi Bilal. Baba yuko hai. Na taarifa kubwa itakayokusapraiz ni kwamba baba anatokea kwenye familia yenye utajiri mkubwa sana huku Abu Dhabi. Wana uwekezaji kwenye makampuni makubwa duniani kote. Ni stori ndefu sana kuielezea kwa sasa lakini jua tu wewe ni kijana tajiri sana huko, sidhani kama kuna kijana anaekufikia kwa utajiri huko. Sasa mdogo wangu mimi naingia kwenye kikao huku, tutaongea vizuri nikipata nafasi.”
Bilal alishtuka na maelezo haya. Upande mmoja alitamani kuamini lakini kuzingatia na maisha waliyokulia na changamoto walizopitia alihisi dada yake anamtania tu.
“Dada acha masihara yako bwana. Kweli unataka tupoteze muda na salio kuongea hadithi za abunuasi wakati tuna mambo ya msingi chungu nzima ya kuongelea?”
Bilal alimjibu.
“Sikutanii Bilal. Kwanza nimetuma pesa ya matumizi kwenye akaunti yako kiasi cha dola elfu kumi na tano. Kwa kiwango cha kubadilisha fedha cha huko utakua umepokea kwenye shilingi milioni arubaini. Benki watazuia hio pesa kwa ajili ya kujiridhisha kuwa hutakatishi fedha hivyo kuna maelezo na vithibitisho nimekutumia kwa whatsapp uwaelezee ili uweze kutumia hio pesa. Naingia kwenye kikao sasa, tutaongea baadae.”
Bilal hakuamini alichosikia. “Kwa hio hizi pesa ni zangu?” alijiwazia. Kuhamaki alikua kashafika kwenye tawi la benki ya CRDB. Baada ya kuingia kuhojiwa na kutoa maelezo ya pesa ile, benki ilijiridhisha na kuondoa zuio kwenye akaunti yake.
Alivyotoka, akaingia kwenye atm kujiridhisha. Akajiaribu kutoa laki nne iliotoka bila ya changamoto yoyote. Aliruka ruka pale kwenye atm kufurahia hadi watu wakamshangaa. Ndipo aliporudi hostel za chuo na kwenda moja kwa moja chumbani kwao. Akajitupa juu ya kitanda huku akitazama juu na kusema kimoyo moyo:
“Mimi Bilal Hassan, mtoto niliyekulia kwenye umaskini..leo hii ni tajiri? Asante Mungu kwa kujibu dua zangu!”
Sura ya pili itaendelea
Whatsapp: 0746260961