Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Na James Mbotela.
MUHTASARI WA MAISHA YA MWANDISHI
Mwandishi wa kitabu hiki, ni mzaliwa wa Frere Town, Kisauni, Mombasa. Baba yake ni Myao, akiitwa Mbotela ambaye alikuwa mmoja wa vijana wale waliookolewa baharini na Wazungu wa manowari za Waingereza zilizokuwa zikizuia biashara ya watumwa. Huyo baba alipenda sana kusafiri na Wazungu wa misheni pamoja na Wazungu wa kampuni katika safari zao za miguu kwendea nchi za bara. Alikuwa ni mmoja wa wale walioandamana na Bishop Hannington, Uganda. Na safari yake ya mwisho, yeye na wenziwe waliandamana na Mzungu wa biashara akiitwa Dick, kuelekea nchi za Wakikuyu na Wamasai. Mbotela alikuwa mchukuzi wa bunduki ya Bwana Dick, nao wote wawili waliuawa na Wamasai siku moja katika matata yaliyotokea huko Kedong Valley.
Mama yake mwandishi alikuwa Mnyasa wa ukoo “Kamtunda” akiitwa Halima, na alipobatizwa aliitwa Ida Halima. Yeye pia alikuja kutoka Mpanda, na chombo chao kiliwateremsha Unguja kwanza. Mwisho waliletwa Frere Town kwenye wajoli wenzao, na hapo ndipo alipopata kuolewa.
Mtoto wao alizaliwa Frere Town. Hajui lugha ya wazazi wake, basi kwa asili yeye ni Mnyasa, lakini kwa kawaida ni Mswahili wa Mombasa hasa. Baba yake alifariki akali mtoto yuko skuli, na mama yake alikuwa mtu wa shamba akitumainia kiserema chake.
Mama yake mjane, alipata taabu sana hata asiweze kumtunza mwanawe. Juma akaanza kuwa mtoro, ala apatapo, akikosa yuashukuru. Mama yake alimpeleka kwa mjomba wake, Mlenga, akakae huko.
Mwandishi alibatizwa akaitwa James Juma Mbotela (Juma yaani, alizaliwa Ijumaa, na Mbotela ni jina la ukoo, naye mwenyewe aona fahari sana kwa hilo jina la mababu). Basi huyu James Juma mwana wa Mbotela ingawa alikuwa maskini, lakini aliendelea sana na kusoma.
James Juma alimaliza masomo yote yaliyowekwa kuwa- fundisha watoto. Akashinda Scholarship iliyowekwa na Bishop wa Mombasa, Bishop Peel, akaingizwa kusoma katika Buxton High School.
Mama yake James alifariki mwaka wa 1904 wakati huo James yuasoma.
Katika mwaka wa 1903 Chama cha “Industrial Mission Aid Society” kilituma Bwana na Bibi Harrison waje Frere Town kufunza watu kazi, chini ya msaada wa Church Missionary Society. Ndipo Wazungu hao walipomtunuka James Juma. Baada ya Bwana Harrison kukaa Frere Town miaka miwili, alishikwa na homa mbaya, na daktari akamruhusu arudi Ulaya akapate afya njema. Walitaka waende na James Juma, mwishowe Bishop Peel akakubali, ndipo alipoandamana na Wazungu hao mpaka kwao Ulaya Uingereza, naye hakutaka kurudi Afrika hata kidogo. Na huo ni ushuhuda wa kutosha kuwajulisha kuwa alikuwa na raha kweli kweli!
Kwa vile alivyokuwa amekwisha onja utamu wa masomo, hakukaa bure Uingereza. Aliendelea kusoma katika L.C.C. School, West Hill School, Wandsworth, na sehemu nyingine katika Wandsworth Technical Institute. Nyakati za ruhusa alitem- bezwa mahali pengi, akapata rafiki wengi sana. Alipokuwa Uingereza alijaribu kuongeza maarifa katika kazi ya ukarani aliyokuwa akiifanya katika Buxton High School. Kwa neema ya Mwenyezi Mungu, aligeuzwa kuwa mwalimu Mwinjilisti!
Mwisho wa mwaka wa 1906 alirudi Afrika na Wazungu wale wale aliotoka nao Frere Town. Lakini mambo huendelea yakigeuka. Juma akawa Mwinjilisti, kwanza katika nchi za Wakikuyu, pili katika nchi za Wamasai, katika kabila lile lile lililomwua baba yake. Tatu alikuja akawa mkaaji kabisa Ukambani, pamoja na Wazungu wale wale.
Alimwoa Grace David mwezi wa March mwaka 1908 katika kanisa la Kambui, Kikuyu, ambaye alizaliwa Seychelles.
Watoto wake wote walizaliwa Ukambani, waume wanane na msichana mmoja. Na wawili, binti mmoja na mtoto wa kiume, walifariki dunia, mmoja mwenye umri wa miaka kumi na mmoja, na mwingine umri wa miaka tisa.
Mwalimu huyo James Juma alikuwa mtu wa mashughuli mengi. Alikuwa mwalimu wa skuli, mhubiri Injili, mfasiri lugha, fundi wa kujenga na wa kufanya na kuchoma matofali.
Sasa watoto wake wamepata elimu ya kutosha, maana wengine ni walimu, na wakulima, na mmoja ni mkalimani.
Yule Juma, mwana mmoja wa baba na mama, mpaka sasa ana wajukuu ishirini na wanne.
MUHTASARI WA MAISHA YA MWANDISHI
Mwandishi wa kitabu hiki, ni mzaliwa wa Frere Town, Kisauni, Mombasa. Baba yake ni Myao, akiitwa Mbotela ambaye alikuwa mmoja wa vijana wale waliookolewa baharini na Wazungu wa manowari za Waingereza zilizokuwa zikizuia biashara ya watumwa. Huyo baba alipenda sana kusafiri na Wazungu wa misheni pamoja na Wazungu wa kampuni katika safari zao za miguu kwendea nchi za bara. Alikuwa ni mmoja wa wale walioandamana na Bishop Hannington, Uganda. Na safari yake ya mwisho, yeye na wenziwe waliandamana na Mzungu wa biashara akiitwa Dick, kuelekea nchi za Wakikuyu na Wamasai. Mbotela alikuwa mchukuzi wa bunduki ya Bwana Dick, nao wote wawili waliuawa na Wamasai siku moja katika matata yaliyotokea huko Kedong Valley.
Mama yake mwandishi alikuwa Mnyasa wa ukoo “Kamtunda” akiitwa Halima, na alipobatizwa aliitwa Ida Halima. Yeye pia alikuja kutoka Mpanda, na chombo chao kiliwateremsha Unguja kwanza. Mwisho waliletwa Frere Town kwenye wajoli wenzao, na hapo ndipo alipopata kuolewa.
Mtoto wao alizaliwa Frere Town. Hajui lugha ya wazazi wake, basi kwa asili yeye ni Mnyasa, lakini kwa kawaida ni Mswahili wa Mombasa hasa. Baba yake alifariki akali mtoto yuko skuli, na mama yake alikuwa mtu wa shamba akitumainia kiserema chake.
Mama yake mjane, alipata taabu sana hata asiweze kumtunza mwanawe. Juma akaanza kuwa mtoro, ala apatapo, akikosa yuashukuru. Mama yake alimpeleka kwa mjomba wake, Mlenga, akakae huko.
Mwandishi alibatizwa akaitwa James Juma Mbotela (Juma yaani, alizaliwa Ijumaa, na Mbotela ni jina la ukoo, naye mwenyewe aona fahari sana kwa hilo jina la mababu). Basi huyu James Juma mwana wa Mbotela ingawa alikuwa maskini, lakini aliendelea sana na kusoma.
James Juma alimaliza masomo yote yaliyowekwa kuwa- fundisha watoto. Akashinda Scholarship iliyowekwa na Bishop wa Mombasa, Bishop Peel, akaingizwa kusoma katika Buxton High School.
Mama yake James alifariki mwaka wa 1904 wakati huo James yuasoma.
Katika mwaka wa 1903 Chama cha “Industrial Mission Aid Society” kilituma Bwana na Bibi Harrison waje Frere Town kufunza watu kazi, chini ya msaada wa Church Missionary Society. Ndipo Wazungu hao walipomtunuka James Juma. Baada ya Bwana Harrison kukaa Frere Town miaka miwili, alishikwa na homa mbaya, na daktari akamruhusu arudi Ulaya akapate afya njema. Walitaka waende na James Juma, mwishowe Bishop Peel akakubali, ndipo alipoandamana na Wazungu hao mpaka kwao Ulaya Uingereza, naye hakutaka kurudi Afrika hata kidogo. Na huo ni ushuhuda wa kutosha kuwajulisha kuwa alikuwa na raha kweli kweli!
Kwa vile alivyokuwa amekwisha onja utamu wa masomo, hakukaa bure Uingereza. Aliendelea kusoma katika L.C.C. School, West Hill School, Wandsworth, na sehemu nyingine katika Wandsworth Technical Institute. Nyakati za ruhusa alitem- bezwa mahali pengi, akapata rafiki wengi sana. Alipokuwa Uingereza alijaribu kuongeza maarifa katika kazi ya ukarani aliyokuwa akiifanya katika Buxton High School. Kwa neema ya Mwenyezi Mungu, aligeuzwa kuwa mwalimu Mwinjilisti!
Mwisho wa mwaka wa 1906 alirudi Afrika na Wazungu wale wale aliotoka nao Frere Town. Lakini mambo huendelea yakigeuka. Juma akawa Mwinjilisti, kwanza katika nchi za Wakikuyu, pili katika nchi za Wamasai, katika kabila lile lile lililomwua baba yake. Tatu alikuja akawa mkaaji kabisa Ukambani, pamoja na Wazungu wale wale.
Alimwoa Grace David mwezi wa March mwaka 1908 katika kanisa la Kambui, Kikuyu, ambaye alizaliwa Seychelles.
Watoto wake wote walizaliwa Ukambani, waume wanane na msichana mmoja. Na wawili, binti mmoja na mtoto wa kiume, walifariki dunia, mmoja mwenye umri wa miaka kumi na mmoja, na mwingine umri wa miaka tisa.
Mwalimu huyo James Juma alikuwa mtu wa mashughuli mengi. Alikuwa mwalimu wa skuli, mhubiri Injili, mfasiri lugha, fundi wa kujenga na wa kufanya na kuchoma matofali.
Sasa watoto wake wamepata elimu ya kutosha, maana wengine ni walimu, na wakulima, na mmoja ni mkalimani.
Yule Juma, mwana mmoja wa baba na mama, mpaka sasa ana wajukuu ishirini na wanne.