kiamangwana
Senior Member
- Feb 28, 2015
- 175
- 89
Nakumbuka miaka ya nyuma mchambuzi mmoja wa soka alikuwa maarufu sana kupitia DTV chanel ten kama sijakosea,alikua anaitwa LIKY ABDALA,kutokana na yule bwana kuonekana kila siku ya mechi kubwa akifanya uchambuzi basi baadhi ya wa TZ wakapendekeza agombee u katibu mkuu wa FAT enzi hizo kwani waliamini kwa jins anavyochambua basi moja kwa moja anafaa kuwa kiongozi,wakasahau kuwa kuwa mchambuzi tu hakufanyi uwe bora,,nimetoa mfano huu nikiangalia hiki kinacho endelea sasa,eti kwa kuwa tu ALLY MAYAYI anaonekana kila siku akifanya uchambuzi wa soka kupitia AZAM TV basi huyu anafaa,zaidi ya hapo watasema eti alicheza mpira,hivi tunataka viongozi wa kutupeleka WC au tunataka viongozi wa simba na yanga?simuungi mkono malinzi lakini sijaona wa kumng'oa au mwingine labda huyo mgombea aitwaye twaku kuru,,,yangu macho.