Sina hamu ya kula

mrsfulani

Senior Member
Joined
Oct 19, 2015
Posts
113
Reaction score
69
Habari zenu wapendwa

Mim ni mama mjamzito mimba ya kwanza nipo siku za mwisho kabis mda wowote Mungu akijalia najifungua..
Tatizo nimepoteza hamu ya kula kabisa nakunywa chai tu na uji pamaoja na maji ya barid basi

Haiwez kuleta madhara kwa kiumbe kilichopo tumboni au mim mwenyew nawez kushindwa kupush kwa kukosa nguvu.
Naogopa sana ila nimejitaida sana kula nashindwa.
Nawasilisha
 

Nitakushauri ule chakula baada ya mda mfupi. Unaweza kula kidogo hata mara sita. Pia, ni vizuri ukila supu za mboga na ya kuku pia ili upate nguvu pamoja na madini yanayohitajika ndani ya mwili wako. Ni vizuri zaidi ukila mboga za majani. Kunywa fresh juisi za matunda pia. Ni muhimu sana kwa wakati hii upate madini na virutubisho zote.

Nakutakia kila la kheri. Kama unamaswali lolote unaweza kuniuliza hapa: Nakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

Asante Sana.
 
unapo kunywa chai tia na kipande 1 cha Tangawizi mbichi unywe pamoja na chai na usipende kunywa maji baridi kunyw amaji ya uvuguvugu utakuwa na hamu ya kula .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…