Cvez
JF-Expert Member
- May 19, 2018
- 4,405
- 13,411
Mambo ni mengi hizi siku mbili tatu kama masikhara Mama kala kichwa cha Chalamila, akiwa huko huko kapita na yule wa Morogoro.
Jana asubuhi tu, tukaone Selfie ya Masheikh wa Uamsho na familia zao hata kabla ya taarifa rasmi ya kuachiwa kwao. Siku hiyo hiyo Bwana Seth nae kaachiwa kwa kutakiwa kulipa Bilioni 26. Ila watu wana mawe aisee jamaa hata hakuwaza kaamue arudi kitaa hela zipo tu.
Huku nako Oscar Oscar mzee wa Kaliua kaliwa kichwa. Walace Karia na TFF yake sio watu poa kabisa chinjilia mbali kabisa wote wanaotaka kutia kitumbua chao mchanga.
Kwengine GSM na Wazee wa Yanga wanasagiana Kunguni tu. Ila hayo ni mambo ya kifamilia sisi tunachotaka kujua ni je wataleta timu tarehe 3 July?
Mara tena unasikia eti Ronaldo katia hasara CocaCola ya zaidi ya dola bilioni 5 kisa kasogeza chupa wakati wa interview. Aisee Kuna watu wana nguvu wengine tunajaza ulimwengu tu.
Hata sijui nilikua naleta ujumbe gani?
Jana asubuhi tu, tukaone Selfie ya Masheikh wa Uamsho na familia zao hata kabla ya taarifa rasmi ya kuachiwa kwao. Siku hiyo hiyo Bwana Seth nae kaachiwa kwa kutakiwa kulipa Bilioni 26. Ila watu wana mawe aisee jamaa hata hakuwaza kaamue arudi kitaa hela zipo tu.
Huku nako Oscar Oscar mzee wa Kaliua kaliwa kichwa. Walace Karia na TFF yake sio watu poa kabisa chinjilia mbali kabisa wote wanaotaka kutia kitumbua chao mchanga.
Kwengine GSM na Wazee wa Yanga wanasagiana Kunguni tu. Ila hayo ni mambo ya kifamilia sisi tunachotaka kujua ni je wataleta timu tarehe 3 July?
Mara tena unasikia eti Ronaldo katia hasara CocaCola ya zaidi ya dola bilioni 5 kisa kasogeza chupa wakati wa interview. Aisee Kuna watu wana nguvu wengine tunajaza ulimwengu tu.
Hata sijui nilikua naleta ujumbe gani?