Sina raha wife katoka clinic kuambiwa mimba ipo upande..

menya inganyi

Senior Member
Joined
Aug 10, 2016
Posts
169
Reaction score
109
Naombeni ushauri wife ana mimba ya miezi 6 sasa katoka clinic ananiambia docta kuangalia kaona mimba ipo kwa juu upande sasa hii imenipa wasiwasi sana je tatizo gani linaweza kutokea na husababishwa na nini?
 
Kwani baada ya Dr.kugundua icho kitu amesemaje(nini ilikua hitimisho lake).
 
naombeni ushauri wife ana mimba ya miezi 6 sasa katoka clinic ananiambia docta kuangalia kaona mimba ipo kwa juu upande sasa hii imenipa wasiwas sana je tatizo gani linaweza kutokea na husababishwa na nini
Dr alieona tatizo ndio alitakiwa aeleze sababu ya tatizo, madhara yake na nini kifanyike only in TZ Dr haweki wazi mambo kwa mgonjwa wake MUNGU IBARIKI TZ
 
watu wengine wapumbavu sana.mtu ana siriaz case wao wanajua kubeza tu.pole mkuu. natumai wenye elimu na ujuzi watakusaidia
 
No siyo kubezi tatizo mkuu,hyo kesi ilibidi hyo mwanamama amuulize hy docta kwa nin imetokea sababu za kutokea hlo tatizo na madhara na solution vilevl nin anatakiwa afanye, mi naamini angepewa maelezo ya kujitosheleza huku asingekuja believe mi.
 
Polee sana,nenda clinic alipoenda mkeo ukaonane na huyo doctor ukiwa pamoja na mkeo then umuulize sababu ya kutokea kwa hiyo kitu na kipi kifanyike hope mtapata majibu yatayokuondoa hofu.
 
Ndio inaitwa ectopic pregnancy au?? nadhani sio genetic issues zinatakiwa care tu yakutosha!
 
Dr alieona tatizo ndio alitakiwa aeleze sababu ya tatizo, madhara yake na nini kifanyike only in TZ Dr haweki wazi mambo kwa mgonjwa wake MUNGU IBARIKI TZ
Achana kabisa na ma dr wetu wa kibongo weee....tena ukute nje ana nyoma anawahudumia fasta fasta muishe....hata maongezi (kumuelezea mjamzito maendeleo yake) kati ya dr na mgonjwa hakuna...
 
"Mimba ipo kwa juu upande"!! Kk ungetumia neno la kitaalam lililokuwa documented ingekuwa rahisi kukupa ushauri maana nafikiria ECTOPIC PREGNANCY ila sina uhakika cuz alwayz insemwa kama "mimba imetunga nje ya mfuko wa uzazi"..weka clear mkuu ushauriwe..
 
Naombeni ushauri wife ana mimba ya miezi 6 sasa katoka clinic ananiambia docta kuangalia kaona mimba ipo kwa juu upande sasa hii imenipa wasiwasi sana je tatizo gani linaweza kutokea na husababishwa na nini?

Usiwe na wasiwasi kwani tunapokuwa kwenye womb tunazunguka zunguka na hatua ya karibu na kutoka wengi wetu tuligeuka na kutanguliza kichwa kuelekea kwenye mlango. Unaweza kuta baada tu ya kutoka kwa doctor jamaa kesharudi kwenye right position.

Huyo doctor alitumia njia gani kupima position ya mtoto? Halafu ni vyema sana kwenda clinic na mkeo kwani mkeo anaweza akaelewa tofauti na doctor alichosema.

Angalia cheti cha mkeo halafu ingia kwenye Google na scholarly journals za maternity or pregnancy issues. La sivyo rudi nae kwa doctor in a week's time. Mwisho kabisa msaidie mkeo kazi zote za nyumbani ili apumzike vya kutosha.
 

Ingekuwa Ectopic isingefika miezi sita kwa maanake ni kuwa mimba ipo nje ya nyumba ya uzazi - womb yaani imetungwa na kubaki kwenye fallopian tube.
Ectopic pregnancy - NHS Choices
 
Muone specialist mkuu,kama upo Dar nenda Kairuki hospital ulizia Dr Mchonvu.
 
Ingekuwa Ectopic isingefika miezi sita kwa maanake ni kuwa mimba ipo nje ya nyumba ya uzazi - womb yaani imetungwa na kubaki kwenye fallopian tube.
Ectopic pregnancy - NHS Choices
Mkuu ectopic sio lazima ikae kwenye Falopian tubes(which is common) inaweza kukaa even kwny abdomen na sometime inaweza kwenda mpk term(40 weeks)..

Sent from my HTC Desire 816 dual sim using JamiiForums mobile app
 
ila ananiambia kua anasikia mtoto akicheza cheza tumboni kama kawaida
 
Watanzania wengi huwa hatuhoji kuhusu jambo fulani ili tupate kujua kwa undani, sijajua nani alitujengea tabia hii.

Kweli kabisa tatizo kubwa kiasi hicho dokta anamwambia mtu halafu haulizi chanzo ni nini na nini solution mpaka anakuja kuuliza JF iliyojaa division five za kutosha??

Mme naye badala ya kufuatilia tatizo kwa huyo dokta na madaktari wengine ili akiamua kureta mrejesho alete kitu kikiwa kimeshafanyia kazi; naye amekaa akisubiri majibu ya JF, mlioana lakini bado hamjajitegemea kifikra-HAMWEZI KUJIAMLIA MAMBO YENU WENYEWE. Na utakuta wote ni magraduates sijui wa chuo gani kile......

TUWE SIRIASI NA ISSUES ZINAZOHUSU AFYA ZETU JAMANI, LOOOOOOO.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…