Singa Singa Aua mtu kwa Bastola Kinondoni Mkwajuni

Singa Singa Aua mtu kwa Bastola Kinondoni Mkwajuni

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2007
Posts
4,120
Reaction score
3,468
Waheshimiwa wana JF Nimeleta taarifa hii ambayo chanzo chake ni WAPO FM inayosema kwamba hapo jana mnamo majira ya saa kumi jioni maeneo ya Kinondoni Mkwajuni Bondeni kulitokea mauaji. Tukio hilo linasema chanzo ni mzozo uliojitokeza kati ya jamaa mmoja mwenye asili ya Asia (Singasinga) ambapo wakati wakiwa katika vyombo vyao vya usafiri Singasinga akiwa kwenye pikipiki na mtu mwingine ambaye sasa hivi ni marehemu akiwa katika gari aina ya Toyota Carina.

Inasemakana singasinga huyu alitaka kulipita gari lililokuwa limeharibika mbele yake na kwa bahati mbaya akaanguka barabarani na katika harakati za kumkwepa huyo jamaa ambaye ni marehemu akabamiza gari lake kwenye kingo za barabara na kupasuka gurudumu. Alimwendea ili kumdai amlipe kwa kusababisha ajali ile hususani gurudumu kupasuka. Singasinga yule aliinuka akiwa na chupa ya kilevi aina ya wine akiwa anakunywa, ubishi ulipokolea alichomoa bastola yake na kumpiga kichwani yule mwenye Carina na kupanda pikipiki yake na kutoweka. Wananchi walioshuhudia tukio hilo kwa bahati mbaya hawakuweza kuchukua namba za pikipiki ile.

Kupitia JF nikiamini ni mtandao mkubwa ningeomba tujitahidi kutafuta taarifa na mwenye usahihi wa namba au kumfahamu huyo Singasinga atoe vyote hapa JF na bila shaka makachero wa polisi ambao ni wanachama wa JF watashughulikia.

Nawasilisha.
Asanteni.
 
Waheshimiwa wana JF Nimeleta taarifa hii ambayo chanzo chake ni WAPO FM inayosema kwamba hapo jana mnamo majira ya saa kumi jioni maeneo ya Kinondoni Mkwajuni Bondeni kulitokea mauaji. Tukio hilo linasema chanzo ni mzozo uliojitokeza kati ya jamaa mmoja mwenye asili ya Asia (Singasinga) ambapo wakati wakiwa katika vyombo vyao vya usafiri Singasinga akiwa kwenye pikipiki na mtu mwingine ambaye sasa hivi ni marehemu akiwa katika gari aina ya Toyota Carina.

Inasemakana singasinga huyu alitaka kulipita gari lililokuwa limeharibika mbele yake na kwa bahati mbaya akaanguka barabarani na katika harakati za kumkwepa huyo jamaa ambaye ni marehemu akabamiza gari lake kwenye kingo za barabara na kupasuka gurudumu. Alimwendea ili kumdai amlipe kwa kusababisha ajali ile hususani gurudumu kupasuka. Singasinga yule aliinuka akiwa na chupa ya kilevi aina ya wine akiwa anakunywa, ubishi ulipokolea alichomoa bastola yake na kumpiga kichwani yule mwenye Carina na kupanda pikipiki yake na kutoweka. Wananchi walioshuhudia tukio hilo kwa bahati mbaya hawakuweza kuchukua namba za pikipiki ile.

Kupitia JF nikiamini ni mtandao mkubwa ningeomba tujitahidi kutafuta taarifa na mwenye usahihi wa namba au kumfahamu huyo Singasinga atoe vyote hapa JF na bila shaka makachero wa polisi ambao ni wanachama wa JF watashughulikia.

Nawasilisha.
Asanteni.

hii nchi muda si mrefu itakua taleban
 
PoliceCCm wako bize kuwafuatilia Chadema na kuwabambikia kesi zisizo na kichwa wala mguu.
 
sijui nani anatakiwa kulinda usalama wa raia mbona matukio ya wananchi kupigwa risasi yanajirudia rudia namna hiyo?
 
Singasinga was under the influence of alcohol and then he was provoked by the dead man.! Hapo kimsingi hana case ya kujibu kwa sheria za Tanzania..!
 
Na si ajabu huyo singasinga asikamatwe!

Duh! Inasikitisha jamani!
 
Na si ajabu huyo singasinga asikamatwe!

Duh! Inasikitisha jamani!

Saa hizi keshavua kilemba akanyoa ndevu na nywele na kawa Baniani wa kawaida kabisa
images
images
 
Haya ndio matatizo ya kumilikishana bastola kama manati, ni juzi tu hapo Sinza Kumekucha dereva mwingine wa Coaster kauawa kwa risasi.
 
Back
Top Bottom