Singida tuchukue tahadhari ya Ugonjwa Kipindupindu

Singida tuchukue tahadhari ya Ugonjwa Kipindupindu

try me

Member
Joined
Nov 8, 2024
Posts
16
Reaction score
11
Kumekuwa na taarifa za mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu kwenye baadhi ya mikoa nchini. Mkoani Singida jambo hili sijalisikia lakini ni vyema mamlaka wakachukua hatua ya kuhamasisha usafi wa mazingira na haswa kwny migahahawa ya chakula na wauzaji wa vyakula mtaani.

Ukipita maeneo ya sokoni iwe soko kuu, Msufini, au hata stendi ya zamani Ginery ni kawaida kukuta wauza samaki wakiwa wanauza samaki bila kufunikwa. Lkn pia wao wauzaji wanashikashika hao samaki bila kuvaa japo mifuko laini kuepusha kuwagusa na mikono moja kwa moja.

Nafikiri Singida akipatikana mgonjwa mmoja tutashika rekodi ya kuwa na wagonjwa wengi wa kipindupindu kuliko sehemu nyingine nchini.

Mkuu wa wilaya Gondwe fanyia kazi jambo hili.

s1.jpg
s2.jpg
 
Inabidi kwanza elimu itolewe juu ya magonjwa ya milipuko ndipo muweze kukabiliana na hilo tatizo shida naiona ni wakazi wa huko hawana elimu.
 
Nimeshtuka hapo, nikadhani tayari
Miaka ya nyuma sana kulilipuka ugonjwa huu Singida nakumbuka sana
Unaingia Hoteli kula wameweka mapazia mlangoni
 
Back
Top Bottom