Sintofahamu katika upatikanaji wa wajumbe wa baraza la katiba!

Sintofahamu katika upatikanaji wa wajumbe wa baraza la katiba!

ungonella wa ukweli

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
4,210
Reaction score
556
Habarini wana jf! Taarifa za uhakika zilizopatikana toka maeneo mengi nchini hasa vijijini wananchi wengi hawajaelimisha au kujulishwa kwa uwazi juu ya nafasi zinazoombwa katika makundi mbalimbali kama ya mtu mzima,kijana.mwanamke na hata mtu mwingine. Wananchi wengi wameomba nafasi hizo kiujumla na kusababisha baadhi ya makundi kutowepo. Mfano baadhi ya maeneo vijana ni wachache kwenye orodha ya waombaji kuliko wazee, maeneo mengine wameomba watu wa aina moja tu kama watu wazima tu. Udhaifu huo umechochewa na watendaji wengi wa vijiji na mitaa kutojua namna ya kuwapata wajumbe hao. Pia baadhi ya maeneo madiwani wakishirikiana na watendaji wa kata wameteua watu wao kwa siri, na kutowatangazia umma juu ya namna ya kuomba nafasi hizo. Baadhi ya wananchi waliohojiwa maeneo mengi nchini hasa vijijini wanasema kulikuwa na ugumu katika kuomba nafasi hizo, hasa watendaji wakiulizwa walikuwa wakijibu hawana taarifa ya mambo hayo. Taarifa zilitolewa siku moja kabla ya tarehe ya mwisho ya kuomba ujumbe wa baraza la katiba yaani tarehe 20 march 2015. MYTAKE: TUME YA KATIBA ilipaswa kutoa semina kwa viongozi wa kata madiwani na watendaji wa vijiji na kata kabla ya kutoa tangazo kwa wananchi la kuomba nafasi hizo. Vinginevyo hatutapata wajumbe sahihi waliochaguliwa na wananchi!
 
That's true! hata huku ukerewe mambo ni uozo mtupu hata nafasi za walemavu na wanawake hawakuangaliwa kwa nafasi zao. Pili wajumbe wengi walichaguliwa kutokana na udini na itikadi za kisiasa bila kujali au kuangalia uwelewa na upembuzi wa kuweza kuichambua katika vizuri. JE KWA NAMNA HIYO KWELI WATANZANIA TUTAPATA KATIBA ITAKAYOKIDHI MAHITAJI YETU? WANA Jf. JADILI HAYA MAONI YANGU, NASUBILI!
 
kima eneo fulani watu wanachaguana kwa kigezo cha dini tena wanabebana kwenyd malori
 
Sitofahamu pia imeingia katika utaratibu wa nani ashiriki katika upigaji kura ndani ya kata hasa baada ya baadhi ya halmashauri kuwataka madiwani na wenyeviti washiriki peke yao bila makundi mengine ndani ya kata kushirikishwa mfano halisi lindi vijijini. Na shakushangaza wagombea hawakuhitajika katika mkutano huo. hii siyo haki wala sawa.
 
wanalipwa shilling ngap hawa wajumbe wa mabaraza ya katiba??
 
Kwa mtazamo wangu binafsi naona watanzania bado ni wachanga sana kuweza kutunga katiba, tunacho takiwa kufanya ni kuiga katiba bora duniani ya Marekani na kufanya marekebisho kidogo kuendana na nchi yetu.Marekebisho hayo yafanywe na wataalamu waliobobea na wazalendo.Ili tuendelee tunahitaji Wisdom, Precision and beauty. Hata hayo aliyosema Nyerere ya Siasa safi n.k yapo katika hayo mambo matatu niliyoyataja.Hakuna haja ya kupoteza muda tuwaige wazungu na tuchanganye na akili zetu kama walivyofanya India, China n.k. hatuwezi kutembea wakati wenzetu wanakimbia.
 
Back
Top Bottom