Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Mkuu tuletee pia na version yako inafikirisha sana, ila mpk watu wanafikia kupigana ujue wamegota mwisho kwa uonevu

Sent using Jamii Forums mobile app
Wale watu hawakua wanapigana wala kuuwana bali walikua wanaua tu. Na ilkkua ni mauwaji yaliopangwa. Bora wangeendelea kupigana baina ya majeshi ya serikali na majeshi ya Kagame hadi mshindi apatikane au wange implement makubaliano ya Arusha waliokua wote wamesaini bila kuua raia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo ni Sabato. Hahaha. Tunasubiri mzee mwenzangu leta Habari.
 
Mnaanza uchawi eeeeeenh kwamba itaendelea kwenye kitabu au

Sent using Jamii Forums mobile app
Uchawi upi? Ule ni ushauri tu nimempa maana yake sio kwamba aikatishe hapa ili aitolee kitabu, hapana, nadhani utakua hujanielewa point yangu.. Unajua hizi issue za history history ni asset kubwa sana hasa kwa wenzetu wazungu wanaopenda mambo ya kufanya tafiti na documentary..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bahati mbaya mlolongo wa masimulizi haujapewa namba ili nikurejeshe katika kipande husika, Bossless alidai ubalozi wa Malawi na nyinginezo zilivamiwa siku chache kabla ya hawajapandishwa malori kuondoka Kigali, wakati huo mambo yalipamba moto. Vamizi za balozi hazikulenga wanadiplomasia bali wale wanyarwanda walokimbilia hapo kusaka hifadhi kama ambavyo walikuja ubalozi wa Tanzania. Na hadi watanzania wanaanza safari yao, hakukuwa na shambulio wala uvamizi mkubwa kwenye ubalozi wetu.

Yaani kitu ambacho akili yangu huwa haikiamini katika mikutano ya usuruishi ni nia ya dhati ya wenyeji wa mikutano hiyo. Mara nyingi wasuruhishaji wanao upande wanaoutegemea ushinde. Ndo maana tunayo matukio kadhaa ya viongozi kulipuliwa angani wakitokea katika hiyo mikutano ua suruhu! Rejea kwa Museveni dhidi ya South Sudan; Abyarimana na mwenzake wakitokea Tz... Hata Nkurunziza amekataa kuhudhuria baadhi ya mikutano kwa hofu ya kukutwa na yalowakuta watangulizi wake.

Jamii huelezwa kile ambacho wakuu wanataka kifahamike, ukweli huwa hauwekwi hadharani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnaanza uchawi eeeeeenh kwamba itaendelea kwenye kitabu au

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeonaeee wameanza kumhamisha mawazo mleta mada wakati jamaa ameamua kutema nyongo tu kwa yanayomsumbua siku nyingi.

Huyu mtu kufanya kazi ubalozini moja kwa moja anakuwa Usalama wa Taifa, anajua mambo mengi ya ndani nje ya nchi alizofanyia kazi.

Isikute Jamaa ana nafasi kubwa tu serikalini huko, sasa ushauri wa kuanza kufanyia biashara matukio aliyokutana nayo akiwa kazini ni kama uhaini tu.

Mwacheni jaamaa ateme nyongo yake maisha yaendelee, tuburudike,tujifunze na kuelimika kuhusu yaliyowakuta wenzetu.
 
Mkuu! wakati raia wanauawa hovyo hawa askari wa UNAMIR walikuwa kimya tu bila kufanya kitu?
 
Well spoken kiongozi. Na nikwambie kitu mara baada ya ndege ile kushambuliwa na kuuawa kwa marais hao mtutsi yeyote aliyekuwa ughaibuni alifanya sherehe kubwa au ndogo, kwa uwazi au kwa usiri kufurahia tukio hilo.

Wiki chache sana kabla ya tukio la ndege kutunguliwa kulikuwa na mkutano mkubwa sana pale jijini Mwanza uliowakutanisha watutsi wote kutoka kanda yote ya ziwa. Mkutano huo mkubwa na wa aina yake ulifanyika pale Vijana Social Hall jirani na uwanja wa mpira wa CCM Kirumba. Lango kuu kulikuwa na udhibiti mkubwa sana na walioruhusiwa kuingia ndani ni watutsi pekee yake.

Hata hivyo mimi nikiwa nje nilibahatika kuwaona watu fulani watutsi waliokuwa wakiishi Mwanza kipindi hicho kwa kivuli cha wafanyabiashara na wengine watumishi wa serikali waliokuwa na nyadhifa kubwa kubwa kwenye taasisi mbalimbali za serikali wakihudhuria mkutano huo ulioashiria kwamba kuna jambo kubwa walikuwa wanapanga kulitekeleza, wanataarifiwa au kuwekana sawa. Kiufupi hakuna mtutsi yeyote aliyekuwa na umri wa zaidi ya miaka 18 ambaye hakuhudhuria mkutano huo pasipokuwa na sababu maalumu maana kulikuwa na uhamasishaji sana ili wahudhurie bila kukosa.

Baada ya vifo vya marais hao wawili, mauaji ya kimbari yaliyofuatia na baadae watutsi wengi kurudi kwao Rwanda, wengi wa watu hao niliowafahamu waliokuwa katika mkutano huo walipata nyadhifa kubwa kubwa katika serikali ya Rwanda.

Hata baadhi ya watu nchini (watutsi) waliokamatwa kwa kudaiwa kufanya sherehe za waziwazi kutokana na furaha waliyokuwa nayo baada ya kuuawa kwa marais hao, baadae waliachiwa huru kwa amri kutoka mamlaka za juu. Ndiyo maana kuna speculations za hapa na pale kwamba hata TZ kuna upande ilikuwa ikipendelea kwenye yale majadiliano yaliyokuwa yakiendelea ili kuleta muafaka wa amani/kiuongozi.
 
Good analysis ila hapo mwishoni umekunya japo ni haki ya kikatiba kunya
Kunya ni haki ya kiafya si ya kikatiba, kama wewe haunyi ujue bawasili ndo inakwamisha...nakutania mkuu!

Nilijua kuwa hiyo sentensi itawakwaza wengi. Ila point yangu ilikuwa hivi, sisi watanzania ni wazuri sana kuonyesha hisia zetu za kuipinga serikali huku mitandaoni, ila hakuna kabisa vijana wenye ujasiri wa hata kuwatetea mademu zao kama alivyofanya Bossless kwa manzi wake wa kinyarwanda mbele ya interahamwe wenye mikanda ya risasi. Sasa kwa haina hiyo ya vijana, nani ataweza kusumbuana na nguvu ya dola, hata kama uonevu upo dhahiri...!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaweza kusema mauaji ya huko Rwanda yalichochewa zaidi na chuki ya kikabila ndani ya Rwanda kwenyewe na kama kuna uhusika wa nchi jirani huenda ni kwa uchache sana tofauti na chanzo kikuu ambacho ni chuki za kikabila ndani ya nchi husika.

Uhusika wa nchi jirani upo kimaslahi ya kiushawishi kikanda mfano Uganda ya Museveni inafahamika ilikuwa na urafiki na RPF ya Kagame huku Zaire (DRC) ya Mobutu ilikuwa na urafiki mzuri na serikali ya Habyarimana.

Hata upande wa mabeberu kama walihusika basi ni ushawishi wa kikanda tu maana hapo awali Ufaransa ilikuwa na ushawishi mkubwa huko Rwanda wakati wa Habyarimana na hata huko Zaire wakati wa Mobutu.

Ila baada ya RPF kushinda Vita huko Rwanda na Mobutu kupinduliwa huko Drc basi nafasi ya ushawishi ya Ufaransa imechukuliwa na Marekani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…