Mkuu una hoja.Ila punguza kwanza hasira ili uweze kueleweka vizuri.
Nchi yetu sote hii,tukosoane katika namna ya kujenga na si venginevyo.
Ok mkuu unajua nilikasirika zaidi sababu mimi ni mtaalamu katika tropical infectious disease control. Kilicho fanyika pale ni siasa tupu na hatari sana kwa Taifa na uji.nga sana.
Ngoja nikueleze tu kidogo kwa nini ni hatari. EBOLA ni a very highly infective virus. Yani kwenye kugrade level ya tahadhari ya kuchukua katika ku handle mdudu huyu scientist wanachukua tahadhari ya juu kuliko kitu chochote. Iko category 5 ya infection ambayo ndio highest.
Africa nzima kuna maabara 1 tu iliyopo South Africa ambayo ina kiwango cha usalama cha kuweza kuruhusiwa ku run research ya ya virusi kama EBOLA, hii ni kutokana na umahiri wake wa kuambukiza.
Nafikiri nawe umeona katika television yale masuti wanayovaa watu wa afya wanapoenda maeneo yenye EBOLA.
Pia umeona kifaa maalumu walichobebewa wazungu wale waliopata EBOLA kwenda kutibiwa huko kwao. Na kule kwao waliwekwa kwenye high quarintine rooms. Hivi vyumba ndugu vimejengwa mahususi kiasi ambacho hewa ilioyoko mle ndani haitolewi nje bila kuchujwa, maji yanayotoka mle hayapelekwi kwenye system ya kawaida ya maji na vitu vingine vingi kuepusha risk ya maambukizi.
Sasa kile kibanda alichoenda kufungua huyu rahisi wenu na kuwaambia ni wodi mahususi ya wagonjwa wa EBOLA hakiwezi hata kuzuia maambukizi ya TB. Na ni uji nga kuweka ile wodi sehemu yenye kadamnasi kama TEMEKE.
Hivyo kama ikitokea kweli akatokea mgonjwa wa EBOLA na mkampeleka pale Temeke, (Mungu epusha) itakua ndio mnapalilia maambukizi ya huu ugonjwa na kuukaribisha kabisa Tanzania kwetu.
Yani inaweza kutokea mlipuko huo ambao hamtaamini.
Kama basi ilibidi ijengwe wodi ya wagonjwa wa EBOLA cha kwanza ilitakiwa iwe karibu na mipaka yetu ya Kaskazini Magharibi, na mbali mno kutoka katika eneo lolote lenye watu, sababu hatuna ujuzi wala uwezo wa kujenga a quarentine ward katikati ya jiji kwenye mahopsitali yetu. Hili tu jamaa kaenda fungua halafu mabomba hayatoi maji!! Ingetafutwa secure isolated area ndio hio ward ijengwe.
Kujengwa kwa ile ward Temeke ni rahisi kutaka kuonekana ana jali na uongozi wake uko makini lakini ni uji.nga na hatari sana kwa Taifa letu. Tuache kuchanganya Siasa kwenye mambo ya kitaalm.