VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
Wengi mnajua jinsi Spika Job Ndugai alivyokuwa 'akiwashughulikia' Wabunge wa Upinzani wakati ule wa Mwendazake. Alikuwa akitimiza agizo la 'kuwashughulikia' wapinzani ndani ya Bunge huku kazi ya kuwashughulikia nje ya Bunge ikifanywa kwa ustadi mkubwa na Mwendazake mwenyewe. Walengwa wakuu wamekuwa ni CHADEMA na Wabunge wao.
Kulingana na kikichotokea wakati na baada ya uchaguzi wa mwaka jana, CHADEMA 'haina Wabunge' katika Bunge la sasa. Ndiyo kusema, Spika hana 'targets' zake za kuzishughulikia. Ghadhabu zake zinakosa pa kujitokeza na kuzifaidi. Sasa ameamua kuanzisha maigizo yasiyo na maazigo.
Bunge la CCM yetu limefikia 'kuwashughulikia' wanaCCM wenyewe. Hakuna wapinzani wa kushughulikiwa. Inabidi tu kuwe na filamu ya Askofu Gwajima na Jerry Silaa. Wote hawa wana majimbo Dar es Salaam. Wote hawa wameonesha vituko kuelekea na mbele ya Kamati katika kuicheza filamu isiyotia hamu.
Askofu Gwajima alikataa kiti na kinasasauti. Akapata kiki yake. Jerry yeye alikataa kusindikizwa na askari kulekea mbele ya Kamati ya Maadili ya Bunge kwa kile alichokisema kuwa anajua anapokwenda na anazijua Kanuni za Bunge. Pia, akawasili na nyaraka na vitabu mujarabu vyenye majawabu yasiyo na tabu. Naye akatrend. Filamu ikaendelea.
Laiti kungekuwa na wapinzani Bungeni, Spika Ndugai angefurahi sana kucheza 'picha' zake na kutamka maneno yake mbele ya Wabunge. Angeonesha mabavu yake kwa kila mtanzania. Wapinzani wamekosekana. Sasa ni CCM dhidi ya CCM. Ni kama fisi kula fisi mwingine. Spika atakuwa anajuta kukosekana kwa CHADEMA Bungeni.
Askofu Gwajima hakamatiki?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mwanza Mjini)
Kulingana na kikichotokea wakati na baada ya uchaguzi wa mwaka jana, CHADEMA 'haina Wabunge' katika Bunge la sasa. Ndiyo kusema, Spika hana 'targets' zake za kuzishughulikia. Ghadhabu zake zinakosa pa kujitokeza na kuzifaidi. Sasa ameamua kuanzisha maigizo yasiyo na maazigo.
Bunge la CCM yetu limefikia 'kuwashughulikia' wanaCCM wenyewe. Hakuna wapinzani wa kushughulikiwa. Inabidi tu kuwe na filamu ya Askofu Gwajima na Jerry Silaa. Wote hawa wana majimbo Dar es Salaam. Wote hawa wameonesha vituko kuelekea na mbele ya Kamati katika kuicheza filamu isiyotia hamu.
Askofu Gwajima alikataa kiti na kinasasauti. Akapata kiki yake. Jerry yeye alikataa kusindikizwa na askari kulekea mbele ya Kamati ya Maadili ya Bunge kwa kile alichokisema kuwa anajua anapokwenda na anazijua Kanuni za Bunge. Pia, akawasili na nyaraka na vitabu mujarabu vyenye majawabu yasiyo na tabu. Naye akatrend. Filamu ikaendelea.
Laiti kungekuwa na wapinzani Bungeni, Spika Ndugai angefurahi sana kucheza 'picha' zake na kutamka maneno yake mbele ya Wabunge. Angeonesha mabavu yake kwa kila mtanzania. Wapinzani wamekosekana. Sasa ni CCM dhidi ya CCM. Ni kama fisi kula fisi mwingine. Spika atakuwa anajuta kukosekana kwa CHADEMA Bungeni.
Askofu Gwajima hakamatiki?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mwanza Mjini)