Siri imefichuka Wachezaji wa Yanga Nahodha Cannavaro na Kessy wapigana wakigombea posho

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Habari iliyonifikia hivi punde kutoka katika chanzo changu kikubwa kabisa na ninachokiamini ndani ya Klabu ya Yanga kimenitaarifu kwamba kuna taarifa ambayo Wadau wa Michezo tunafichwa ila ukweli ni kwamba baada ya mechi ya Kirafiki ya juzi ya Yanga SC na Rhino FC katika Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi Mkoani Tabora kulitokea ' Ngumi ' baina ya Nahodha wa Yanga Nadir Haroub ' Cannavaro ' na Beki wa Kulia Ramadhan Kessy.

Sababu Kuu iliyopelekea kuwa na mpambano huo wa Ndondi usio rasmi na usio na mkanda ni pale ambapo Nahodha Cannavaro alipoamua kugawa ' Posho ' kwa Wenzie kwa kadri alivyokuwa akipanga Yeye hali ambayo iliondoa uvumilivu wa Beki Kessy ambaye aliamka na kutaka ajue kimepatikana Kiasi gani ndipo baada ya kutopata maelezo ya kutosha kutoka kwa Nahodha wake akaamua kumnyang'anya zile Hela ndipo Nahodha Cannavaro alipoamua nae kujibu mapigo wakapelekea ' Kudundana '.

Mara baada ya kutokea ' tafrani ' hiyo Viongozi wa Yanga FC na ' Benchi ' zima la Ufundi liliamua kulifanya hili Siri kubwa ili Mwandishi wa Habari yoyote asiijue lakini kumbe hapo hapo wakasahau kwamba GENTAMYCINE popote pale nina ' Vyanzo ' vyangu ambavyo huwa havinifichi kitu na hatimaye leo ' nimepenyezewa ' hii.

Aidha chanzo changu hicho Kikubwa kilichopo ndani ya Klabu ya Yanga kimeniambia kwamba kwa sasa hali ya Kiuchumi / Kipesa ndani ya Timu ni mbaya sana na kwamba Wachezaji wamekosa ' morale ' na wamesikitishwa mno na taarifa wanazozisikia kutoka katika Vyombo vya Habari mbalimbali kwamba aliyekuwa Mfadhili wao Manji amerudi wakati siyo kweli na kwamba Uendeshaji wote wa Timu kwa sasa unatokana na Timu Kukopa Pesa kutoka kwa Makampuni na watakatana taratibu na kwamba si kweli kwamba Yusuph Manji amerudi Yanga rasmi.

Haya sasa nimeleta hii taarifa huku nikimsubiri kwa hamu sana Msemaji wa Yanga FC Dismass Ten aikanushe kisha niweke ' hadharani ' bomu lingine ambalo linakaribia kupasuka ndani ya Yanga na ambalo naamini Wanachama wake wakilisikia sasa hivi hapo Kaunda Jangwani ' bakora ' zitaanza kutembea na ' Kitanuka '. Hakuna kinachoendelea au kitakachoendelea ndani ya Yanga GENTAMYCINE nisijue au nisikipate hivyo wana Yanga SC popote pale mlipo acheni kuwa na viherere na kuwashwawashwa mno na masuala ya Simba SC wakati nyie ya kwenu ni mengi na yanawashindeni.

Nawasilisha.
 
Adui yako muombee, njaa swahiba [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Asante kwa taarifa mkuu

Habari ndiyo hiyo Mkuu na hakikisha unaichukua kama ilivyo kwani nimeileta kama nilivyopewa na sijaichuja kokote ila namsubiria tu Msemaji wao Yanga SC Dismass Ten aikanushe ili nimdhihirishie kwamba japo Mimi ni mwana Simba SC tena lia lia / kindakindaki lakini nazijua habari za ndani za Yanga pengine hata kuliko ninavyojua habari za ndani za Klabu yangu pendwa, bora na kipenzi cha Mwenyezi Mungu na Malaika wake wote Simba Sports Club.
 
Ile habari uliyoileta humu kuhusu mambo yaliyokuwa yanafanyika ndani ya jengo lile na ukatusihi tumuachie Mungu hadi ikazua taharuki humu iliishia wapi!?
 
hapa mimi na wewe tunapopishana kwa nini usihamie yanga! kwa kuwa unaweza kuwa msemaji wetu mnzuri

Mkuu kote nimekubaliana nawe ila kuniambia nijiunge na Yanga SC nadhani utakuwa umenikosea mno adabu kwani Klabu ninayoichukia kuliko hata ninavyomchukia Shetani Lucifa ni Yanga SC na kama patatokea ' gaidi ' yoyote mkubwa akitafuta Mtu wa kwenda ' Kujilipua ' pale Makao Makuu kwenu Kaunda Mimi GENTAMYCINE nitakuwa ' radhi ' kabisa nipoteze maisha yangu na Jengo lote la Yanga lipotee na pale Jangwani paharibike kabisa.
 
Japo siiiamini kivile sana mkuu
 
Hivi wewe si ndio yule alietuambia kua FIFA watawapa mbumbumbu kombe?nauliza tu

Hapa tunaongolea ' ngumi ' zilizopigwa huko Tabora baina ya Nahodha wenu Nadir Haroub ' Cannavaro ' na Beki Ramadhan Kessy na siyo hayo mengine uliyoyauliza sawa? Namsubiri kwa hamu mno Msemaji wenu Yanga SC Dismass Ten aikanushe hii ili ' nikinukishe ' au ' nikiwashe ' tena kwa taarifa nyingine ambayo ndiyo itachafua kabisa hali ya hewa huko Jangwani. Namsubiria kwa hamu sana!
 
Angalia unakoelekea mkuu sio kuzuri ukileta taarifu usilazimishe watu waamini.Hatujasahau ulimtabilia jamaa Fulani kifo lakini bado mzima sijui ndio utabili unaendelea
 
Japo siiiamini kivile sana mkuu

Na bahati nzuri au mbaya hakuna mahala nimeandika kwamba unatakiwa uiamini na humu JF hatuna utaratibu wa kulazimishana tuamini ' mabandiko ' yetu. Kama una namba za Msemaji wa Yanga SC Dismass Ten tafadhali nakuomba umwambie mbona anachelewa kuikanusha au kuikubali hii taarifa? Tatizo nini?

Na mpaka kuelekea tarehe 28 October, 2017 katika ile Mzizima Derby au Dar es Salaam Derby au Ilala Derby au Tanzania's Derby au East and Central Africa Derby ya Simba na Yanga ' tutawateseni ' sana Kisaikolojia wana Yanga SC na kupelekea ' kuchanganyikiwa ' vibaya hatimaye kufungwa magoli mengi na Simba SC yangu. Kuanzia sasa hadi hiyo siku ni ' ' fitna ' tu kwa kwenda mbele. Kwa siku hizi zilizobaki wana Yanga SC ' mtanisamehe ' tu kwani nina ' Jukumu ' kubwa la kuwaharibuni ' Kisaikolojia ' hivyo Kipele kimempata Mkunaji.
 
Angalia unakoelekea mkuu sio kuzuri ukileta taarifu usilazimishe watu waamini.Hatujasahau ulimtabilia jamaa Fulani kifo lakini bado mzima sijui ndio utabili unaendelea

Nimtabirie Mtu ' Kifo ' Mimi nimekuwa Israeli mtoa roho? Hebu nitake radhi upesi sana Mkuu.
 
do! tehe tehe... afadhari angalau likitokea hatutaangaika na wasio julikana ni wewe mzimamzima tunakufuata!
 
Hahaaa haya kiongozi sorry Ila utakuwa ushakumbuka.Bas tufunike kombe mwana haramu apite.

Umeshasamehewa tayari baada ya kuomba radhi. Haya sasa tuendelee na suala letu la ' Kupigana ' kwa Nadir Haroub ' Cannavaro ' Nahodha wa Yanga SC na Beki Ramadhan Kessy ' wakigombea ' posho baada ya mechi yao ya Kirafiki na Rhino Rangers ya Tabora hivi karibuni. Yaani leo hii Wachezaji wa Timu ya Kimataifa wanafikia hatua ya ' Kudundana ' kwa ajili tu ya ' Posho ' ambayo nasikia ilikuwa wagawane Tsh 9,700/ kwa kila Mchezaji wa Yanga SC aliyekuwepo pale ila Cannavaro akataka awape Wenzake Tsh 3,200/ tu na zingine ' achikichie ' mfukoni. Vipi tumwombe Mo Dewji awasaidieni na atawadai kidogo kidogo / taratibu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…