Rozela
JF-Expert Member
- Jan 5, 2024
- 845
- 2,235
Baada ya mahojiano ya watumishi wa Umma 83 wa kada za ualimu, uuguzi, ,aafisa kilimo na watendaji wa kata tumebaini kitu fulani ambacho kimetushangaza kidogo.
Hao 83 ni wale ambao wamefanikiwa sana katika biashara japo ni watumishi wa umma tuliwapata kama sampuli katika mikoa 15 ya Tanzania bara. (Tunajua wako watumishi wengi zaidi wenye mafanikio makubwa ambao hatuku wahoji)
Biashara wanazofanya hawa 83 ni
1. Ufugaji wa kisasa, hapa nazungumzia ufugaji sio majaribio ya ufugaji.
2. Mashamba makubwa na mitambo ya kilimo na kuchakata mazao.
3. Nyumba za kulala wageni zenye hadhi mbalimbali na restaurants.
5. Biashara ya maduka ya vifaa vya ujenzi.
6. Maduka makubwa ya vinywaji na vyakula.
7. Vituo vya afya na maduka ya dawa.
Kati ya 83 tulio wahoji, 22 waliwahi kuacha kazi zao serikalini kwa miaka kadhaa kisha wakarudi (zamani inaelekea hili lilikuwa jambo rahisi) na walipo rudi hawakushikika kimaendeleo.
Je, kuna uhusiano gani kati ya kuacha kazi na kufanikiwa mara baada ya kurudi kazini? Hawa 83 ni kwamba tulikuwa tunatafuta success story zao tukabaini 22 kati yao waliwahi kuacha kazi na kurudi tena.
Je, walipotoka nje ya mfumo waliona nini ambacho kiliwarudisha kwenye mfumo? Au ndiyo wale watu wa mfumo ambao hupaswi kuwaiga? Wao wanadai walirudi sababu ya changamoto za maisha ila kwanini waliporudi walifanikiwa sana?
Hao 83 ni wale ambao wamefanikiwa sana katika biashara japo ni watumishi wa umma tuliwapata kama sampuli katika mikoa 15 ya Tanzania bara. (Tunajua wako watumishi wengi zaidi wenye mafanikio makubwa ambao hatuku wahoji)
Biashara wanazofanya hawa 83 ni
1. Ufugaji wa kisasa, hapa nazungumzia ufugaji sio majaribio ya ufugaji.
2. Mashamba makubwa na mitambo ya kilimo na kuchakata mazao.
3. Nyumba za kulala wageni zenye hadhi mbalimbali na restaurants.
5. Biashara ya maduka ya vifaa vya ujenzi.
6. Maduka makubwa ya vinywaji na vyakula.
7. Vituo vya afya na maduka ya dawa.
Kati ya 83 tulio wahoji, 22 waliwahi kuacha kazi zao serikalini kwa miaka kadhaa kisha wakarudi (zamani inaelekea hili lilikuwa jambo rahisi) na walipo rudi hawakushikika kimaendeleo.
Je, kuna uhusiano gani kati ya kuacha kazi na kufanikiwa mara baada ya kurudi kazini? Hawa 83 ni kwamba tulikuwa tunatafuta success story zao tukabaini 22 kati yao waliwahi kuacha kazi na kurudi tena.
Je, walipotoka nje ya mfumo waliona nini ambacho kiliwarudisha kwenye mfumo? Au ndiyo wale watu wa mfumo ambao hupaswi kuwaiga? Wao wanadai walirudi sababu ya changamoto za maisha ila kwanini waliporudi walifanikiwa sana?