Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Mshambuliaji wa Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini raia wa Uruguay Gaston Sirino ,30, ameeleza kusikitishwa kwake kwa vilabu vya Al Ahly na Mamelod kuchelewa kufikia muafaka wa uhamisho wake.
“Naumia na ishu ya Mamelod Sundowns kushindwa kutimiza ndoto yangu ya kujiunga na Al Ahly, natumaini pande zote mbili watafikia makubaliano” Sirino
Sirino alikuwa anashinikiza kujiunga na Al Ahly kwa muda sasa, uwepo wa Kocha Pitso Mosimane ndani ya Al Ahly akitokea Mamelod Sundowns ndio kunachochea zaidi, Sirino bado ana mkataba wa miaka minne Mamelod.