Sitaki kuamini kuwa pesa ina nguvu kuliko sheria

MAHELO. E.B

Member
Joined
Aug 13, 2013
Posts
27
Reaction score
6
Inasikitisha, watuhumiwa dhidi ya MAUAJI ya Stephano Bahati (14/05/2010), aliyekuwa Katibu wa CCM kata ya Isamilo jijini Mwanza wote wameachiwa huru. Kibaya zaidi aliyekamatwa (Jumanne Osca) akikimbia baada ya mauaji hayo nae kaachiwa huru baada ya Jaji kukataa ushahidi wa Mkemia wa serikali kuwa damu iliyomwagika ofcn alipochomewa kisu marehemu hadi kufa ilikuwa inafanana na damu iliyokuwa kwenye nguo ya muuaji (ndugu Jumanne Osca) pamoja na mnuso wa mate yake.
Kesi ilimhusisha aliyekuwa Meya jiji la Mwanza (Biyondo) baada ya bwana Jumanne Osca kudai kuwa alikodiwa kuua kwa ahadi ya kulipwa donge nono la pesa.

Baada ya Jaji kuwaachia huru imekuwa kama tamthilia na kusababisha gumzo kuanzia ndani ya hiyo Mahakama kuu iliyopo Jijini Mwanza hadi maeneo mbalimbali ya mjini kati.
Wananchi wengi wamesikika wakisema wajipange kuiadhimisha kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa (Mwl. J.K. Nyerere) wakidai alizikwa na sheria zote za nchi hii. Sheria zilizobaki ziko chini ya sheria mama iitwayo MONEY LAW (sheria pesa).
 
Naamini tena kwa asilmia mia kwa tanzania pesa ina nguvu kuliko sheria. Kuanzia police mahakama. Wote mbele ya pesa sheria mfukon.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Hiyo kweli kiongozi. Kwa hali hii ni hatari. Tutafika ila tutakuwa tumechoka sana kwani ipo siku sheria itasimama kama sheria.
 
Anyway, no research no right to speak. Chunguzeni kwanza, na Mnaweza kukata rufaaa.
 

Si ajabu hili maana sheria ya ushahidi inatawaliwa sana na technicalities, upande wa jamhuri wajipange na kukata rufaa.
 
kweli ndugu, jana watumiwa wameachiwa huru, kila mtu anajua wahusika waliua lakini jana sheria imepindiswa na watumiwa walioachiwa walifanya sherehe kubwa.
 
Inatisha ndugu. Ila naamini kwamba malipo ni hapa hapa duniani.
 
I know that no research no right to speak. But for what happened on this case, even a blind one can comment something.
 
Unajua tusipende kila kitu tuwe watu wa kutanguliza hisia badala ya fikra,mahakamani ushahidi ndio kila kitu,ushahidi ukiwa na mapungufu au usipokamilika kisheria basi usitegemee kushinda kesi,hata kama Jaji alikuona wakati unaua bt kama hakuna ushahidi unaachiwa huru....so lets be curious kidogo wakuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…