Sitaki kutukanwa, nataka nishauriwe

Je mkeo akikuomba kupata mme wa pili utakubali? maana mapenzi yanauma sana hasa unapofahamu kwamba muda huu yupo kwa naniii.
 
Heheheee nilijua tu huwezi.



Kwamba kuna baadhi ya mambo ambayo watu wengi huwawia vigumu, hiyo ni kweli. Kwa hiyo nimekuelewa.




I say hi too. Nataka nimnunulie personalized sipper cup ya Disney ila nataka kujua favorite Disney character wake...

huyu bado sijajua atapenda character gani maana bado kila kitu kwake ni mshangao.
Tumwache ushamba umtoke ndo nitakwambia favorite wake ili hata ukimnunulia aweze kukithamini.
 
kwani akioa kuna shida gani jamani?
Mbona mwajijaza taabu za bure?

Aoe tu mtu mwenye quality za kuosha, sio alete Asha Ngedere nyumbani.
 
Naam! Kwani nina wivu kukaa nyumba za kupanga ni hatari na humu ndani ya madaladala michezo ya kupeana namba za simu hupendwa sana!

Na hata namba ya simu ya huyo mwandani wako, hakikisha inasajiliwa kwa jina lako...laini ikipata matatizo unaenda ku-renew mwenyewe; otherwise, ukiogopa namba yake kuitoa kwenye daladala, lazima akaiache kwa brazamen wa customer care pale tigo!!
 
ongeza tu mkuu mradi uwatimizie wote kusiweko na malalamiko
 
USIOE kisa dini,hio dini ambayo inaruhusu mwanaume kuwa na wake wengi na si mwanamke kuwa na waume wengi HUONI KAMA HAISMAMII HAKI???? ingekuwa inasimamia haki ingeruhusu pia na mwanamke kuwa na waume wengi!

Haki kwako wewe ni ipi kwani pale wanawake wanapopewa viti vya upendeleo ndio wewe unaita haki? Haki na upendeleo ni vitu viwili tofauti. Kama wewe uliona ni sawa kpendelewa kwanini useme kupendelewa kwa dini hakuzingatii haki. Halafu bibi yangu kwani wewe ulijiamulia kuwa mwanamke? Kwanini hupeleki malalamiko kwanini wewe tu ubebe tumbo la mimba na mwanamme asibebe. Tafadhali nishauri yenye kuwa ndani ya uwezo wetu na tuache kulaumu amri za Mungu!
 
Upuuzi, haya ni maamuzi yako binafsi ambayo hayatuhusu!

Nahisi wewe ni mpuuzi iwapo unahangaika muda wako kujali mambo ya kipuuzi! Ulimwengu ni mkubwa na hii siyo thread pekee iliyomo humu. tafuta yanayokuhusu na tuwachie upuuzi wetu la ni mwanachama endelea!
 

Cheusi mbona unanifanya kama hao wanaume wenye roho mbaya? Nimesema ndowa inatufunga kuamua kubadilisha wanawake hata kama kila siku wanazaliwa wazuri basi na sio naowa kwasababu natafuta wazuri(nitapata tabu kama nina lengo hilo).
Hili la kuongeza mwengine huwezi kunizuia kwani mimi sitegemei kitendo cha ndowa (Kuingiliana) kuwa ndio kila kitu kwangu. Inawezekana kuna mengine na wewe mwenyewe umekiri kuwa kuna sababu zilizowekewa kuowa wake hadi wanne. Unataka kuamini kuwa mimi simo katika hao waliopewa ruhusa?
Kwenye dini kisisitizo ni kuowa wake wawili, watatu au wanne na ikiwa huwezi uadilifu basi owa mke mmoja. Sasa wapi palipotowa masharti hayo unayoyasema wewe? Iwapo ndowa ni mfumo mzima wa mahusiano katika jamii kwanini hili la mie kuowa ulielekeze kwenye hamu ya mwili?
Usiwe na waswasi iwapo wewe bado hujaolewa unaweza kuwa candidate kwani nitakapoamuwa kuowa nitafuata maagizo yote na kitoka nyumba nitatowa! Mke wangu hana sababu ya kunizuia nisiowe mwengine kwani haki aliyonayo inaishia pale anapokosa sababu ya kunizuia nisiowe.
 
hakuna mwanamke anayependa,wanaridhia baada ya kuona hamna jinsi,kwa mwanaume hamna u turn ndio afanyeje in short wanakubali shingo upande....mtu uliyempenda huwezi kumruhusu awe na mtu mwingine period.
Usifikiri watu wote wako sawa na wewe amabe hata maagizo ya Mungu unayatia dosari. Sasa kuna haja gani ya kuolewa si utowe tu kwa unaempenda kwani pana haja ya mkataba maalum kwenye aina ya mapenzi unayotaka wewe?
 
Ushauri wangu wa bure, ndoa ya pili au ya tatu ni ndoa ya utapeli au uwizi, keep in mind love is not enough to convince someone lazima kutakuwa kuna maslahi fulani yanatarajiwa from both side.

Hakuna mwanamke anayekubali kushare mume if there is nothing in return apart from love thats the fact.
 

Cheusi, haya ni malezi na mila tulizozooleshwa. Kwa mfano si kuna makabila ambayo wanawake wanaowa wanawake wenzao na kuwapagaza wanaume ili wapate watoto? Si kuna makabila kwanza unapiga ngwala na kubikiri ndio unapeleka posa? Si wazungu mwanamke anaweza akakukataa na kuondoka na mwanamme mwengine nawe ukabaki solemba usimfanye kitu?(Fanya Bongo uone).
Mimi naowa mke wa pili kwa vile dini yangu imenipa ruhusa na mke wangu kwa kufahamu hilo atakubaliana nalo huku akisisitiza haki zake zilizowekwa.Inashangaza kuwa unakubali sheria mama ya kuishi na mwenzio baada ya kuowana lakini unakataa kifungu kinachofuata na kudai kuwa sheria ni batili.
Cheusi unakumbuka Marehemu sofia Kawaw alifanyiwa maandamano kwa hili na wanawake walishiriki?
 
NN mim nilikuomba wewe ujibu kama wewe.UNGEMKUBALIA?

Ha Ha Ha! Hivyo hujaona wanaume wakawapeleka wake zao kwa mabosi? Hujaona wanaume hawaendi nyumbani kwanza kabla hawajawapigia simu wake zao ilikupewa ruhusa? Hujasikia wanaume wanaondoka nyumbani kutwa hawajaacha kitu nyumbani wakirudi wakafakamia pilau wala wasiulize kitu? Hebu kamuulize Busheke!
Hii si sawa na kuruhusu mume wapili?
 
Ngabu nilijua huwezi kukubali,hata ungesema ungekubali bado ningejua unadanganya,sbb najua haiwezekani.
Nakuomba utuambie kwanini wewe moyo wako umeona kwamba usingemkubalia.

Cheusi hata mimi ninaetaka kowa wa pili nisingemkubalia.Kwasababu hii ni out of context katika jamii yetu

 

Nitazingatia,tena ahsante kwa kunikumbusha hilo!
 
Kwani mmoja hakutoshi???? Au keshachuja kwani miaka 20 mingi ati!

Hanitoshi! Napenda mambo mengine yeye hayawezi au bora azidishe muda wake kunifanyia hayo ninayompendea yeye badala ya kugawa muda kwa mambo ambayo hayaniridhishi!
 

Cheusi sikulaumu lakini ulipaswa kwanza kuona huo uchungu wa kuolewa matara ndio ungeweza kujuwa kweli hilo jambo ni baya au vipi. Bado nakupa nafasi unifanyie majaribio mimi (kama hujaolewa) na baadae utajuwa kwanini wanawake wenzio wanaweza kukubali kile unachoona wewe huwezi. Jaribu kidogo haiumi, ukiona mambo magumu utaondoka!
 

Nauheshimu msimamo wako lakini nini tusi katika ulimwengu wetu wa sasa? Samahani, lakini kama kivazi chenyewe ni kuvionyesha hivyo vinavyoitwa matusi unafikiri dunia yetu ni ya kujali nani kasema nini? Angalia maslaha dada angu after all hakuna uhakika wa mtu chake peke yake dunia yetu ya leo. Tukiowana angalau tutakuwa tumehalalisha huo usasa wa leo.
 
Omba Mungu yasikukute! Unaonaje wale wanaojitundika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…