Sitta: Ageuka Jiwe (Amebadili kauli yake Wabunge viti maalumu)

Sitta: Ageuka Jiwe (Amebadili kauli yake Wabunge viti maalumu)

calory

Member
Joined
Apr 29, 2013
Posts
31
Reaction score
6
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amebadili kauli yake ya awali, kwamba katiba mpya iondoe viti maalumu kwa kuwa wabunge wa viti maalumu hawana umuhimu wowote.
Kauli hiyo ambayo aliitolea Busega mkoani Simiyu, na kunukuliwa na vyombo kadhaa vya habari, imekuwa inapingwa na wananchi kadhaa, hasa wabunge hao wa viti maalumu.
Juzi akiwa mjini Tabora, Sitta alikanusha habari hizo akisema zinalenga kumchonganisha na wabunge wenzake. Alienda mbali na kudai vyombo hivyo vinaathiriwa na washindani wake kisiasa, hasa wanaotafuta urais.
“Nimebaini kuwa upotoshwaji huo ni sehemu ya mkakati wa kundi la kisiasa ambalo kinara wake anatafuta urais huku akibebwa na marafiki matajiri,” alisema.
Kauli hii mpya ya Sitta inaweza kulinganishwa na kilichomtokea mke wa Lutu kwenye simulizi za Kibiblia, aliyegeuka jiwe la chumvi baada ya kugeuka nyuma kutazama mji wa Sodoma ukiungua, kinyume cha ushauri wa malaika na msimamo wake wa awali.
Sitta ambaye pia ni Spika wa Bunge wa zamani na mbunge wa Urambo Mashariki, alisema kuwa amebaini upotoshwaji huo ni sehemu ya mkakati wa kundi la kisiasa ambalo kinara wake anatafuta urais wa nchi kwa udi na uvumba.
Waziri huyo machachari ambaye amekuwa na kauli nzito dhidi ya wapinzani wake kisiasa, alisema kuwa katika uchunguzi wake amebaini upotoshaji mkubwa na wa makusudi juu ya mambo aliyotamka na kunukuliwa kuhusu wabunge kutotembelea majimbo na yale yaliyohusu hatima ya wabunge wa viti maalumu katika katiba mpya.
Kwamba amebaini kuwa mhariri wa gazeti hilo lililomnukuu anapokea malipo ya kila mwezi pamoja na bonasi kwa kazi maalumu kutoka kwa mwanasiasa mmoja japo ambaye hata hivyo hakumtaja jina.
“Njama hizi ni mwendelezo wa vita dhidi yangu kutoka kundi la wanasiasa nililolitaja ambalo limepania kununua urais wa nchi yetu,” alisema.

Source: Tanzania Daima
 
Baba: Mwanangu mbona umeamka alfajiri
kwenda shule, kulikoni?
Mtoto: Baba namuwahi mwalimu wa bagia.
Baba: Mjinga sana wewe, badala ya kuwahi
elimu, wewe unawahi bagia?
Mtoto: Baba, unajua kiukweli kabisa kuwa elimu
haina mwisho, ila bagia mwisho saa nne.
 
Wabunge wa viti maalum ni mzigo na janga kwa taifa!
 
Sitta na Slaa hawana tofauti. Wote wanasumbuliwa na magonjwa ya uzee.
 
inaonekana dr.slaa alikuchomolea ulipojipendekeza kwake dada,ch*pi inakupwaya kila unapomuwazia dr.slaa!!!mmeo ana miaka mingapi?

Unaulizia umri wa mume wangu ili akufanye nini? Mbona we hujawahi kutaja umri wa boyfriend wako?
 
Sitta yaani kuna watu kweli walikaa chini wakadhani Sitta ana maana yeyote ?CCM wote watu wa kucheza deals kuzidiana basi hakuna lolote .
 
Mimi nashindwa kumuelewa sita ana matamko mengi lakini naona kama yana umbea mwingi
 
Dr. Slaa alishasema huyu jamaa ni bonge la mnafiki na mtu asiye na msimamo.

 
Last edited by a moderator:
Teh teh, 6 bwana, c angemtaja tu mh. Ustadh Abdallah,..., kuzunguka huku kwote kwa nin? Unafiki mbaya sana!
 
sita anajikosha nini? Ukweli si ndo huo? Aache kuzunguka mbuyu na kuwapa ukweli wazee wa kulala na ndiyoooo bungeni
 
Back
Top Bottom