Sitta aondolewe uenyekiti bunge la katiba achaguliwe Kificho

Sitta aondolewe uenyekiti bunge la katiba achaguliwe Kificho

Stabilaiza

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2012
Posts
1,843
Reaction score
1,143
Mwanzo mbaya unamwisho mbaya. Sitta amedhihirisha kuwa hawezi kuliongoza bunge la katiba. Pamoja na kuwa ametengenezewa kanuni na watangulizi wake ambao waliongoza bunge la katiba vizuri bila kanuni, yeye ameanza vibaya kwa kuvunja kanuni zilizotungwa na kupititishwa na bunge hilo.

Napendekeza wabunge wa bunge maalumu wamwondoe na wamchague Mheshimiwa Pandu Amer kificho ambaye anaiweza kazi hiyo. Kificho yeye anafahamu kuwa katiba inapatikana kwa maridhiano kama mheshimiwa Mbatia na wengine walivyosisitiza mara nyingi. Ubabe wa Sitta hauendani na maridhiano na hivyo hawezi kuongoza bunge hilo. Baada ya kuchaguliwa Mh. Pandu Amer Kificho kuwa mwenyekiti, inabidi uchaguzi wa makamu mwenyekiti ufanyike ili apatikane mwanamke kutoka Tanzania bara.
 
Sita nachokifanya ni kuitafuta ikulu kwa hudi na uvumba. anataka sasa awapendeze ccm ili wampe ridhaa ya kuwa mgombea wa ccm.

Inasikitisha,
hatukutegemea.
 
Chadema mmeshaanza kulalamika.
 
Kanuni hairuhusu mwenyekiti wa muda kuwa mwenyekiti wa bunge maalum,nawe unataka kuvunja kanuni kama Sitta!!?
 
Sita nachokifanya ni kuitafuta ikulu kwa hudi na uvumba. anataka sasa awapendeze ccm ili wampe ridhaa ya kuwa mgombea wa ccm.

Inasikitisha,
hatukutegemea.
Hawezi kuipata ikulu kwa staili hiyo. Atakuwa very unpopular na wala katiba haitapatikana kwa ubabe wake kwa sababu katiba inatungwa kwa maridhano.
 
...hivi kanuni inasemaje endapo Mwenyekiti wa Bunge maalumu la Katiba aki-act Ultra Vires???????
 
Mgema akisifiwa, tembo hulitia maji! Sitta ameshindwa mwanzoni mwa safari tu, ingekuwa nchi za wenzetu angeshatolewa haraka sana!
 
Naona timu Lowassa mmeanza kumkwamisha 6,hongereni na mtapotea nyote.
 
Sita nachokifanya ni kuitafuta ikulu kwa hudi na uvumba. anataka sasa awapendeze ccm ili wampe ridhaa ya kuwa mgombea wa ccm.

Inasikitisha,
hatukutegemea.
Mimi namshukuru sana Mungu,kwa kutuonyesha dhahiri unafiki wa Sitta,huyu ndie alikuwa anajifanya eti mkombozi wa Watanganyika na walala hoi,leo hii Mungu katuonyesha Sitta ni mtu wa aina gani kupitia hili bunge la katiba.Ni dhahiri sasa Sitta kajipaka kinyesi mbele ya umma wa Watanganyika ,kama kupata kura huenda atapata kwao Urambo na si kwingineko,ni hatari kwa nchi kuongozwa na viongozi wanafiki,ambao wako tayari kuharibu taratibukwa manufaa yao.
 
What happenned exactly leo jamani? Mbona mimi sielewi? Maana tunasikia na kusoma mambo nusunusu tu humu pasipo ufafanuzi wa kina, mara Sitta mnafiki,kavunja kanuni,mara Warioba kazomewa na CCM mara vile nk,nk. Nini hasa kimetokea leo?

Ni kanuni gani specific Sitta alitaka kuivunja? Na kwa nini tunadhani alitaka kuvunja kanuni kwa makusudi? Ili iweje? Je nini kilitoea baadaye? Je ni kwa nini Warioba alizomewa (kama ni kweli)?
 
Huyo sitta anacho kitafuta nikuona damu ya wa tz ikimwagika mana bila ya katiba mpya itakayo simamia haki bas machafuko lazima yatatoke mana wa tz washachoka kuburuzwa
 
Back
Top Bottom