Sitta: DOWANS iliirithi Richmond isiyotambuliwa kisheria; Aapa kamwe hatakubali serikali kuilipa!

6 ni mpiga mayowe.
ccm wanajua sana kuwahadaa wa tz dah...
 
Yote tisa, swali moja tu kwa Sitta -Mbona mmeitambua Symbion walirithi wengine wa mitambo ile ile yenye historia ya Richmond??

Mkuu Mkandara, hebu twende taratibu hapa.

RICHMOND ilikua na MKATABA BATILI. DOWANS wakaja kuurithi huo MKATABA BATILI toka kwa Richmond kinyemela. Kumbuka hapa hakuna suala la Mitambo. Ni suala la kurithishana MKATABA BATILI. Ni matter of principle tu kuwa haramu haiwezi kuzaa halali. Na hapa ikumbukwe Mitambo ya DOWANS haikua mipya.

Serikali ilipotaka kununua hii mitambo kutoka kwa DOWANS, wakabanwa na Sheria ya Manunuzi ya Umma inayokataza serikali kununua mitambo
chakavu. Nadahani tuko pamoja mpaka hapo.

DOWANS wakaamua kutafuta mnunuzi wa MITAMBO yao iliyokuwepo Ubungo na sio Kampuni ya kurithisha MKATABA. Hapa ndio SYMBION ilipoingia na kuinunua MITAMBO kutoka kwa DOWANS. Ukumbuke hapa walinunua MITAMBO sio Kurithi MKATABA wa Dowans.


SYMBION ikawa approach UPYA Tanesco, na kuomba MKATABA MPYA ambao una best prices per KWH kati ya mikataba yote ya Tanesco. Tanesco wakaingia mkataba MPYA na SYMBION. Hapa mmiliki wa MITAMBO chakavu ni SYMBION ila anawauzia umeme Tanesco. Hivyo inachonunua TANESCO ni UMEME. Na ndipo mama Clinton alikuja kwenye uzinduzi wake.

Sasa hapa sijui ugumu wa kuelewa kilichotokea unatoka wapi?

Sijui tatizo ni kutokuelewa kilichojiri, au kuchanganya mambo, au kupotosha kwa makusudi au kwa vile ni Samuel Sitta.

Jamani, tujaribu kuwa fair na objective. Hao wasiokua wanafiki waliojazana huko CCM na hawaoni kama haya malipo
ya DOWANS ni wizi wa mchana sijui ndo ma hero wenu au vipi, mi sijui...
 

Mkuu with all due respect, naona wewe ndio umeonesha tabia ya usahaulifu na kuchanganya mambo hapa.

Kwanza kabisa kamati ya Mwakyembe ilikua SI kamati ya Rais, bali ilikua ni kamati ya bunge na ilijulikana kama KAMATI TEULE YA BUNGE Kuchunguza Richmond, chini ya uenyekiti wa Harrison Mwakyembe.

Halafu unajichanganya kusema bunge halikuruhusu mjadala wa kina. Kamati ilipewa nguvu za kufanya uchunguzi lakini haikuwa na nguvu za
kuenforce mapendekezo yake. Hapa ndio mihimili mitatu ya taifa inapoingia. Bunge lilifanya wajibu wake na waliscore A kwenye hili...

Kamati teule kwenye kumalizia ripoti yake ilikuja na mapendekezo 23, ambayo yalijulikana kama Mapendekezo ya Bunge, ambayo yalitakiwa yafanyiwe kazi na Serikali. Nadhani mkuu wa Serikali unamjua na unajua kipi kilifanyika au hakikufanyika. Sasa sielewi ulitaka Sitta kama Sitta afanye nini wakati Bunge halina Mahakama, halina polisi, halina vyombo vya kijasusi na kiuchunguzi? Sitta aliplay his part and beyond, alialmost cross the border kwa kutaka kumshurutisha Rais awe mkali zaidi kwa watuhumiwa wa ufisadi, alipotembelea bunge.

Besides vita dhidi ya ufisadi haiwezi kupiganwa na kushinda kwa kutegemea mtu mmoja tu ajitoe muhanga kila siku, na wengine tumekaa pembeni
na milk shakes zetu, as arm chair generals just busy pointing at the faults za frontline soldiers. Tunatakiwa kuwatia moyo badala ya kuwabeza!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…