Mkuu kufanikiwa kuwin market kunavitu vingi sana..
Ninaweza kukupa mfano mzuri, mimi nyumbani kwetu nikimuuliza mama na bibi kuhusu davido wanamfahamu na watakwambia wanamjulia skelewu na sanasana my number one... Wizkid hawamjui kabisaaa licha ya kuwa mwanamuziki mkuwa saana Africa.
Mwanamuziki kuongeza idadi ya mashabiki nchi tofauti ni tofauti kabisa na Jina kama jina kuongezeka kama kupata views kwasababu hapo views M14 hao unaweza ukaona ni asilimia kubwa wa Uganda na ndio wimbo wake pekee ulio hit saana kimataifa, na ukijaribu kuangalia hana wimbo mwingine wowote uliofika views hata millioni mbili youtube, unafikiri kwanini?????
Jose chameleone huwa anatoboa kwa kuangalia watu wanataka nini, kwanza aliamua kutumia kiswahili maana Silaha ya msanii ukiachana na yeye kama yeye ni Aina ya nyimbo zako zinachezeka? tune zake zipo poa? Na kwa àmbao hawazijui lugha yako je maneno yanaweza kuimbika kirahisi na kilamtu?
Ndio maana
diamond inakuwa rahisi saana kutoboa hata mtu asiyejuwa lugha ya kiswahili nyimbo zake zitachezeka na kuimba kuna maneno lazima hayawezi kumpita "Oh na na na, baby ooh" "my number one my sweetie sweetie" hata mtoto anaeanza kuongea hizi nyimbo atakuimbia vizuri mnoooooo, au hata mzee asiefuatilia mziki... Mwanamuziki unatakiwa ujuwe watu wanataka nin? Wimbo wa Roberto wa Zambia 'AMARULA' umetoboa Tanzania vizuri saaaana kaimba vitu vya ajabu ajabu ila in a simple way ambapo lazima ujikute umeimba pale unapooga japokuwa huijui lugha aliyotumia... vitu kama hivo kati ya mengi anayofanya kujipromote pamoja na kutaka attention ya kwanza kwa kufanya collable kuwafanya watu wasiokufuatilia wajaribu kuonja ladha yako afu uwateke kabisa