Siwapendi msiotandika vitanda vyenu!

nakwambia Nyamayao, kuna wababa wengine ni balaa kana jehanam, mtoto mpaka anakua hajawahi kuogeshwa, kubadilishwa nepi wala kulishwa na baba yake, baba akiwa amempakata akilia tu anakabidhiwa kwa mama haraka sana,


ndio hapo sasa, laiti mtu ungejua kuanzia mwanzoni mbele uendako kuna nini nadhani mwanaume wa hivyo ucngemtaka, hata mwanae? hapana aise.
 
kwani ili suala la mgawanyo wa majukumu watu wanalichukulia vp?au ndo majukumu ya mwanamke yanachanganywa kwenye majukumu ya mwanaume?au itafikia sehemu mwanaume analaumiwa kwa kutofanya majukumu ya mwanamke? au ndo tumeaanza?
 

Ulishawahi kusikia wimbo wa mume *****? Asikudanganye mtu bana. Mume atabakia kuwa mume, na mke atabakia kuwa mke. Thats why nyoka akiingia ndani mama haingii mpaka mzee aje afanye vitu vyake. Kama paa la nyumba linavuja baba atachacharika, kitasa cha mlango kimeharibika mzee atafanya vitu vyake au siyo? Banda la kuku sijui limefanyaje mzee anatafuta nyundo na vitu kama hivyo!

Mama ataendelea kuwa pambo la nyumba. Usafi hiyo ni sehemu ya kazi yake. Usafi wa nyumba na watoto, kupika na kupakua bila kusahau kufua na kumpa mzee ile huduma muhimu. Mtoto akiwa mchafu atakayesemwa ni mama, nyumba ikiwa chafu atasemwa mama nk nk.

Acheni baba aitwe baba na mama aitwe mama. Hakuka kitu bama au maba! FULL STOP!
 
mimi msimamo ule ule!mke wangu anapaswa kulijua hilo kwamba:
KUFUA
KUTANDIKA KITANDA
USAFI
KUPIKA
AND ALL DAMN DOMESTIC JOBS NI ZAKE

mimi kama mwanaume nina majukumu yangu!kufanya kila jambo ni kunikosesha muda wa kupiga TASKA NA KUTENGENEZA MARAFIKI
 
tatizo na kwamba watoto wanakosa mapenzi ya baba, yaani watoto jinsi wanavyokuwa wakubwa hata wanavyoongea na baba ni tofauti na anavyoongea na mama kwa sababu u close wao na kina baba una walakini, sio vizuri jamani...tuwatendee haki watoto
Hakuna lolote hapo kua na ukaribu na mtoto sio mpaka umbadilishe nepi!!!
 
Well said nsha kugongea ka thanx!
 



du kazi ipo.....
 
Hakuna lolote hapo kua na ukaribu na mtoto sio mpaka umbadilishe nepi!!!

Mpwa kaangalie senks nimekugongea kule. Leo mtazipata senksi zangu sana wapwa. Hii mada mmeitendea haki, ma-SHE wote wamesepa, kabaki king'ang'anizi nyamayao na mwenzie triplets. Hawa kwa taarifa yenu waume zao hata hawajui neti zinashushwaje, wanatuzuga hapa tu!
 

Bwashee kaangalie senksi ya hiyo red nimekugongea.
 
You can say it Again....nshakugongea!!
 
Sawa Mr. anaweza kutandika ila utandikaji wake ni tofauti sana na utandikaji wa Mrs.

Kama ni sanaa ya kutandika pamoja na kupamba kwa ujumla utaipata kwa kinadada.
 

haaa ndugu yangu wee, wababa wa siku hizi hata vi tool box hawana...nyumba hazina bisi bisi wala nyundo..kitasa kimeharibika, paa linavuja ataitwa wa pale mtaa wa pili aende kurekebisha...eti baba yupo bize na kazi
 
Haya nepi usimbadilishe na kumbembeleza akilia nako vipi???

Nimbembeleze? kama ana njaa maziwa ya kumnyonyesha ninayo mimi? Si mama ndio ana matiti jamani? Akilia ni kazi ya mama kumbembeleza na kumtimizia anachohitaji.
 
serengeti zinaongeza konfidensi kwenye ndoa!

Hahaha! Hasahasa kama ukipata chaji za mdudu au kokoto! Ukichanganya na valuu, atatandika kitanda mwenyewe kwa raha zake.
 

jamani jamani embu acha kusingizia wenzio..mwe!!!
 
Nimbembeleze? kama ana njaa maziwa ya kumnyonyesha ninayo mimi? Si mama ndio ana matiti jamani? Akilia ni kazi ya mama kumbembeleza na kumtimizia anachohitaji.

kumbe ndio hivi? kwa mtaji huu nimenyoosha mikono juu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…