Siyaelewi makato ya benki ya CRDB

Sasa wakiingia wake jamaa kuchukua flati si wataziona? au utawaambia wazee si mmejia flati, sepeni basi.

Labda ungeshauri kabisa huko ndani tuwekeje na zibaki salama.

Ila kweli ishu ya benki usiweke pesa utakazokuwa unachukua mara kwa mara, kuna siku utacheki salio hutaamini unachokiona.
 
hahaahhahahaaaa, CRDB gharamaaaa...tena makato ya ATM sio ATM yoyote tu, ukitoa ATM ya crdb bei sio mbaya, jipeleke katoe ya VISA uone, them days ilikuwa 3000, ukipachika tu, hatakama kuangalia salio siku hzi sijui cz niliwahama.

Equity ni bora kabisaaaaaa! tena kwa mida hii na ANKO ikienda 1000 tu roho inauma.
 
Nenda equity bank wako mwenge wana best service ever wan app yao kwanza kuangalia salio nibureeeee......hawana makato ya mwsho wa mwezi nakutoa atm ni mia 7...so far kwa wafanyabiashara it is the best choice
 
Hahaaa bora niendelee kutunza pesa zangu nyumbani.
 
Tatizo equity bank haipatikani kwa wingi kama Nmb
Nenda equity bank wako mwenge wana best service ever wan app yao kwanza kuangalia salio nibureeeee......hawana makato ya mwsho wa mwezi nakutoa atm ni mia 7...so far kwa wafanyabiashara it is the best choice
 
Kila baada ya miez mitatu benk huwa zinatoa reports zao...moja ya report zinaonesha minimum charges....so ni vizur ukawa unapata muda kipitia na kujua gharama mbali mbali mbali za kibenki.

Hata hvo...crdb ni zile benk zinaitwa tie1...sina hakika na spelling but maanake ni kati ya benk za class ya juu kidogo....katika nyanja nyingi ikiwamo usalama wa kimfumo na kimtaji...so kwa maneno mengine....ni sawa na kuchagua kutumia vogue..kama gari lako la kawaida....usilalamike kwann linakula mafuta kuliko ist.....zote ni gari ila ingine ni zaidi ya gari....ndivo zilivobenk pia
 
Chapchap akaunti 400 tu kila muamala unaofanya hakuna makato ya mwezi.
 
Hapa kuna kitu mnaficha au haukijui kama una card ya visa mastercad kuna hela mnakata sijui ya nini kama 6000 hivi
 
Kweli mimi nimegundua CRDB wamekuwa wanyangsnyi badala ya kutafuta pesa wao kwa wateja wao wanawaibia
 
Kuna gharama ya kuendesha visa na tembo card wanakukata tuu
 
Nliwahi kutunza hela yangu kW ajili ya field kama miez minne SKU niloenda kuichukua skuamini kwakweli ...niliamua kuhama kabisa crdb
 
Ukitaka kutoa 1m, CRDB wanaweka 5000 tu hivyo inakuladhimu utoe 5times(Bank limit ni note 40 kila muhamala) na hivyo wanalamba 4,720/= ni wizi wa mchana.
 
Simu banking itumie tu kuangalia salio. Usitoe hela huko utafilisika fasta. Labda kama umepata shida isiyowezekana kwenda kwenye ATM.

Hata ukiangalia salio kwa simu banking unakatwa pesa pia, unaliwa kwenye salio na kwenye akaunt yako wanakata.
 
La haulah hawa jamaa ndio maana wanapata hela sana na faida kubwa sijuagi kama wanakata hizi huwa nachukua tu basi, nilikuwa na current account na savings account, ila current account wanakata sh 10,000 kwa mwezi huduma zingine sijawahi kukagua na sijui labda nichukue statement ya miezi 2 ndio ntajua, ila tatizo lingine nikiwekewa hela kutoka nje ya nchi exchange rate wanayoitumia ni mbovu sana haifai kabisa isitoshe wanakata sh 10,000. nikiwekewa hapa nchini yani ktoka mikoani kiwango mara nyingi ni mil 2 kwenda juu wanakata sh 10,000 yan nakatwa mimi kwa kuingiziwa huwa sielewi hii pesa kwa nini wasisubiri nitoe ndio wakate kweli nitahama nimewasoma sasa ntakuwa nimeshakatwa hela nyingi sana mpaka sasa hivi.
 
Hata NMB nilitoa laki 9 ikakataa nikatoa laki tano ikakataa ilibidi nitoe laki 3 mara 3 nikajiuliza kwanini kumbe wameweka kibiashara ili wapate ile service fee ya kutoa.
 
kwani hawa equity wanayo huduma ya sim banking?
Nenda equity bank wako mwenge wana best service ever wan app yao kwanza kuangalia salio nibureeeee......hawana makato ya mwsho wa mwezi nakutoa atm ni mia 7...so far kwa wafanyabiashara it is the best choice
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…