Siyo kila ugonjwa wa akili ni mapepo

Siyo kila ugonjwa wa akili ni mapepo

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2017
Posts
3,402
Reaction score
4,532
Nimeshawahi toa mada kama hii siku za nyuma.Kuna jirani yangu mtoto wake binti wa kidato cha pili anapatwa na mapepo kipindi flani flani.Kuna binti ya rafiki yangu naye miaka ya nyuma kama mitano akiwa kidato cha pili alipatwa na hali kama hiii.

Kuna mwingine tena hivyo hiyvo lakini sasa ugonjwa haupo tena ameshakuwa mkubwa na ameolewa huwa nimejiuliza sana ni kwanini hizi hali zinawakuta tu watoto wakike wanaokua?

Nikajiwa na wazo ni HYSTERIA.

Ajabu sasa wanamaombi wa dini hapa ndipo wanapopata dili kuwa ni mapepo hili jambo linani kera mno kuwa kuingiza waumini mkenge hapo nyumbani kila siku ni makelele ya maombi lakini mimi nimeshajua sababu.

Kuna siku aibu ilinitoka kidogo nikamuuliza huyo binti umeshawahi kutembea na mwanamme akaniambia bado kabisa nikaishia hapo nikatingisha kichwa.

Mtu mwingine akiugua malaria ikapanda kichwani nao wanaita mapepo kila kitu kumsingizia shetani iko siku shetani mbele ya mungu atasema jamani vingine sio mimi.

Kuna rafiki yangu mmoja mkristo aliniambia sisi wakristo tumesoma sana kuliko waislam lakini ajabu sasa waislam ni vigumu sana kuingizwa mkenge.

Sisi wakristo ni rahisi mno mfano akaniambia ona babu wa Loliondo alivyoingiza watu mkenge mpaka viongozi wakubwa wa kisiasa.

Kila kitu au tatizo watu hao wa hayo madhehebu kuita ni mapepo inanikera mno kuna mahali namkumbuka kiongozi mmoja wa na nchi yetu alisemaga nanukuu ''AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO'' mwisho wa kunukuu.

Huwa nawaza hivi akitokea muislam akajitangaza kuwa ni nabii watamfanyia nini?
 
Unapofanya tafiti usidhani solution uliyopata ndio ni bora zaidi, endelea na tafiti zaidi.
 
Sawa, Ila visa vingi ni vya kutengenezwa, mf. Kichaa kinavyoshamiri kuna mtu anavuta pesa ndefu, au mafanikio ya kiaina . Dunia Ina mambo hasa wake wanaojificha kwenye dini
 
Acha kuwapotosha mabinti wetu ndugu.Hayo ni mapepo tu full stop.Mbona kama ni kawaida isiwe kwa mabinti wote ambao hawajawahi kuzini/kufanya uasherati wasipate hilo tatizo?
 
Ufafanuzi tafadhari HYSTERIA ndio Nini wadau?
Hysteria is a term used to describe emotional excess, but it was also once a common medical diagnosis.kwa kiswahili msisimko ni ugonjwa wa akili lakini wa muda unapenda kushambulia zaidi wanawake hasa wanaoanza kubalehe.Umeshawahi kusikia story ugonjwa wa kucheka cheka kwa watoto wa bweni wa kike?
 
Acha kuwapotosha mabinti wetu ndugu.Hayo ni mapepo tuu full stop.Mbona kama ni kawaida isiwe kwa mabinti wote ambao hawajawahi kuzini/kufanya uasherati wasipate hilo tatizo?
kila binadamu na kiumbe ana nguvu ya kuhimili kitu na ndio maana kipindupindu kinaweza ingia sehemu wengine wakapata wengine wasipate.Hata hii Corona imeingia wako wanaokufa na wako wanaogua na wanatembea nayo lakini hawafi.

Sio mabinti wote lazima wapata kila mtu kuna jinsi mwili unaweza kuhimili jambo. I am talking from medical terms I am a dr by profession I know what i write i have met with this cases several time ninachotaka kuwaasa watu tu ni kuwa wasipelekee kila tatizo ni mapepo
 
Nimeshawahi toa mada kama hii siku za nyuma.Kuna jirani yangu mtoto wake binti wa kidato cha pili anapatwa na mapepo kipindi flani flani.Kuna binti ya rafiki yangu naye miaka ya nyuma kama mitano akiwa kidato cha pili alipatwa na hali kama hiii.
Kuna mwingine tena hivyo hiyvo lakini sasa ugonjwa haupo tena ameshakuwa mkubwa na ameolewa huwa nimejiuliza sana ni kwanini hizi hali zinawakuta tu watoto wakike wanaokua?
Nikajiwa na wazo ni HYSTERIA.
Ajabu sasa wanamaombi wa dini hapa ndipo wanapopata dili kuwa ni mapepo hili jambo linani kera mno kuwa kuingiza waumini mkenge hapo nyumbani kila siku ni makelele ya maombi lakini mimi nimeshajua sababu.Kuna siku aibu ilinitoka kidogo nikamuuliza huyo binti umeshawahi kutembea na mwanamme akaniambia bado kabisa nikaishia hapo nikatingisha kichwa.Mtu mwingine akiugua malaria ikapanda kichwani nao wanaita mapepo kila kitu kumsingizia shetani iko siku shetani mbele ya mungu atasema jamani vingine sio mimi.
Kuna rafiki yangu mmoja mkristo aliniambia sisi wakristo tumesoma sana kuliko waislam lakini ajabu sasa waislam ni vigumu sana kuingizwa mkenge.Sisi wakristo ni rahisi mno mfano akaniambia ona babu wa Loliondo alivyoingiza watu mkenge mpaka viongozi wakubwa wa kisiasa.Kila kitu au tatizo watu hao wa hayo madhehebu kuita ni mapepo inanikera mno kuna mahali namkumbuka kiongozi mmoja wa na nchi yetu alisemaga nanukuu ''AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO'' mwisho wa kunukuu.
Huwa nawaza hivi akitokea muislam akajitangaza kuwa ni nabii watamfanyia nini?
Hili tatizo linaitwa CONVERSION DISORDER zamani lilijulikana kama HYSTERIA! Ni tatizo linalowapata akina mama zaidi kuliko wanaume. Mwazoni liliitwa Hysteria likihusishwa na mfumo wa uzazi wa mwanamke lakini baadae ikagundulika sio na ikawa chanzo cha kubadili jina.

Tunapopata msongo wa mawazo (stress) ni lazima tuwe na mbinu (skills) za kukabiliana na huo msongo vinginevyo miili yetu itashindwa kujua ifanye nini na huo msongo. Kwa vile mwili haujui ufanye nini na huo msongo basi hubdilisha huo msongo kuwa maumivu (SOMATOFORM DISORDER maumivu mara ya kichwa, mgongo, tumbo, nk lakini vipimo hospitali vitaonyesha huna tatizo). au kubadili kuwa CONVERSION DISORDER.

Conversion au Hysteria ni kule kushindwa kuitawala misuli ambay tunaweza kuitawala (mfano, ninaweza kuamua kukunja mguu au ngumi kwa vile nina utawala juu ya misuli hiyo). Ninapopatwa na tatizo hilo nitashindwa kuitawala nitakuwa kama mtu aliyepooza au mwenye kiharusi! Inaweza fanya nishindwe kumeza kitu au hata kupoteza uono! Utaenda hospitali lakini watasema hawaoni kitu! Hawa wanaumwa kwelei lakini tatizo lao halielezeki kitabibu bali linaelezeka kisaikolojia! Namna nyingine ya hili tatizo ni kukosa nguvu na kuanguka (ikumbukwe kwamba, kama mazingira yako sawa, tatizo hilo "litaambukiza". Ndio maana tutasikia shule fulani watoto wanaanguka hovyo).
 
Kwahiyo chief unataka kuniambia kwamba watoto wa kike ambao hawapigwi pumbu ndo wanakumbwa na hii hali...majibu tafadhali
Zamani iliaminika hivyo lakini tafiti zimebaini kwamba sio kweli. It is stress related disorder.
 
kuna shule moja ya
Kwahiyo chief unataka kuniambia kwamba watoto wa kike ambao hawapigwi pumbu ndo wanakumbwa na hii hali...majibu tafadhali
shule nyingi za wanawake ,walikua wakiona hii.ishu kwa wanafunzi ,faster wanaita debate na shule za boys,na baada ya debate ni full kuwabambia,kwa nadhani sio lazima kumpiga mbupu,ata kuwashika shika,kukaa na boys,inakua ahueni kwao
 
Hysteria is a term used to describe emotional excess, but it was also once a common medical diagnosis.kwa kiswahili msisimko ni ugonjwa wa akili lakini wa muda unapenda kushambulia zaidi wanawake hasa wanaoanza kubalehe.Umeshawahi kusikia story ugonjwa wa kucheka cheka kwa watoto wa bweni wa kike?
nimekupata mkuu hilo ni kweli kabisa
😂😂😂
 
Back
Top Bottom