Siyo sawa kwa Shirika la Utangazaji la TBC, kukata matangazo mbashara ya Bunge na kutuletea matangazo mengine!

Siyo sawa kwa Shirika la Utangazaji la TBC, kukata matangazo mbashara ya Bunge na kutuletea matangazo mengine!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Imekuwa ni jambo la kawaida sana Kwa shirika la utangazaji la TBC, kukata matangazo mbashara ya Bunge na kutuletea matangazo mengine.

Kwa mfano hivi leo, weshakata mara mbili, matangazo mbashara ya Bunge na kutuletea matangazo mengine, likiwemo hili la sasa hivi la kuteletea semina ya viongozi wa JMAT wa mkoa wa Dar-es- salaam.

Shirika la utangazaji la TBC, linaendeshwa Kwa Kodi zetu wananchi wa nchi hii, Kwa hiyo sisi wananchi ndiyo tunapaswa kuwaeleza hao TBC ni kitu Gani muhimu tunachopenda kukitazama.

Kwa mfano leo, huko Dodoma, ndiyo tunategemea hotuba ya Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, ndiyo anatoa hotuba yake.

Hiyo ni hotuba muhimu sana Kwa Kila mtanzania, kwani hiyo hotuba ndiyo tutakayojua watanzania kama tunaendelea kukamukiwa zaidi Kwa upande wa Kodi.

Hiyo siyo mara ya kwanza, kuondoa matangazo mbashara Kwa TBC na kutuletea matangazo mengine.

Wiki iliyopita, Bunge lilikuwa na hotuba muhimu sana ya wizara ya Maliasili na utalii, lakini badala ya kutuonyesha hotuba hiyo muhimu, TBC walikata matangazo hayo na kutuletea viongozi wakifanya usafi wa mazingira!

Hivi shirika la utangazaji la Taifa TBC, linawezaje kuondoa matangazo hayo muhimu sana Kwa watanzania na kutuletea matangazo hayo mengine, yasiyo na maana kubwa sana kwetu watanzania??

Hata hivyo najua kuwa hata hayo matangazo ya mbashara ya TBC yamerudishwa na serikali hii ya CCM Kwa shingo upande.

Kwa kuwa katika utawala wa awamu ya 5, chini ya Mwendazake Magufuli, alishapiga marufuku Kwa TBC kuonyesha mbashara, matangazo hayo ya Bunge!

Najua kuwa shirika hilo haliko huru katika maamuzi yake, Bali matangazo yake yote ya vipindi, yanaamuliwa na kuratibiwa na hawa watawala wetu wa serikali ya CCM!

Ni vyema shirika hilo likaachwa kuwa huru, badala ya kuingiliwa katika shughuli zake za uendeshaji
 


USHAURI WANGU👆👆👆
Nadhani ushauri mzuri ila ni ngumu
 
Bunge halina mvuto
Ni Bunge ambalo halina mvuto??

Hilo Bunge ndilo linalojadili maisha yetu watanzania ya Kila siku, Kwa hiyo hatuna budi kulifuatilia Kwa kile kinachoendelea
 
Samahanu mkuu....
Ni bunge la nchi gani wanaonyesha🤔🤔
 
Imekuwa ni jambo la kawaida sana Kwa shirika la utangazaji la TBC, kukata matangazo mbashara ya Bunge na kutuletea matangazo mengine.

Shirika la utangazaji la TBC, linaendeshwa Kwa Kodi zetu wananchi wa nchi hii, Kwa hiyo sisi wananchi ndiyo tunapaswa kuwaeleza hao TBC ni kitu Gani muhimu tunachopenda kukitazama.

Hivi shirika la utangazaji la Taifa TBC, linawezaje kuondoa matangazo hayo muhimu sana Kwa watanzania na kutuletea matangazo hayo mengine, yasiyo na maana kubwa sana kwetu watanzania??

Hata hivyo najua kuwa hata hayo matangazo ya mbashara ya TBC yamerudishwa na serikali hii ya CCM Kwa shingo upande.

Ni vyema shirika hilo likaachwa kuwa huru, badala ya kuingiliwa katika shughuli zake za uendeshaji
Naunga mkono hoja, sio busara kwa TBC kukata matangazo muhimu ya Bunge na kutuletea live nyingine isipokuwa pale tuu inappbidi.

Kunapotokea mgongano wa events kati ya Bunge na shughuli za Ikulu, Bunge linakatwa.
Hili niliwahi kushauri.
1. Kwa vile Bunge session ya asubuhi ni just 90 min, toka saa 3:00 mpaka saa 4:30, then TBC isipokee live nyingine yoyote ya muda huo siku za Bunge.
2. Akija mtu au taasisi nyingine yoyote inataka live, wa schedule live yao baada ya Bunge.
3. Hata shughuli za live za Ikulu ziwe zinaanza baada saa 4:30.
4. Ila Rais anapokuwa kwenye ziara za ndani, ratiba zake za live zianze saa 4:30
5. Ila rais anapokuwa ziara za nje ya nchi, hakuna namna, and that is understandable.
P
 
Nitawaona TBC ni Vilaza wa kwanza Kama wataendelea kuonesha Hilo bunge la matahira wakati Kuna jambo la muhimu. Kwa Sasa ni Ruksa TBC kukata Hilo bunge na kuonesha watoto wakicheza mchezo wa rede.
 
Naunga mkono hoja, sio busara kwa TBC kukata matangazo muhimu ya Bunge na kutuletea live nyingine isipokuwa pale tuu inappbidi.

Kunapotokea mgongano wa events kati ya Bunge na shughuli za Ikulu, Bunge linakatwa.
Hili niliwahi kushauri.
1. Kwa vile Bunge session ya asubuhi ni just 90 min, toka saa 3:00 mpaka saa 4:30, then TBC isipokee live nyingine yoyote ya muda huo siku za Bunge.
2. Akija mtu au taasisi nyingine yoyote inataka live, wa schedule live yao baada ya Bunge.
3. Hata shughuli za live za Ikulu ziwe zinaanza baada saa 4:30.
4. Ila Rais anapokuwa kwenye ziara za ndani, ratiba zake za live zianze saa 4:30
5. Ila rais anapokuwa ziara za nje ya nchi, hakuna namna, and that is understandable.
P
Naunga mkono hoja zako Pascal Mayalla
 
Nitawaona TBC ni Vilaza wa kwanza Kama wataendelea kuonesha Hilo bunge la matahira wakati Kuna jambo la muhimu. Kwa Sasa ni Ruksa TBC kukata Hilo bunge na kuonesha watoto wakicheza mchezo wa rede.
Hahahahaha.......😁😅
 
Back
Top Bottom