Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,478
- 3,659
Kila nikipata muda huwa natazama hiki kipindi kinachorushwa katika EATV na host wake akiwa ni Allan Laki. Sina shaka na upeo wa huyu kijana maana maswali yake ya papo kwa hapo kwa wanafunzi yanatoa changamoto ya kutosha. Hofu yangu ni uelewa finyu mno wa wanafunzi ambao huwa wanakutana na maswali ya huyu kijana.
Ni vijana walio kati ya umri wa miaka 14 hadi 22 hivi. Ukiwaona kabla ya maswali ni vijana waliochangamka sana na wenye kujiamini. Confidence zao huanza kupotea pale wanapotupiwa swali la kwanza tu, mathalan tofauti kati ya trekta na katapila. Mwanafunzi anaweweseka. Glacier erosion ni nini. Mwanafunzi anaweweseka wakati amesoma hayo.
Wanafunzi hao ni werevu sana kwenye burudani lakini taaluma zao wako hoi mno. Nini kifanyike? Hili ni suala letu kujadili wote hapa.
Ni vijana walio kati ya umri wa miaka 14 hadi 22 hivi. Ukiwaona kabla ya maswali ni vijana waliochangamka sana na wenye kujiamini. Confidence zao huanza kupotea pale wanapotupiwa swali la kwanza tu, mathalan tofauti kati ya trekta na katapila. Mwanafunzi anaweweseka. Glacier erosion ni nini. Mwanafunzi anaweweseka wakati amesoma hayo.
Wanafunzi hao ni werevu sana kwenye burudani lakini taaluma zao wako hoi mno. Nini kifanyike? Hili ni suala letu kujadili wote hapa.