SKONGA: Kipindi 'kinachovua nguo' wanafunzi

Mazao ya kuporomoka kwa elimu chanzo chake ni Nyerere na vibaraka wake, nani alifuta masomo ya History na Geography mashuleni? na nani kayarudisha?

Naona umerudi kulaumu na kulalamika (sishangai), niilifikiri utanieleza hizo product nzuri zinazotengenezwa ulizozisema ghafla umerudi kwa Nyerere!!

Kwa mantiki hiyo wanafunzi hawaelewi hayo kwa sababu Nyerere alifuta History na Geography. Hebu tuendelee kwenye mjadala wetu kuhusu "best result" za walimu watakaokuja (achana na wa History na Geography kwa sababu Nyerere "aliharibu").
 
Imebidi nicheke. Unazungumzia hawa Walimu wa toleo la kipindi hiki!! Nina bahati ya kuishi nao ama kukutana nao..Ni msiba! Tena ukiongezea na ugumu wa maisha "product" zitakazotoka baada ya miaka 5 ni balaa mara mbili ya hili tulilonalo.

sijui FaizaFoxy kalishwa limbwata la aina gani na uongozi huu. Dada hasikii haambiwi. Hajui kuwa voda fasta ni zao la awamu hii ya nne? Hajui kuwa katika awamu hii waliofeli ndio wengi kuliko waliofaulu?
 
Last edited by a moderator:
Labda hujuwi mipango na mikakati ya elimu inavyokwenda sasa hivi. Big Results.

mkukuta, mkurabita, ari mpya..., maisha bora kwa kila mtanzania, vision 20-25, kilimo kwanza, vua gamba, na sasa big results now. Hadi muondoke madarakani tutashiba misamiati
 

Lol.... Ati wanafunzi na wazazi wao!
Google "answer" is at a touch of a thumb!
 
Waziri wao tu ana slip of the tounge mpaka hajui mambo ya muungano lol ila huyo mtoto wa tabora na mtemi ametisha halafu form iv anayependa history.
 
He he he, basi wewe ulikuwa msongo

Mie nilikuwa nikiona wanafunzi wa special skul nataka nibadilishane nao vimiminika, angalau nibahatishe mtoto mmoja kipanga.
Ilikuwa raha jamani khah!

dooh ..wee mwana weee!!
 
Wanafunzi wanajua majina ya kina Wema sepetu, Uwoya, Lulu, Cheni, Ngassa..n.k Lakini hata Jina tu la waziri wao wa Elimu hawalifahamu. c.cRaia Fulani , FaizaFoxy ,
 
sijui FaizaFoxy kalishwa limbwata la aina gani na uongozi huu. Dada hasikii haambiwi. Hajui kuwa voda fasta ni zao la awamu hii ya nne? Hajui kuwa katika awamu hii waliofeli ndio wengi kuliko waliofaulu?

Hao waliofaulu mwaka mmoja tu uliopita ni wengi kuliko wote waliokuwa wanasoma sekondari kipindi cha Nyerere. Kumbuka hilo.
 
mkukuta, mkurabita, ari mpya..., maisha bora kwa kila mtanzania, vision 20-25, kilimo kwanza, vua gamba, na sasa big results now. Hadi muondoke madarakani tutashiba misamiati

Kuondoka madarakani, tumpe nani aongoze? Slaa? au DJ? - Wewe kweli umeichoka hii nchi.
 

Hao waalim unawaona waona leo hii wabpvu ni zao la kuharibiwa elimu na Nyerere na vikaragosi wake. Subiri uone mfumo ulivyobadilishwa na uone miaka ijayo zao litakalotoka.

Kikwete amenza na mashule, kila moto awe na uwezo kusoma Sekondari. Hii haijawahi kutokea kabla yake ni rekodi ya pekee, shule zaidi ya 5000 za sekondato kwa miaka 7 tu. Linganisha na shule chini ya 2000 kwa miaka 45 ya Nyerere, Mwinyi na Mkapa.

Hali kadhali vyuo vikuu, zaidi ya 45 kwa wakati wake tu, linagnisha na vyuo visvyozidi 5 kwa miaka 45 ya hao niliowataja hapo juu.

Bado unalo?
 

Heri mliosoma kipindi hicho, leo shule hazina madarasa mwalimu mmoja wanafunzi mia, kama chalks tuu hakuna unategemea Daily News litakuwepo?

Program nyingi kwenye vyombo vyetu vya habari bado hazimjengi mwanafunzi, TBC walitakiwa wawe na channel ambayo ni maalum kwa vipindi vya sayansi, historia etc. Magazeti machache yenye education and technology pullouts hayafikii wanafunzi.

Naona kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na mfumo wa elimu utakao jumuisha matumizi ya mitandao na vyombo vya habari.
 
Huenda ukawa sahihi kwamba tulianguka wapi, kosa letu tumeshindwa kutengeneza na hali inazidi kuwa mbaya!

Hali inakuwa nzuri sana, nchi imebomolewa kwa miaka 45, kuiona ilivyo sasa ni muujiza wa Kikwete. Hilo anastahili kila sifa.

Leo hakuna asiye na fursa ya kwenda sekondari. Uliyajuwa hayo kabla ya Kikwete?
 

Kwa misukule tu. Ngoja siku Jerry Slaa akishika Urais uone kama kutakuwa na upuuzi huo.
 

Mimi na wewe na pengine wengine tulikuwa tunaangalia quality sio quantity. Hata kama watoto wote watapata elimu ya sekondari kama kichwani hamna kitu ni bure kabisa, afadhali hizo resources wangenunulia pembejeo za Kilimo angalau tuondokane na aibu ya njaa!
 

Hizo fikra zako ni finyu sana. Hakuna nchi duniani inawacha kusomesha watoto wake walio wengi na kusomesha watoto wachache ili ipate quality. Mass education ndio pekee inayoendeleza taifa kwa kuwa na wasomi na si vingine.

Ikiwa mawazo ndio kama hayo yako, tuna kazi, kazi kubwa sana ya kuwaelimisha watu kama wewe.
 
 

Wewe ndiyo umeonyesha ufinyu kabisa wa kufikiri. Sijasema uchache ndiyo "quality", nimesema hapa tunaongelea "quality" na siyo "quantity" unayoipigia debe.

Narudia: "Hata kama watoto wote watapata elimu ya sekondari kama kichwani hamna kitu ni bure kabisa, afadhali hizo resources wangenunulia pembejeo za Kilimo angalau tuondokane na aibu ya njaa!"

Jifunze kusoma bila kuhemkwa. Tulia
 

Tatizo lako kubwa ni huelewi unachokipinga ukiambiwa hivi unasema vile ukiambiwa vile unasema hivi.

Nakueleza hivi, watoto wote waliofaulu mwaka jana ni wengi kuliko wote walioingia sekondari wakati wowote ule kabla ya Kikwete. Jee umeelewa hapo?

Sasa fikiri ni vichwa vingapi viliachwa bila kupewa fursa na Nyerere, Mwinyi na Nkapa kwa miaka 45.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…