Elections 2010 Slaa: Matokeo yataishangaza dunia

Bila shaka Dr Slaa anamaananisha kura ya urais. Kwani akishinda hiyo si ndo amechukuwa nchi? Katika nchi za Kiafrika power iko Ikulu -- na siyo Bungeni. Mutharika alitawala Malawi miaka mitano with a hostile Parliament na kuleta maendeleo makubwa. Last year wananchi walimpa kura nyingi mno na upinzani ukatokomea kunakostahili.

Tusisahau pia Mrema mwaka 1995 alikuwa tishio kubwa sana kushinda kura ya urais hadi CCM wakaingia hofu, na kama siyo Nyerere kuingia kuwakampenia na pia kutumia faulo kubwa siku ya uchaguzi kupitia Tume yao ya uchaguzi katika mkoa wa Dsm ambako Mrema alikuwa na ngome kubwa CCM, huenda ingeaanguka.

Kumbuka pia wakati ule kulikuwapo ulazima wa mgombea wa urais kupata asilimia 50+ ili kushinda ama sivyo kuna re-run kati ya top two.
lakini kutokana na hofu hiyo kutoka kwa Mrema, wamebadilisha hiyo na kwamba Rais sasa anaweza kuchaguliwa hata kwa asilimia 30 tu ya kura, hata iwapo jumla ya kura za wapinzani wake watamzidi kwa kura! Hivyo ndivyo CCM inavyojihakikishia ushindi, na siyo kupendwa na watu.

Tatu, ajabu inaweza kutokea kwani wewe unaweza kupanga mambo yako, lakini Mwenyezi Mungu pia an mipango yake. Chochote kinaweza kutokea hapa katikati katika medani ya kisiasa kabla ya uchaguzi na kuleta mshgangao mkubwa. Ndo maana sasa hivi ukiwatonesha CCM kuhusu uifisadi wanalia hovyo kama watoto wadogo badala ya kukabiliana vilivyo na hoja hiyo. Sijui kwa nini wanaiogopa hiyo hoja -- mara maadili, mara matusi -- ilimuradi hawana nerve ya kuijibu kwa ufasaha.
 
kazi ndo imeshaanza tuko pamoja na chadema.....MUNGU IBARIKI CHADEMA MUNGU IBARIKI TANZANIA.................
 
Kweli wataushangaza dunia kwa kupata 10% ya kura zote,Padri ajiandae kurudi mizabahuni!
watu kama ninyi ndio watu hatari amabao kwa ufinyu wenu wa mtazamo mnazalisha fikra ovu na mbovu.
Nani kakwambia udini wa mtu una manufaa kwa taifa? nani kakwambia Dk Slaa akienda ikulu anakwenda kufanya kazi ya kanisa?
Wapo watu wangapi katika historia ya dunia hii wamefanya mabadiliko makubwa na ya kutiliwa mfano ilhali walikuwa na historia ya kuhusika na dini kabla?
Mbona Dk Lwakatare alivyopewa ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya CCM watu kama ninyi hamkusema ilhali alikuwa active leader wa kanisa lake?
Mbona Uongozi wa juu Tanzania bara na visiwani ni wa kiislamu lakini hakuna anayesema?
Nitakwambia ni kwanini. Sababu ya msingi ni kuwa hatuko interested na dini ya mtu, bali uwezo wa mtu huyo wa kutimiza matakwa ya Taifa kwa ujumla. Hata kama Sheikh Gorogosi angegombea leo na akawa na fikra na misimao thabiti ya maendeleo ya taifa hili tutampigia kura bila kujali yeye ni Sheikh! Tunajua akienda ikulu haendi kuhubiri uislamu. Hali kadhalika angekwenda Kadinali pengo ama hata Kakobe, hatutajali udini wala historia yake ya dini kwakuwa udini wake ni irrelevant to the issues on the table!
Tunaangalia uwezo wa mtu husika na dhamira ya chama chake!
Je akisema atakuwa mkali kwa watendaji wa serikali tukimtazama tunaona anadhamira ya kweli katika kutekeleza hayo?
Hilo ndilo jambo la msingi tutakalojiuliza tutakapokuwa tukitafakari kabla ya kupiga kura.
Kwa hiyo watu kama ninyi mnaohubiri dini za watu hampaswi hata kuishi, (sorry for being so harsh, but it is the fact). Imagine watu wa aina yako mnaweza kuleta dosari kubwa namna gani miachwa mzungumze na watanzania wengi wasiojua kupambanua mambo?
Tunasema hivi, tunawatazama wagombea na vyama vyote vinavyoshiriki ktk uchaguzi, tunawapima na kuwatathmini, na jibu tunalopata ni kuwa wapinzani wana nia na dhamira ya kweli kutuletea maendeleo na kutufikisha pale tunapotaka kufika.
CCM wanacheza michezo michafu, ni wala rushwa, wanaamini katika rushwa na kubwabwaja - ushahidi wa kura za maoni ulionekana wazi!
Ktika upinzani wenye bidii ni CHADEMA na CUF, hatutajali nani zaidi lakini tunahitaji mpinzani kuwa rais mwaka huu tupime!
Kenya walimpa mpinzani, tizama leo wana katiba mpya na siasa za nchi ile zimechangamka! Uingereza na Marekani hali kadhalika. Watu wanaoamini katika kuutumia unyonge wetu kwa manufaaa yao na familia zao na maswahiba zao hatuwataki na nikisema hivyo namaanisha CCM hatuitaki!
Kura zote safari hii kwa upinzani.
Kuna wale wanamkosoa mgombea mwenza wa CHADEMA kuwa ameishia darasa la saba, nawauliza: So what? Zuma wa Afrika kusini has never seen an inside of a formal class, kwa hiyo ukimfanyia tathmini utaona hakusoma, but he is talent, has charisma etc and he is in the driving seat of his country!
Tunataka sera wala sio bwabwaja za CCM. Tangu lini maendeleo yakahitaji kusimuliwa? Watu si wapo wanatakiwa kuyaona wenyewe? Nani anahitaji takwimu? Kumbe ndo maana mmeamua kufanya elimu yetu kuwa kichwa cha mwendawazimu ili tusielewe kuchambua na kupambanua mambo muendelee kututawala kwa rushwa na uongozi mbovu tena? Katu hatutakubali! TUMECHOKA, safari hii ni upinzani, kwa uchache wao tumeona matunda yao ktk bunge lililopita. Nawaasa wananchi, wabunge madiwani na raisi safari hii ni wapinzani. Na kwa mtazamo wangu ni DK Slaa anayefaa!
Toa mtizamo wako, fanya maamuzi yako! Alicho-accomplish Dk Slaa kwa resources alizokuwa nazo kama mbunge ni kingi kuliko alicho accomplish Kikwete na resources zote zilizokuwa ta his disposal kwa muda wa miaka mitano!
Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabariki watu wetu!
 
Marksman

Anything can happen,

Uchaguzi wa 1995 uligubikwa na mambo mengi sana lakini hata hivyo wapinzani wakapata 40% ya kura zote.
- wakati huo mfumo wa vyama vingi ulikuwa mchanga
- watu hasa wanawake walikuwa wanahofu ya kutokea vita refer picha za ITV
- Nyerere alikuwa msaada mkubwa kwa CCM
- vyombo vya habari vilipendelea chama tawala tofauti na sasa ambpo baadhi ya vyama vina magazeti yao
- dora, FFU ilikuwa inavuruga kampeni za wapinzani kitu ambcho hatukioni sasa mabomu yalikuwa nje nje
- vyama vingi vilikuwa havijaeleweka misimamo yao hivyo kuhujumiana vyenyewe kwa vyenyewe tofaiti na sasa vinaonekana
- ingawa Mrema alikuwa icon figure lakini bado watu walikuwa na wasiwasi naye tofauti na icon ya sasa Slaa ambaye ameonekana toka bungeni.
- Wakati ule hakukuwa na chama cha upinzani kilichokuwa na mtandao kama ilivyo sasa ambapo kuna vyama vina wabunge na madiwani
- CCM ya 1995 ni tofauti na ya leo iliyogawanyika

Kwa maelezo hayo naweza kukubaliana na Dr. Slaa kuwa anything might happen.
 
thanks mkuu i cant wait.... maana hawa jamaa walisha-procure ballot papers zamaani na saa hizi watakua wanachakachua kwa kwenda mbele

Mkuu ikiwa CHADEMA watajipanga kuchunga kura kama ilivyotokea tarime. CCM hawataweza kuchakachua!! Wakijipanga kwa wasimamizi hodari na wakali, yote yawezekana mkuu. I hope for better!!
 
Kelele za panzi hazimnyimu mtu usingizzzi


ngoja ajipe moyo mara Slaa anaamini kura atapata kutoka kwa watoto, vijijini ni sisimu damudamu

Vuvuzela wewe!! Huna jipya!!
 

well said
 

Kuuliza si ujinga mzee ulimaanisha Cardiovascular system?
 
Mkuu umenena.

 
Anything is very possible! Kura zitalindwa na wananchi na mawakala ambao hawanunuliki kama mimi na watu kibao hapa jamii forums naomba muombe kulinda kura zetu, matokeo yatangazwe vituoni na kupata jumla ya kila jimbo! Kama sheria inavyotaka, ukitokea usanii wowote nchi haita tawalika na uongozi wa chadema need to send clear message kwa tume ya uchaguzi kuwa damu ya watanzania itakuwa mikononi mwao if they try to rig an election, lazima kupiga mikwara mizitu kabla ya tukio lenyewe na chadema tutajiandaa kuzivaa combat na kuwashughulikia watakao leta any kind of conspiracy
 
CCM is not invincible. It can be defeated. Above all, the CCM Presidential candidate can and will be defeated this time around. It won't be the first time. Mkapa was defeated by Mrema in the 2005 elections, but some powerful players prevailed on the NEC to alter the results. This theft was divulged here by Invisible a couple of weeks ago. But he only confirmed what many of us had always known.

Chadema beat the vote riggers of CCM during the local elections in Tarime. It will beat them again in October. This is not wishful thinking. Tanzanians are sick and tired of CCM. They would like to have a fresh start. Fifty years of abject poverty is enough.

There is one query CCM cannot answer. Why have they ruled for fifty years without leading us to meaningful development? Do they think they can do in five years what they failed to do in fifty?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…