Slaa na Wenzake Kukamatwa ndani ya 3 months-Tambwe Hiza

Slaa na Wenzake Kukamatwa ndani ya 3 months-Tambwe Hiza

jmushi1

Platinum Member
Joined
Nov 2, 2007
Posts
26,329
Reaction score
25,263
Tambwe atishia CHADEMA

na Kulwa Karedia

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimetoa siri ya kuwapo mpango wa kukamatwa viongozi wa juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwa kuhusishwa na kifo cha aliyekuwa mbunge wa Chadema, marehemu Chacha Wangwe.

Siri hiyo ilitolewa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Propaganda, Tambwe Hiza, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Itirya.

Tambwe alisema viongozi hao wa juu, watakamatwa baada ya miezi mitatu, kwa madai ya kuhusika na kifo cha Wangwe.

Tambwe alitumia mkutano huo kuzungumzia kifo cha Wangwe na kukihusisha moja kwa moja na viongozi wa Chadema.

Kutokana na hali hiyo, Tambwe amewataka wananchi wa Tarime kuacha kumpigia kura mgombea wa Chadema, Charles Mwera, kwa madai kuwa chama hicho hakina dola na viongozi wake watasambaratika.

Katika hatua nyingine, CHADEMAimemwaga zaidi ya baiskeli 20 zenye thamani ya sh milioni 2.6 katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Tarime, ikiwa ni sehemu ya kurahisisha usafiri kwa mawakala wake, ili waweze kuwafikia wanachama kirahisi katika kampeni zinazoendelea.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi baiskeli hizo, makao makuu ya chama hicho mjini hapa jana, Mkurugenzi wa Kampeni na Uchaguzi, Msafiri Mtemelwa, alisema hiyo ni moja ya hatua ya kukabiliana na mbinu chafu zinazofanywa na wapinzani ambao wamekuwa wakipita na kutangaza kwamba chama hicho hakina uwezo.

“Tumeamua kuwawezesha viongozi wetu wa kata ambao tunaamini kwamba wao ndio wako karibu zaidi na wapiga kura wetu... hivyo tumeona vyema kuwapatia baiskeli hizo ili ziwawezeshe kuzunguka maeneo mbalimbali wakati huu wa kampeni,” alisema Mtemelwa.

Alisema hiyo ni moja ya hatua ya kuwajengea uwezo ambao utawawezesha kuwafikia kirahisi watu walioko maeneo ya vijijini, ambako usafiri wa magari umekuwa mgumu, kutokana na hali halisi ya kijografia iliyopo wilayani hapa.

“Huu ni mwanzo, tumejipanga vya kutosha kukabiliana na mbinu chafu zilizoandaliwa na baadhi ya wapinzani wetu ambao wanaonekana sasa wanaweweseka kwa kuandaa mbinu za kutaka kutuvurugia mwenendo wetu wa kampeni...naamini lengo letu litatimia tu,” alisema Mtemelwa.

Alisema mbali ya baiskeli hizo kutolewa sasa, pia zitatumika katika uchaguzi wa serikali za vitongoji mwaka ujao, hatua ambayo alisema itakuwa imewajengea uwezo wa kusambaza ujumbe maeneo mbalimbali kwa wanachama wao.

Naye Katibu wa chama hicho, Wilaya ya Tarime, Joseph Anthony, aliwapongeza viongozi wa chama hicho kutoka makao makuu kwa hatua ya kutoa baiskeli hizo ambazo alisema zitatumika kama zilivyokusudiwa kwa nia ya kurejesha jimbo ambalo lilikuwa likishikiliwa na marehemu Chacha Zakayo Wangwe.

Alisema baiskeli hizo zitatumika zaidi maeneo ya vijijini ambako ndiko kuliko na wapiga kura wengi, ambao wamekuwa hawafikiwi kwa usafiri wa magari na badala yake husababisha chama kukosa kura kutoka kwa wanachama wake.

Kuhusu kampeni zinazoendelea hivi sasa, Mtemelwa alisema zinaendelea vizuri licha ya vikwazo mbalimbali ambavyo wamekutana navyo, hasa kutoka kwa Jeshi la Polisi ambalo limekuwa likishindwa kuwachukulia hatua baadhi ya watu ambao huripotiwa kwao.

Alisema mara baada ya kufanya mazungumzo ya kina na viongozi wa jeshi hilo jana, wanaamini kwamba hali itabadilika na kuona haki inatendeka kwa kila chama ili kufikia malengo yaliyokusudiwa hadi siku ya uchaguzi Oktoba 12, mwaka huu.

Katika hatua nyingine, Chama cha TADEA, na UPDP, kimelaani vurugu zinazoendelea katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime na kwamba endapo hali ikiendelea hivyo, kuna hatari ya uchaguzi huo kutofanyika au kuwa uwanja wa mapambano.

Wakizungumza katika mkutano wa pamoja kwa nyakati tofauti uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl, jijini Dar es Salaam jana, Rais wa Tadea, Lifa Chipaka, alisema kuwa vurugu hizo zinachochewa na wanasiasa wenyewe wawapo kwenye mikutano ya kampeni.

Alisema kuwa kila chama kimekuwa na kauli za uchochezi, lakini alilaani kitendo cha Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Mtikila kupigwa, huku baadhi ya viongozi wa CHADEMA, wakiipongeza hatua hiyo.

“Mimi nimeshangazwa sana na kauli ya Zitto Kabwe, kusema kipigo cha Mtikila ni sawa, kwani amezidi kuropoka, hii si sahihi, hatutarajii vyama vya upinzani vishabikie mmoja wao kupigwa,” alisema Chipaka. Naye Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa, alisema kuwa kuna uwezekano mkubwa wa Tarime kuwa kama Zanzibar ilivyochafuka mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2000, ambapo zaidi ya watu 30 waliuawa na wengine kukimbilia Kenya kutokana na machafuko ya kisiasa. “Sisi hatutaki taifa lipoteze amani, lakini ndiyo maana tunakemea hali hiyo.

Yanayotokea Tarime yasipodhibitiwa, yatatokea tena sehemu nyingine. Sasa hii ni hatari,” alisema Dovutwa.
 
Tambwe anasema watakamatwa baada ya miezi mitatu...Hii ni karata ya kisiasa kwasababu baada ya miezi mitatu uchaguzi utakuwa umekwisha....Kwanini wasikamatwe kabla ya uchaguzi ili tujuwe ukweli?
Mimi naona uchaguzi huo wa Tarime usimamishwe hadi hapo ukweli utakapowekwa wazi ili kuwa protect wananchi.
Wananchi wa Tarime waruhusiwe kuujuwa ukweli kabla hawajapiga kura kwa mtu asiyependa maendeleo yao.
 
Tambwe anasema watakamatwa baada ya miezi mitatu...Hii ni karata ya kisiasa kwasababu baada ya miezi mitatu uchaguzi utakuwa umekwisha....Kwanini wasikamatwe kabla ya uchaguzi ili tujuwe ukweli?
Mimi naona uchaguzi huo wa Tarime usimamishwe hadi hapo ukweli utakapowekwa wazi ili kuwa protect wananchi.
Wananchi wa Tarime waruhusiwe kuujuwa ukweli kabla hawajapiga kura kwa mtu asiyependa maendeleo yao.

Tambwe kumbe ni mtupu namna hii ? Do we have a room for scare politics ?Tarime sawa na Moshi mjini .Tambwe kweli ameshindwa kuelewa kwamba hata kama Slaa atakamatwa bado Slaa si wa Tarime na wale wataendelea kumchagua kiongozi wa Chadema ambaye ni Mtarime mwenzao anaye gombea Ubunge ?

Hivi haya madai kama hayawezi kutokea Slaa hana haki ya kwenda Mahakamani ama kwa kuwa Mahakama ni za CCM ? Hivi kweli JK na CCM wanaweza kudiriki kutumia habari hizi kuomba kura za wananchi wa Tarime ? Ni CCM kuzidiwa ama do I smell something stinky ?
 
Tatizo tz watu siasa wanachukulia kama usanii wakati its a serious profession.
Sasa hayo ndo mambo ya kuongea mbele za watu kweli.
Why after 3month?
Bongo kazi ipo
 
Tambwe kumbe ni mtupu namna hii ? Do we have a room for scare politics ?Tarime sawa na Moshi mjini .Tambwe kweli ameshindwa kuelewa kwamba hata kama Slaa atakamatwa bado Slaa si wa Tarime na wale wataendelea kumchagua kiongozi wa Chadema ambaye ni Mtarime mwenzao anaye gombea Ubunge ?

Hivi haya madai kama hayawezi kutokea Slaa hana haki ya kwenda Mahakamani ama kwa kuwa Mahakama ni za CCM ? Hivi kweli JK na CCM wanaweza kudiriki kutumia habari hizi kuomba kura za wananchi wa Tarime ? Ni CCM kuzidiwa ama do I smell something stinky ?

Kaka salama lakini kaka?
 
Wakamate kwanza mafisadi au hii si sawa?
 
michkp.jpg
 
GT Mkuu ana itikadi za chama?
Anyways..Hili kwa kweli si la kukenulia mapengo kwa kusema ukweli...Hujasikia wanasiasa walevi wa chadema na ccm wamechomana visu kwa mujibu wa kamanda Rwambow?
 
Natabiri mpasuko mkubwa CCM wakishindwa Tarime. Na ole wao CCM wanshindwe huko. tusubiri tuone. Hizi lugha sizo kabisa. Hawana tofauti na mtikila
 
wamefilisika.Maji yapo shingoni watasema chochote,wataua Mbwa,kuku,watanunua shahada,wata-end up kumwagiwa pilipili na kuangukia pua siku ya motokea.poor CCM!
 
Upinzani wametu let down. Kwa kutoungana kwa ajili ya kupigana na nunda sisiemu tumekwisha. Najua hii ni habari mbaya lakini habari ndiyo hiyo.
Unajua kwa nini sisiemu walituma mwana sisiemu kwenda kununua kura za Chadema tena ofisini kwao?
 
Tatizo tz watu siasa wanachukulia kama usanii wakati its a serious profession.
Sasa hayo ndo mambo ya kuongea mbele za watu kweli.
Why after 3month?
Bongo kazi ipo

Kusema baada ya 3 months ndiyo fishy....Kisaikolojia wananchi tayari watakuwa wanajuwa ama kuamini kuwa kina Slaa walimwua Wangwe...Kwa maana hiyo wananchi wanasubiri tu muda wa uchaguzi upite ili Slaa akamatwe...What a PITTY.
Hii ni HATARI sana na mimi nadhani kuna uwezekano wa machafuko zaidi kama siasa za namna hiyo zisipowekwa kando.
Kuanzia wakati Dk Slaa akitowa habari za ufisadi huko bungeni..Marmo naye alileta madai hayo hayo kuwa watamkamata...Yani wameona hawa watu wanaweza kuchukuwa nchi na sasa desparation imekuwa unbelievable na kwa kweli tutaona mengi sana.
Nawaombea Mungu wale wote ambao maisha yao yamo hatarini wakati huu mgumu kwenye historia ya Taifa letu na dunia kwa ujumla.
Watanzania we should rise to the occassion and confront the evil when ever possible.
This time we should do it ONCE AND FOR ALL.
 
Kwa CCM na serikali yake, kushinda uchaguzi mdogo Tarime ni kitu muhimu sana bila kujali kama ushindi huo utapatikana kwa gharama ya maisha ya watu au la. Ku "counter" matukio ya watu kunyunyiziwa pililpili, leo magari yanayorusha maji ya kuwasha yameingia Tarime. Kwa mambo yanavyoendelea, kuna kila dalili kuwa CCM wamepania kulazimisha ushindi. Muhimu hata hivyo, inatakiwa kutafakari kitakachofuata iwapo CCM watalazimisha ushindi. Mbunge takayepatikana bila ridhaa ya wapiga kura atakuwa katika nafasi ipi mbele ya wapiga kura wake ukizingatia na ujasiri wa wapiga kura hawa? CCM na serikali yake bado watakuwa nguvu ya kumwaga huko baada ya miaka miwili uchaguzi utakapofanyika nchi nzima?
 
Tambwe anasema watakamatwa baada ya miezi mitatu...Hii ni karata ya kisiasa kwasababu baada ya miezi mitatu uchaguzi utakuwa umekwisha....Kwanini wasikamatwe kabla ya uchaguzi ili tujuwe ukweli?
Mimi naona uchaguzi huo wa Tarime usimamishwe hadi hapo ukweli utakapowekwa wazi ili kuwa protect wananchi.
Wananchi wa Tarime waruhusiwe kuujuwa ukweli kabla hawajapiga kura kwa mtu asiyependa maendeleo yao
.

Tatizo la Tambwe ni kuwa anatumiwa na CCM kuropoka yale ambayo CCM wanayapanga gizani kwa lengo la kuua upinzani.Kauli ya Tambwe ni ya mwanasiasa uchwara ambapo huwezi kumzania Tambwe kwa kumtizama kwa umbo la nje.

Tanzania haihitaji siasa za vitisho na maneno machafu.Inajulukana wazi kuwa CCM wanawatumia wanasiasa uchwara nje na ndani ya chama chao pamoja na vyombo vya dola kutaka wanatarime na watanzania waamini kuwa Chacha Wangwe aliuwawa na viongozi wa chadema.

Kila mtanzania mwenye hekima hataacha kupuuza kauli rejareja kama hizi za Tambwe.
Ni afadhali kumdanganya mtu anayefahamu kuliko kumdanganya asiyefahamu kwa kuwa siku atakapofahamu kamwe hatadanganyika tena.Watanzania siyo mabwege tena asilani
 
Upinzani wametu let down. Kwa kutoungana kwa ajili ya kupigana na nunda sisiemu tumekwisha. Najua hii ni habari mbaya lakini habari ndiyo hiyo.
Unajua kwa nini sisiemu walituma mwana sisiemu kwenda kununua kura za Chadema tena ofisini kwao
?

Mchukia fisadi,

Wajua vita yoyote haikosi kasoro.Katika harakati za kuifikia demokrasia pevu kwa nchi kama yetu kuna milima na mabonde sana.Bahati mbaya wengi wa wanaoingia kwenye siasa ni wabinafsi.Wanaifanya kazi ya siasa kama mradi wa familia hivyo kula yao na vaa yao inatokana na siasa.

Katika hali kama hiyo tusitegemee kila anayejiita mwanasiasa kuwa mwadilifu.La msingi mimi na wewe tujitambue na kuchukua hatua.Uchafu wa mwenzio usiwe sababu ya wewe na mimi kuwa wachafu.Pili pale panapoonekana kuwa na mwelwkeo wa siasa safi na adilifu ndipo ps kuanzia.Kwa wingi wetu na umoja wetu tusitizame wengi wanaotuvunja nguvu bali wachache wanaotutia moyo.

Ni ngumu sana kuunganisha nguvu kisiasa kama mmoja anaweka maslahi ya taifa mbele wakati mwingine anawaza kujaza tumbo lake apate usingizi.Kuna wanasiasa wanadiriki kusema bora wapinzani tukose wote majimbo kuliko chama fulani kipate na sisi tukose.Huko ni kuishiwa kisiasa ndugu.
 
Kusema baada ya 3 months ndiyo fishy....Kisaikolojia wananchi tayari watakuwa wanajuwa ama kuamini kuwa kina Slaa walimwua Wangwe...Kwa maana hiyo wananchi wanasubiri tu muda wa uchaguzi upite ili Slaa akamatwe...What a PITTY.
Hii ni HATARI sana na mimi nadhani kuna uwezekano wa machafuko zaidi kama siasa za namna hiyo zisipowekwa kando.
Kuanzia wakati Dk Slaa akitowa habari za ufisadi huko bungeni..Marmo naye alileta madai hayo hayo kuwa watamkamata...Yani wameona hawa watu wanaweza kuchukuwa nchi na sasa desparation imekuwa unbelievable na kwa kweli tutaona mengi sana.
Nawaombea Mungu wale wote ambao maisha yao yamo hatarini wakati huu mgumu kwenye historia ya Taifa letu na dunia kwa ujumla.
Watanzania we should rise to the occassion and confront the evil when ever possible.
This time we should do it ONCE AND FOR ALL.

It really a pitty Jmushi lakini tufike mahali watanzania tuwazoee sisiemu kuwa pale wanapoona wanazama wako tayari hata kuua sembuse kuzusha maneno kama hayo.
 
Kama maneno haya yametoka mdomoni mwa Tambwe kwelikweli, basi jamaa huyu ni pumbavu kweli kweli kwani amekosa hata diplomacy ya kiuongozi.
 
Mnaweza mkaungana katika maana kwamba wote mnapigana kuelekea upande mmoja. Lakini kuungana pekee yake bila ku Define vizuri adui yenu ni nani kunaweza wanyima ushindi vile vile.
Adui wa nje siku zote ni rahisi sana kumtambua na kupanga mbinu za kupambana naye, tatizo ni pale azukapo adui katikati ya kundi lenu.

Mtamtambua vipi? na mkimtambua mtapiga vipi?

Adui ni pamoja yule mmoja wenu apiganaye kwa maslahi yake binafsi na yule apiganaye kwa mshahara na si kwa lengo la pamoja.

Kuna maadui wengi ndani ya vyama vya upinzani.
Maadui waliopandikizwa na CCM kupitia usalama wa Taifa.
Pia maadui waliozaliwa ndani kwa ndani walio tayari kuwa vibaraka, wasio na matako wala kikao, hawana jinsi, wako tayari kutumika kama nguo ya ndani ili maradi tu malengo yao binafsi yatimie.

Maneno ya kubuni toka kambi moja kamwe hayawezi kuivunja kambi nyingine, labda tu kambi husika iwe ni kambi via na kugeuka kuwa kambi tegemezi kimawazo, kimtizamo na kimwelekeo.

Mtu mwovu siku zote hujidhihirisha kwa maneno na matendo yake mwenyewe.
 
na maadui wa upinzani siyo ccm peke yao, ni pamoja na james mbatia wa nccr, mtikila wa dp, na hso akina chipaka wanaozungumzia uchaguzi wa tarime wakiwa peackcok hotel dsm
 
Back
Top Bottom