Mwana Ilala
JF-Expert Member
- Jan 29, 2013
- 1,287
- 486
Hallo Wana JF.
Napenda kutoa RAI ya tahadhari kwa wale wanaomiliki vilongalonga aina ya Smartphones kwa kile wanachohifadhi katika simu zao.
Umezuka mtindo hivi sasa,naweza kusema kwa baadhi ya watu wasiokuwa na maadili kutumia simu zao na kujirekodi wakati wakiwa Faragha/Jamiiana/tifuana na wapenzi wao.
Tabia hii naweza kuiita ni Highest degree ya UJINGA. Kwa sababu haileti maana kwa yule unayemuita ni Mpenzi/Mme/Mke umrekodi wakati mnashughulika na kuhifadhi picha kama hizo kwenye simu yako/zenu. Kwa sababu yule ni Mpenzi/mwandani wako, mda wowote unapomuhitaji unampata. Sasa iweje leo hii utembee na Video mlizojirekodi mkiwa mnajamiiana/tifuana!?
Ok, acha niongelee madhara ambayo unaweza kuyapata kama na wewe ni mmoja ya watu wanaojirekodi na wapenzi wao mkiwa faragha.
Moja, Madhara ambayo unaweza kuyapata ni hili la kuachana na huyu unayemuita Mpenzi/Hawara/Mke au Mume. Akiamua kukudhalilisha kwa kusambaza utupu wako kwa Marafiki zako na hata wale wasiokujua, Utaificha wapi sura yako!?
Pili, Kuna suala la Simu kupotea/kuibiwa. Ukiibiwa simu leo hii na ikatokea kuwa ulikuwa umehifadhi huko picha kama hizo!? Utakuwa Mgeni wa nani!?
Mfano, Nchini Philipine,Jamaa mmoja alipokuwa night CLUB aliokota Simu ya Mdada Msanii Maarufu wa Tasnia ya Drama, aliporudi nyumbani kesho yake akamsimulia rafiki yake kuwa ameokota smartphone na anataka amtafute mwenye nayo amrudishie.
Rafiki yake alikuwa ni mtundu sana wa simu akichukua na kuifungua kuangalia contents zilizomo Ndani. Wakagundua kuwa ilikuwa ni simu ya msanii maarufu wa sinema na Mbaya zaidi alikuwa amejirekodi video nyingi na picha kadhaa za UCHI akiwa faragha na mpenzi wake.Akamshauri kuwa hapo umaskini ndio bye bye.
Wakatoa tangazo la kuinadi kuwa kuna simu ya Msanii imeokotwa ila mwenye nayo atalazimika kuikomboa kwa 12M za kibongo. Waandishi wa habari wa udaku huko Philipine walipoliona hilo tangazo wakajua moja kwa moja hiyo itakuwa ilikuwa na kitu cha zaidi haiwezani simu iokotwe kisha inadiwe kwa hela nyingi hivyo.
Waliookota hiyo simu wakavutiwa uzi/simu kutoka kwa waandishi wa habari za udaku(Let's Say GLOBAL PUBLISHER ya huko kwao) kutaka kujua ni nn hasa mpaka hiyo simu ikombolewa kwa bei kubwa hivyo.
Waandishi wa habari wakapanda dau hadi $18,000. Msanii aliyepoteza simu akafikia $15,000.
Waliookota simu Wakawa na utu wakampatia mwenye nayo badala ya waandishi wa habari.
Tatu, hasara ya tatu, Rafiki yako anaweza akakuibia picha/Video zako bila ya ww kujua, halafu siku mkigombana unashangaa picha zako zina-whatsappiwa kila kona ya Mtaa unakoishi bila kujua chanzo ni nani.
Nne, Ukipeleka simu kwa fundi, hata kama umezifuta au umezihamisha hizo picha ndio ukaamua kumpelekea Fundi. Uwezekano wa kuzi-recover ni mkubwa sana. Au let's assume kuwa simu yako imezima ghafla kabla hujazihamisha. Si lazima umpelekee fundi!? What will happen kwa Fundi!?? Jibu unalo Mwenyewe
Nnatoa wito wa tahadhari kwa watumiaji wa smartphone kuwa na matumizi yaliyo sahihi katika simu zao. La sivyo zitawaondolea utu wenu.
Kumradhi kwa kichwa cha habari kukuvutia na kuisoma hii TAHADHARI. Najua umeelimika na. Simu yako utaitumia kwa umakini na Usahihi.
Thanks wana JF.
Napenda kutoa RAI ya tahadhari kwa wale wanaomiliki vilongalonga aina ya Smartphones kwa kile wanachohifadhi katika simu zao.
Umezuka mtindo hivi sasa,naweza kusema kwa baadhi ya watu wasiokuwa na maadili kutumia simu zao na kujirekodi wakati wakiwa Faragha/Jamiiana/tifuana na wapenzi wao.
Tabia hii naweza kuiita ni Highest degree ya UJINGA. Kwa sababu haileti maana kwa yule unayemuita ni Mpenzi/Mme/Mke umrekodi wakati mnashughulika na kuhifadhi picha kama hizo kwenye simu yako/zenu. Kwa sababu yule ni Mpenzi/mwandani wako, mda wowote unapomuhitaji unampata. Sasa iweje leo hii utembee na Video mlizojirekodi mkiwa mnajamiiana/tifuana!?
Ok, acha niongelee madhara ambayo unaweza kuyapata kama na wewe ni mmoja ya watu wanaojirekodi na wapenzi wao mkiwa faragha.
Moja, Madhara ambayo unaweza kuyapata ni hili la kuachana na huyu unayemuita Mpenzi/Hawara/Mke au Mume. Akiamua kukudhalilisha kwa kusambaza utupu wako kwa Marafiki zako na hata wale wasiokujua, Utaificha wapi sura yako!?
Pili, Kuna suala la Simu kupotea/kuibiwa. Ukiibiwa simu leo hii na ikatokea kuwa ulikuwa umehifadhi huko picha kama hizo!? Utakuwa Mgeni wa nani!?
Mfano, Nchini Philipine,Jamaa mmoja alipokuwa night CLUB aliokota Simu ya Mdada Msanii Maarufu wa Tasnia ya Drama, aliporudi nyumbani kesho yake akamsimulia rafiki yake kuwa ameokota smartphone na anataka amtafute mwenye nayo amrudishie.
Rafiki yake alikuwa ni mtundu sana wa simu akichukua na kuifungua kuangalia contents zilizomo Ndani. Wakagundua kuwa ilikuwa ni simu ya msanii maarufu wa sinema na Mbaya zaidi alikuwa amejirekodi video nyingi na picha kadhaa za UCHI akiwa faragha na mpenzi wake.Akamshauri kuwa hapo umaskini ndio bye bye.
Wakatoa tangazo la kuinadi kuwa kuna simu ya Msanii imeokotwa ila mwenye nayo atalazimika kuikomboa kwa 12M za kibongo. Waandishi wa habari wa udaku huko Philipine walipoliona hilo tangazo wakajua moja kwa moja hiyo itakuwa ilikuwa na kitu cha zaidi haiwezani simu iokotwe kisha inadiwe kwa hela nyingi hivyo.
Waliookota hiyo simu wakavutiwa uzi/simu kutoka kwa waandishi wa habari za udaku(Let's Say GLOBAL PUBLISHER ya huko kwao) kutaka kujua ni nn hasa mpaka hiyo simu ikombolewa kwa bei kubwa hivyo.
Waandishi wa habari wakapanda dau hadi $18,000. Msanii aliyepoteza simu akafikia $15,000.
Waliookota simu Wakawa na utu wakampatia mwenye nayo badala ya waandishi wa habari.
Tatu, hasara ya tatu, Rafiki yako anaweza akakuibia picha/Video zako bila ya ww kujua, halafu siku mkigombana unashangaa picha zako zina-whatsappiwa kila kona ya Mtaa unakoishi bila kujua chanzo ni nani.
Nne, Ukipeleka simu kwa fundi, hata kama umezifuta au umezihamisha hizo picha ndio ukaamua kumpelekea Fundi. Uwezekano wa kuzi-recover ni mkubwa sana. Au let's assume kuwa simu yako imezima ghafla kabla hujazihamisha. Si lazima umpelekee fundi!? What will happen kwa Fundi!?? Jibu unalo Mwenyewe
Nnatoa wito wa tahadhari kwa watumiaji wa smartphone kuwa na matumizi yaliyo sahihi katika simu zao. La sivyo zitawaondolea utu wenu.
Kumradhi kwa kichwa cha habari kukuvutia na kuisoma hii TAHADHARI. Najua umeelimika na. Simu yako utaitumia kwa umakini na Usahihi.
Thanks wana JF.