Elections 2010 SMS ya Maandamano nchi Nzima Ijumaa Imeanza


Uchunguzi binafsi hauwezekani, tayari watu wamefanya kwa niaba ya watanzania wote na ndiyo maana chadema wameamua kupeleka rasmi malalamiko kwenye NEC lakini taarifa nilizonazo zinasema kuwa NEC wamepuuza, kwa hiyo tufanyeje? Maandamano ya amani kabisa kuuambia ulimwengu wote kuwa wezi wamechukua nchi.
 
Pamoja. Maandalizi yafanyike vizuri na taarifa rasmi itolewe. Tutaandamana hata miezi 6.
 
Good point, Acid! Mageuzi inatakiwa wawe smart. Huu upuuzi wa kukurupuka na maandamano yasiyo na kichwa wala miguuu, ni wakitoto, na ninaulaani kwa nguvu zote! Naamini kuwa kuna some irregularites kwenye tally zinaozendelewa kutolewa na NEC. Lakini hizo irregularities ni ndogo sana kubadili matokeo ya urais. Kikwete ameshinda kihalali. Jaribu kuangalia trend ya kura toka mijini na viijini utaona kuwa sehemu za mijini, Dr. Slaa amefanya vizuri sana; na sehemu za vijijini Kikwete amefanya vizuri sana. Na kwa kuwa vijijini ndo' kuna wapiga kura wengi na Chadema wameperform poorly huko, then convetional wisdom ni kwamba, CCM wameshinda kihalali. So we can sit here/waste the next five years complaining kwamba CCM wameiba kura, then 2015 ikafika bila hata ya kufanya marekebisho yoyote yale, ama tunaweza tukaamua kujipanga upya [kuanzia sasa] na ku-channel hii anger kwa ajiri ya uchaguzi ujao wa 2015 kwa kujiandaa vizuri ili basi nasi tuweze kutufanya vizuri zaidi kwenye uchaguzi huo, ikiwezekana tushinde kirahisi. [Think of it folks!]

P.S. "Facts do not cease to exist because they are ignored." ~ Aldous Huxley
 
Naanza kuandaa mabango ya kubeba nipeni lengo kuu nifanye mambo nimechoka na mfumo huu wa wachache kufaidi wakati hii ni nchi yetu wote.
 
sitaki kuhoji sana issue ni hivi ni saa ngapi na tunaanzia wapi?
 
siungi mkono maandamano, Ila tujipange upya kuanzia sasa kuimarisha upinzani kwaajili ya 2015, ukizingatia vifaa tulivyopeleka bungeni ni vifaa vya kazi kwelikweli. CCM kwa ninavyowajua tukiandamana wakotayari kufanya lolote ili kuwaaminisha watanzania kuwa upinzani maana yake vurugu, machafuko na umwagaji damu.
 
Wana JF
kwanza, lazima tukubali kuwa kila mtu anamtazamo wake katika kuchambua au kuangalia suala fulani na ni haki yake,
Pili, kila mtu ana haki yake ya kidemokrasia kushabikia upande fulani na hakuna mtu mwenye haki ya kutaka kujua kwanini ni shabiki
Tatu, kina mtu yuko huru kuwa mwanachama wa chama chochote hivyo akajisikia anawajibu wa kusemaa chama chake 'positively'
Nne, Kuna baadhi ya watu hawako katika kundi lolote kazi yao ni kuwa critical katika masuala mbalimbali bila kujari ni la chama gani
Tano, JF ni jukwaa huru kwa mtu yeyote bila kujari yuko upande gani katika makundi niliyotaja hapo juu
Sita, Mara nyingi watu walio upande wa upinzani wakishinda huwa halali wakishindwa huwa haramu

Kwa mantiki hiyo si sahihi kwa wale ambao wanakuwa na mawazo tofauti hasa na wale washabiki na wanachama na wapenzi wa CHADEMA kuanza kusakamwa, kuonekana hawafai, kuwatukana n.k
Wale wanaJF ambao wamekuwa wanawasakama wanaJF wngine ambao wametofautina nao kimawazo, kiitikadi na mitazamo ni namna ya kuonyesha ufinyu wa mawazo, kutokomaa kimawazo na udikteta wa mawazo. Wanatakiwa kubadilika kimawazo wawe wanajibu hoja kwa hoja badala ya kutukana na kukashfu wana JF wengine.

Wana JF hao wakumbuke kelele za chura hazimzii ng'ombe kuywa maji, la msingi ni kufanya uchambuzi wa kina wa hoja na kuona wapi palekebishwe kwa manufaa ya baadae, hivyo kwa namna fulani wan JF tuwe kama pressure / lobbying group kwenye society ili kurekebisha mambo.
Kama mtindo utakuwa wa namna hii JF itakuwa kama jukwaa la MBAYUWAYU ambapo nafikiri hata founders wetu wa JF wasingependa tuwe mbayuwayu ila wangependa tufanye kitu cha kuleta mabadiliko katika jamii yetu bila kumwaga damu. Maisha yetu na familia na ndugu na watanzania wengine yana maana na thamani kubwa kuliko urais wa nguvu na vurugu.
 

Haki ipi? Kwani waliopigia CCM wao hawahitaji haki hasa baada ya kushinda uchaguzi, walioshindwa wanaona hakukuwa na haki, kweli watu vichwa havifikirii , pole sana. TIME HEALS na 2015 iko getini
 
Sio ya kichochezi ndugu yangu kama unavyodhani japo sijaipata.
Miaka mitano mikononi mwa ukoloni wa dhalimu kikwete na jamaa zake ni mingi zaidi ya unavyofikiri hasa watoto wa miaka wa form four na kushuka chini.Tutawasomesha kwa kutumia nini kama tutaiuza nchi kwa hiyo miaka mitano.

Death in freedom is better than life in bondage.
 
count me in, i will sacrifice for justice just like the other comrades! Aluta continua!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…