SMZ yakataa waraka wa wakatoliki

Moderator, nadhani tunahitaji kujadili mambo ya maana ya kujenga nchi na siyo huu ujinga wa akina hamza anayeropoka bila hata kujua anaongea nini. Fungeni hii thread haraka.
 

Halafu wewe ndio unaonyesha mdini namba moja.
mbona umeshupalia waraka wa Wakatoliki na wa shura ya maimamu(Waisilamu)huusemi?
 
Eeeh kijiwe cha wenye kujihita Great Thinkers, sasa haya ndio majibu na mijadala ya wale wenye kujitia wakuu wa hikma na ilmu kubwa. Nawasikitikia wale wasio ishi kwenye nyumba za Great Thinkers, sijui watakuwa katika hali gani.

Unajua ndugu baada JF kuonekana inatoa hoja za nguvu na ambazo ni mwiba kwa baadhi ya watu, sasa hivi kuna mamluki lukuki. Ukichunguza utaona kuna watu wanajaribu kutumia JF kama sehemu ya mhadhara wa dini, kuna wengine wanajaribu kuifanya JF ni Habari Corporation - wanatoa propaganda za kuwatetea fisadis.

Kwa hiyo unakuta JF inaanza kujawa na watu mamluki hawana hoja za msingi lakini wamo tu, mara udini, mara nini, basi ili mradi watibue mtiririko wa mawazo constructive ya great thinkers.

Lakini pamoja na hizo njama, JF will live longer, I tell them.
 
Last edited:

Hivyo uerevu uko wapi kwa kufikiria Zanzibar yenye asilimia karibu 98 Waislamu kupewa muongozo na Kanisa?
Wakati mwengine tunatakiwa tuwe tunatumia akili na sio jazba katika kuangalia haya mambo. Zanzibar ambayo kikatiba ina Taasisi za Kiislamu ndani ya Serikali yake unategemea wataukubali muongozo wa Kanisa? Naona hata hii mada isingekuwepo kwani ni natural kuwa huo waraka hauwezi kukubalika Zanzibar na iliyobaki ni kutowa moshi na shutuma za Bure.
NIOMBE KUULIZA! Wangapi mnaoshabikia waraka wa Waislamu ambao sio Waislamu? Jawabu ni kuwa kila mmoja na lake na ndio maana wale wenye umakini walilipigia kelele hili kwani Waswahili wana msemo " Mtu haachi kutia tonge mdomoni akatia puani". Kila kitu kina mwenyewe na kitu cha jumla kisitolewe na kikundi fulani na ikifanyika hivyo itaonekana kuwa ni chao.
 

Naona unaleta mjadala ndani ya mjadala lakini hili la Zanzibar kunufaika na Muungano unalo uhakika nalo?
Nisingependa jazba lakimi kama ukijana ningeomba uwaulize wakubwa zako vipi Zanzibar ilivyokuwa kabla ya Muungano, wakati wa Karume, chini ya ASP na baada ya kuundwa CCM na kuitawala Zanzibar kwa mpango wa Chama kushika hatamu.
Kijana unahitaji darasa kujuwa kwanini mnangangania Muungano usio na faida kwenu.
 


Hakuna anaekosa usingizi kwa kukosa kupendwa na wewe! Historia inafaa kuwa jawabu lako kwa hili.
Ama kwa kuvunja Muungano, Wazanzibari wengi watakuoneni ni sawa na wale walioondoshwa 1964.
 


Mawazo yako yanakubaliwa na wengi lakini WAKUBWA zenu wanajuwa sababu ya sacrifice hiyo.
 
Wewe ulieanzisha thread cut the crap na kutuletea chanzo cha hii habari usitufanye sisi ni wajinga umeskia?

Chanzo cha Habari kiiwepo au la si neno. Si unaona mjadala unaendelea? INawezekana ikawa huo ni mtizamo wake na kama hauna faida ni sisi wa kuueleza.
 
SMZ ikikataa Waraka ndio kusema itazuia watu kuusoma? Nadhani hizo ni ndoto za alinacha. Katika ulimwengu wa sasa uwezi kuzuiya waraka kusomwa. I am really sorry for such myopic SMZ leaders.

Acha kuwa double standard! Kwa anaeukubali unamkubali kuwa ni mtu na anaeukataa unamuona wa ajabu.
Ulimwengu huu watu huacha kunywa soda yenye sukari kwa gongo lisilo na ladha. Kama wewe umeuona huo waraka ni muongozo kwanini uone wenzio hawana haki ya kuona vyengine? Tuko huru kimawanzo na mwenye mawanzo mgando basi ana tatizo.
 

Sidhani kama chanzo cha huo Waraka hakikusaidia kwa Wazanzibari kutosomwa kwa huo Waraka kule Zanzibar, na hiyo ndio ukweli ambao wengi hamuutaki. SMZ hata haikuwa na haja ya kucoment kwani hauna thamani huko.
 

Nimefuatilia postings zako na kuona kuwa wewe si mmoja wa hao wanaotowa hoja za maana kwani kwa mfano wa hii hoja hivyo wewe huoni kuwa ni jambo la kawaida kwa Zanzibar kukataa kupewa muongozo na Kanisa? Bila kujali huo unaouita udini nini ulitegemea kama mkiristo kama mkiristo na sio mwanajamii (Kama walitaka iwe kama Taasisi ya jamii wasingetumia kanisa) anatowa muongozo kwa mtu wa dini nyengine kwa jambo linalowahusu wote, hilo ni sawa? Na jee yule wa dini nyengine utamlaumu kwa kukataa? unajuwaje kuwa dini yake haimruhusu kupokea muongozo kutoka dini nyengine?
Ni wazi kuwa Wazanzibari hautowahusu huo Waraka na kuukataa isiwe nongwa kwani mlikosea njia ya kuuwasilisha. SI mlitaka Kanisa lionekane linahusika? Sasa nani mdini hapo hebu jiulize.
 
KULA TANO BWANA MKUBWA.....yaani wabongo tumewachoka hawa wazanzibar mpaka inatia kinyaa,siku hizi wala hawaendi huko watu ni china au indonesia.aaaaaaaaah hhhuu mungano ufe wabaki na kakisiwa kao,hovyooo.

Hii ni jazba na kwa mtazamo huu hatutatui tatizo.Suala la muhimu ni kusikiliza malalamiko yao na kuyafanyia kazi huku taratibu tukiendelea na shughuli za kuimarisha shirikisho la Afrika ya Mashariki.

Katika shirikisho kutakuwa na serikali moja bunge moja na sarafu moja,tukifika huko hizi kelele za Zanziba zitakwisha kwa kuwa hawatastahimili kujitenga na shirikisho litakalo kuwa na nguvu kubwa ya soko.
 
KULA TANO BWANA MKUBWA.....yaani wabongo tumewachoka hawa wazanzibar mpaka inatia kinyaa,siku hizi wala hawaendi huko watu ni china au indonesia.aaaaaaaaah hhhuu mungano ufe wabaki na kakisiwa kao,hovyooo.

Haya mambo hayatufikishi popote,ni bora kuhimiza shirikisho la Afrika Mashariki ili kumeza hizi kelele zote za Zanzibar.
 


Hakuna mtu aliyeupeleka waraka wa Wakatoliki kwa Serikali ya Waislamu, sorry, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Hizi taarifa kwamba wameukataa zinatoka wapi? Waraka ule (Pastoral Letter) hutolewa kwa ajili ya waumini wa kanisa Katoliki na hutolewa kila mwaka. Sasa waraka usiokuhusu utasemaje umeukataa. Kwanza wengine hata hawauelewi (kama kweli wameusoma) kutokana na kuwa na upeo mdogo. Acheni kudandia mambo yasiyowahusu!
 
Last edited:
MIMI nadhani wewe ndio ulijaa ujinga na upofu usiyekuwa na uwezo wa kutambua au kuona lipi baya au zuri kwa maslahi ya nchi toka lini kiongozi wa dini akawa mtaalamu wa mambo ya siasa.kwa waraka huo wanapinga hata maandiko ya dini ambapo Yesu alisema ya kaisari muachie kaisari.Hivi wamenogewa nini kutaka kujiingiza kwenye mambo ya siasa.ikumbukwe kuwa roman catholic ilitumika sana na CIA kuangusha ukomunisti.
 
Last edited:


Hapa naona tatizo ni lile lile la upeo wa kuelewa mambo!
 
Mimi naona tuwe watu tunaofikiria. Wakati wenzetu wa nchi nyingine wana "inter-religious dialogues" yaani wanakutanisha dini tofauti kujadili maslahi ya nchi zao, sisi tunaishia kutukanana na kutishia amani. Mimi naona waraka wa Wakatoliki ni mzuri. Ikiwa waislamu wamekuja na wao basi ndio muda muafaka wa kuanza "inter-religious dialogue" ili kuweza kujua maslahi ya waumini katika jamii mchanganyiko ni yapi. Waacheni wakatoliki waje na waraka wao. Halafu waraka huo si wa serikali. Sasa wanaukataa kwa misingi gani? Je kanisa katoliki lifanya maombi ya serikali kuukubali waraka huo? Hapana, sasa serikali, inaukataajae? Je serikali ni mkatoliki? Je, wakatoliki hawana "freedom of expression"? Mimi ninachomshauri Rais Kikwete ni kuachana na masuala ya kidini. Masuala hayo awaachie viongozi wa dini. Ila nilipousoma waraka wa wakatoliki sikuona hata sehemu moja iliyotaka kuvunja amani. Kama ipo ndugu zangu watanzania nifahamisheni. Halafu kama ni mahakama ya kadhi, mbona hata wakatoliki wana "canon law" na mahakama zao, je serikali itawaacha nyuma? Je, "traditionalists" na "wapagani" wakitaka mahakama zao, mtawakatalia? Hata, askofu Kakobe akitaka mahakama yake mtamkataria?

Nadhani masuala ya mahakama yangebaki kwenye madhehebu kama ilivyo sasa, kwani kila mtu akiomba mahakama yake je tutaishije? Nadhani tutumie busara zaidi katika suala hili. Nadhani serikali inalitambua hilo na inalifanyia kazi.

Kwa heshima zote kwa waumini wa dini zote nadhani cha muhimu ni kusali na kuishi maisha ya uadilifu na kupinga kabisa mafisadi. Je, kuna dini inayokubali mafisadi? Nadhani haipo. Hivyo, tusiwape kura zetu mafisadi kwani hawatatusaidia. Wana nia ya kujaza mifuko yao tu, itune mpaka ipasuke. Kwa hiyo ndugu zangu wazanzibar amkeni. Je hilo amlioni?
 
Ahsante sana Ngekewa kwa kutumia muda wako mwingi kuweka mambo sawia.

Hakika Znz na SMZ ipo wazi dhidi ya huu waraka hatari sana wa wakatoliki.

Tunaelewa kuwa WAKATOLIKI walijipanga kwa kutumia nyenzo zote ikiwa pamija na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbalina wengine wengi kuhakikisha kuwa waraka unakubaliwa na watu wote. Na atakaye upinga basi ataandamwa kwa kashfa na matusi kama walivyofanya kwa Mz Kingunge na Askofu Kakobe na hata Dr barubaru .


Dr Barubaru, nakuaminia sana, upo wazi na mkweli katika kubainisha ukweli mpaka watu wanakubali.

Mola awabariki sana
 
Haya mambo hayatufikishi popote,ni bora kuhimiza shirikisho la Afrika Mashariki ili kumeza hizi kelele zote za Zanzibar.

kashindwa Nyerere ataweza nani kuiua Znz na waZnz. Sisi sio wajinga kama Wadanganyika kufuta identity yenu ya Udanganyika.

 
Tatizo nyie watu wa bara mnamambo! kama ngoma mpigiwe mcheze wenyewe Aseye wa unguja mlisikia lini tumeandika warka! tunashangaaa? sasa kama zogo lenu wenyewe sie wa visiwani latuhusunini? MI NASEMA TENA NASEMA NAMUUMNGA MKONO ALIYESEMA MWISHO CHUMBE! TUMEWAVUMILIA WA BARA SASA MNATAKA KUTUTIA VIDOLE VYA MACHO kHEE! INAKHERA!KWANI UMESIKIA UNGUJA HAKUNA MAKANISA?YAPO TELE NA MISKITI IPO TELE LAKINI SIYE TUPO KIMYA NA SWAUMU ZETU HILO ZOGO LENU HUKU VISIWANI TUNASEMA NO!

Tena tunaongeza mwisho ferry na sio chumbe! mkome wa Bara gomvi lenu wenyewe mnataka kutubebesha lawama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…