Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,916
- 43,505
Wasalaam Wanajamvi.
Bila shaka wapenda burudani mnajua fika BASATA nini na wanafanya kazi gani.Bahati mbaya au nzuri hawa BASATA wamekuwa wakionekana wakipaza sauti zao kwenye matukio makubwa, pengine tuseme yanaweza kuwa na manufaa zaidi kwao.
BASATA wamekuwa wakiandaa Tunzo za wasnii hapa nchini kupitia beer ya Kilimanjaro na kuziita Tunzo hizo Kilimanjaro Music Awards.
Toka Tunzo hizi zimeanzishwa Sauti ya'kulinda maadili na kupelekea nyimbo za wasanii kuenguliwa sikuwai kuisikia lakini nimeisikia Mwaka huu 2014 tena kipindi cha hiki cha Mchakato wa Tunzo hizi.
Ni ukweli usiopingika kabisa music wetu hasa bongo fleva umekosa wasimamizi na watu wa kuchuja nyimbo zenye mantiki na kulinda maadili yetu na ndio maana hata wengine wanamua kutukana kabisa kwenye nyimbo zao.
Tukiangalia nyimbo zilizo tolewa nje ya mchakato wa kuwania Tunzo za kili pengine zina stahili kabisa kwa vigezo vyao vya maadili.
Mfano Nimevurugwa -Snura
Tema mate-Madee.
Uzuri wako- Jux
BASATA NA ULINZI WA MAADILI YA WATANZANI KWA MSIMU
BASATA wanaonekana kulinda maadili ya watanzania kwa msimu na si nyakati zote na ndio maana nyimbo wanazo zi zuia kupewa tunzo bado zinaendeleo kuoneshwa kwenye vituo vya luninga.
Na wana sahau kuwa watu wanaendelea kuziangalia lakini wana subiri msimu wa Tunzo ndio waseme Maadili kwakweli huku ni kukosa msimamo.
Basata wana sahau kuwa maadili yetu yana paswa kulindwa wakti wote si wa tunzo tuu?
Mfano.
Hivi kwa nini Video ya Sugua gaga- shaa inaendelea kuoneshwa kwenye runinga? Pamoja na yaliyomo?
Hivi kwa nini Wimbo wa Roma pamoja na kupambwa na matusi bado unaendelea kupigwa kwenye radio?
BASATA ina maana macho yenu na masikio yana fanya kazi lipingi cha Tunzo tuu?
Kwanini msianzishe utaratibu wa wasanii kupeleka nyimbo na video zao kwenu kabla ya kuzipeleka kwenye vituo vya Radio na Runinga?
Kwa mazingira haya ni wazi mmewaonea kuwaengua Kwa kigezo cha kulinda madili wakti video zao zinaonekana kwenye vituo vya Runinga.
Kibaya zaidi zile ambazo hazikuingia kwenye mchuano wa kuwania Tunzo mmeziacha pengine amzioni kabisa.
Pengine kuna swali tuanaweza kujiuliza hivi kuziengua nyimbo na video fulani kuwania Tunzo ni suluhisho?Kwanini zisifungiwe moja kwa moja kuonekana na wahusika wapigwe faini?
Hivi BASATA mmefungia Filamu za Kitanzania zilizo kinyume na maadili? Au hakuna?
Ni vyema BASATA mkafanya kazi yenu kwa wakati hili muonekane mnatenda haki.
Karibu wana jamvi.
Bila shaka wapenda burudani mnajua fika BASATA nini na wanafanya kazi gani.Bahati mbaya au nzuri hawa BASATA wamekuwa wakionekana wakipaza sauti zao kwenye matukio makubwa, pengine tuseme yanaweza kuwa na manufaa zaidi kwao.
BASATA wamekuwa wakiandaa Tunzo za wasnii hapa nchini kupitia beer ya Kilimanjaro na kuziita Tunzo hizo Kilimanjaro Music Awards.
Toka Tunzo hizi zimeanzishwa Sauti ya'kulinda maadili na kupelekea nyimbo za wasanii kuenguliwa sikuwai kuisikia lakini nimeisikia Mwaka huu 2014 tena kipindi cha hiki cha Mchakato wa Tunzo hizi.
Ni ukweli usiopingika kabisa music wetu hasa bongo fleva umekosa wasimamizi na watu wa kuchuja nyimbo zenye mantiki na kulinda maadili yetu na ndio maana hata wengine wanamua kutukana kabisa kwenye nyimbo zao.
Tukiangalia nyimbo zilizo tolewa nje ya mchakato wa kuwania Tunzo za kili pengine zina stahili kabisa kwa vigezo vyao vya maadili.
Mfano Nimevurugwa -Snura
Tema mate-Madee.
Uzuri wako- Jux
BASATA NA ULINZI WA MAADILI YA WATANZANI KWA MSIMU
BASATA wanaonekana kulinda maadili ya watanzania kwa msimu na si nyakati zote na ndio maana nyimbo wanazo zi zuia kupewa tunzo bado zinaendeleo kuoneshwa kwenye vituo vya luninga.
Na wana sahau kuwa watu wanaendelea kuziangalia lakini wana subiri msimu wa Tunzo ndio waseme Maadili kwakweli huku ni kukosa msimamo.
Basata wana sahau kuwa maadili yetu yana paswa kulindwa wakti wote si wa tunzo tuu?
Mfano.
Hivi kwa nini Video ya Sugua gaga- shaa inaendelea kuoneshwa kwenye runinga? Pamoja na yaliyomo?
Hivi kwa nini Wimbo wa Roma pamoja na kupambwa na matusi bado unaendelea kupigwa kwenye radio?
BASATA ina maana macho yenu na masikio yana fanya kazi lipingi cha Tunzo tuu?
Kwanini msianzishe utaratibu wa wasanii kupeleka nyimbo na video zao kwenu kabla ya kuzipeleka kwenye vituo vya Radio na Runinga?
Kwa mazingira haya ni wazi mmewaonea kuwaengua Kwa kigezo cha kulinda madili wakti video zao zinaonekana kwenye vituo vya Runinga.
Kibaya zaidi zile ambazo hazikuingia kwenye mchuano wa kuwania Tunzo mmeziacha pengine amzioni kabisa.
Pengine kuna swali tuanaweza kujiuliza hivi kuziengua nyimbo na video fulani kuwania Tunzo ni suluhisho?Kwanini zisifungiwe moja kwa moja kuonekana na wahusika wapigwe faini?
Hivi BASATA mmefungia Filamu za Kitanzania zilizo kinyume na maadili? Au hakuna?
Ni vyema BASATA mkafanya kazi yenu kwa wakati hili muonekane mnatenda haki.
Karibu wana jamvi.