Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363

Wakati soda za kupunguza uzito au diet soda zinapendwa na kutumiwa sana hasa na watu wanaohofia suala la uzito wa miili yao na kiasi cha kalori wanazokula, uchunguzi mpya umeonyesha kuwa oada hizo zinasababisha matatizo ya figo.
Wataalamu wa Marekani wametangaza kwamba, kunywa soda mbili au zaidi za diet kwa siku, kunazidisha mara mbili uwezekano wa kupata matatizo ya figo.
Katika uchunguzi huu, asilimia 30 ya wanawake wanaokunywa soda hizo mbili au zaidi kwa siku, wameonekana kuwa wamepatwa na matatizo ya figo yanayojulikana kama GFR au Glomerular Filtration Rate ambapo ugonjwa huo huzifanya figo zipoteze uwezo wake wa kuchuja vyakula.
Wataalamu hao pia wameongeza kuwa, kula chumvi nyingi nako kunapelekea figo zishindwe kufanya vyema kazi zake.