Sofia Simba amtosa Hasna Mwilima


Sophia nae Fisadi tu hakuna lolote,mie simfagilii kwa kumwagia mwenzie kitumbua wakati yeye pia kilaza na anakula tu mi kodi yetu...Mungu tuma mwana atuokoe na haya majanga ya kila siku na Ubabe...kama kweli yeye yuko swafii kwa nini kuna ugomvi na mama Kahama?f ss
 
pole hasna mwilima. lakini nasikia na wewe ni kafisadi fulani umekula hela nyingi za wakima mama hapo uwt. na vile vile elimu yako ni darasa la saba tu.
Una uhakika na ulichoandika, maana mie nilimaliza nae Kidato cha NNE pale shule ya Sekondari Kinondoni mwaka 1988 sasa sijui nani kakueleza kaishia darasa la SABA
 
uwezo wake ni hafifu sana sana infact hawezi kudelivre.

kazi akipewa hafanyi, malengo hatimizi.sasa nyie mlitaka wambebe. kule Hai vilevile alishindwa kuonyesha uwezo wa kazi

kwa hilo Sophia Simba ametoa maamuzi sahihi.
 
Jamani huyu akili kichwani ni pro mafisadi..ameng'ang'ania sophia simba sophia simba kila mahali....una nini wewe....haloooo....wake up.......mdanganyika
 
Mimi ninachofahamu SS ni mlokole. Huwa anasali kanisa la Mama Lwakatare. Halafu sielewi kama kweli yuko hivyo kama magazeti yanavyodai. Bila ya shaka magazeti yamembomoa tu
 
- Kwani hii habari imethibitishwa kwamba ni ya kweli? Halafu si majuzi tu huyu katibu mkuu wake si ndiye aliyekuwa akimsifia kwamba mwenyekiti wake ni saafi na hakuna matatizo sasa haya yametokea wapi tena?

Respect.


FMEs!
 

Naona umeruka posts zingine soma zote
 


Any decision,sound loudly if is made without oppressing the culprit. The action which Sofia has taken to chase away her assistant can be acceptable or unacceptable depending the grounds surrounding the whole phenomenon.
 
leteni data kamili za huyu hasna mwilima hapa jamvini.hasa nyie mnaomtetea kama SS amemwonea.unajua pamoja na kuwa SS ana mapungifu yake, lakini huyu jamani ameshindwa kazi!!!!!!! na hiyo ndiyo taarifa aliyopelekewa JK with evidence na ndiyo akaamuru kazi isitishwe ebo!
 

Hatuko hapa kutetea utendaji kazi mbovu wa Husna, ila tunaangalia kwa pande mbili, kwamba mtu anayemwajibisha Husna naye si msafi kihivyo, kwa hiyo angetakiwa kutoa kwanza boriti ktk jicho lake kabla hajaona kibanzi ktk jicho la Husna. Hatuwezi kuwa na mwenyekiti wa UWT ambaye anatukana matusi mabaya hadharani (tena bungeni) halafu tukampa heshima anayoitaka. No way!
Ni hayo tu.
 
Nimejulishwa kuwa tofauti na UVCCM na Wazazi jumuiya ya UWT katiba yake imesajiliwa na Msajili wa Vyama tangu enzi ya TANU. There is not much Mwenyekiti wa Taifa can do. Kwa hiyo hatima ya ajira ya Katibu Mkuu wa UWT iko mikononi mwa Kamati ya Utekelezaji chini ya Mwenyekiti. This also explains kwa nini Halima Mamuya aliotoswa kirahisi na Anna Abdallah wakati Halima aliamua kuvuta michuzi ya pale Gogo Hoteli peke yake na kumwacha gizani mwenyekiti wake. Nasikia mdada yule alivuta 300 m.

Of course kama Hasna alikuwa proposed na JK na Sophia akakubali ulitegemea kwa heshima anayopaswa kumuonyesha JK angeendelea kumvumilia Hasna. Lakini ianelekea masikini Hasna kachinjiwa baharini na mapapa yamekunywa damu na nyama yake. Itabidi UWT apelekwe Katibu Mkuu mwanaume kama ilivyowahi kufanyika miaka ya nyuma enzi ya Mwalimu alipopelekwa Balozi Waziri Juma kuwa Katibu Mkuu. These women have failed to manage themselves. I fail to understand unakuwaje Mwenyekiti uongozi ukushinde uamue kufukuza Katibu Mkuu. Hawa wamepata laana ya kufukuzana. Akija mwingine atafukuzwa tu.
 
ni sophia ndiye aliyempendekeza Hasna Mwilima kwa JK maana ansema alimwamini hapo kwanza,lakini alipoingia kwenye position yake akaanza kumchimba na kumgeuka.

vile vile alipomteua hakujua kuwa uwezo wake ulikuwa mdogo kwa kiwango alichoonyesha ndio maana akapendekeza angolewe.

hasna mama nenda kaendeleze biashara yako ya duka la nguo na saloon mbona ilikuwa inakulipa sana. hayo maji marefu huyawezi!
 
Habari kwa ufupi ya TBC 1 ya saa kumi jioni hii... zimedai ...kuwa taarifa za Hasna Mwilima Kusimamishwa/kutimuliwa zimethibitishwa... Wakati huo huo Mama SS yupo jijini Mwanza katika mkutano wa taasisi ya KUKURU... Snap hio hapo
 

Attachments

  • Mama SS+JK+Hosea.jpg
    94.5 KB · Views: 48
Habari kwa ufupi ya TBC 1 ya saa kumi jioni hii... zimedai ...kuwa taarifa za Hasna Mwilima Kusimamishwa/kutimuliwa zimethibitishwa... Wakati huo huo Mama SS yupo jijini Mwanza katika mkutano wa taasisi ya KUKURU... Snap hio hapo
Sawa sawa , hiyo ni Kukuru tu...Lol!
 
Kikulacho kinguoni mwako, ndiyo shida ya kupewa vyeo on a siliver plate. Kama anataka uongozi seriously na akagombee, aachane na vyeo vya kudondoshewa, mbona wengine tumegombea na tumeshinda katika chama hichohicho na akina Simba wanatugwaya, maana hata yeye ni fadhila tu zinamlinda
 
hivi hiki chama ni chama cha wanawake wa CCM ambao ni waislamu.. uongozi mzima ni wa dini moja...
Huoni kingine ika dini tu?? Lediana na mama Kahama nao waislamu? Wingi wa waislamu kwenye UWT inatokana na kuwa wengi wa wanachama wake hai ni wa mijini na Pwani, sasa unategemea nini?
 
Timbwili timbwili la Sophia Simba jamani mie simwezi huyu mamam sijui ni wa kutoka uswahilini au?? mbona ni visilani ivi kungoza nchi nako kuna majungu au hawawezi uongozi?
 
Yaani jana yule Mama Makame alivyomrarua Hasna mpaka kamfanya aoenekane Kinyago Haki ya nani. Sasa kweli JK atampa cheo kingine mtu ambaye kachafuliwa hivyo. Maana hata akitaka kugombea viti maalum atakutana na hao hao akina Makame aliogombana nao. Napata picha kuwa Hasna kisiasa kwishney. Na Jk akisema ampe uRC au uDC maneno yatakuwa mengi. Pole dada Hasna. MYSRIP
 
WAZAZI(ccm)=UWT=CCM= Vyama vya majambazi na majizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…