Soft drinks na juisi ziwekewe onyo kuwa unywaji kupita kiasi ni hatari kwa afya zetu

Soft drinks na juisi ziwekewe onyo kuwa unywaji kupita kiasi ni hatari kwa afya zetu

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Hizi habari za soft drinks na juisi tumeiga tu kwa wazungu lakini watu weusi hazitufai kabisa.

Kwanza metabolic rate ya mzungu ipo juu kuliko ya mtu mweusi. Pengine sababu ni wao kuishi maeneo ya baridi. Hivyo mzungu anachakata chakula haraka kuliko mtu mweusi.

Pili magonjwa yatokanayo na ulaji m-baya na maisha ya bila mazoezi huwaathiri sana watu weusi kuliko wazungu. Hatari ya muafrika kupata kisukari aina ya pili ni mara mbili ya mzungu. Pia magonjwa kama High blood pressure yanawapata sana watu weusi kuliko wazungu. Na hata madhara yake huwa makubwa zaidi kwa weusi kuliko wazungu.

Sasa, pamoja na hatari hii, bado tunakula vitu sawa. Coca cola zile zile, pepsi zilezile, juisi na vyakula vingine, kitimoto na nyama ya kopo, na siagi na mikate vilevile. Hii ni kujihatarisha. Fikiria hapo. Hatari ya kupata kisukari aina ya pili kwa mtu mweusi ni mara mbili ya mzungu.

Kihistoria, inaonyesha binadamu tunapenda sana vyakula vya sukari na mafuta sababu vilikuwa adimu sana miaka hiyo tunakimbiza wanyama porini. Hatukuumbwa kula sukari na mafuta mengi kama tunayokula leo.

Napendekeza kuwe na onyo kwenye juisi na softdrinks zote. Zikisema unywaji kupita kiasi ni hatari kwa afya. Hata vyakula vya mafuta mengi viwekewe maonyo hayo. Tusiige ulaji wa wazungu, tupo tofauti kulingana na mazingira yetu. Tunachofanya kwenye chakula, ni sawa na mzungu amuige mtu mweusi kujianika juani.
 
Kama umefanya utafiti/ Research mbona imekosa vitu vingi vya msingi

Kwanza Eneo ulipofanyia, Sample yako, mbinu ya ukusanyaji data? Takwimu etc
 
Kama umefanya utafiti/ Research mbona imekosa vitu vingi vya msingi

Kwanza Eneo ulipofanyia, Sample yako, mbinu ya ukusanyaji data? Takwimu etc
Sijafanya research. Hizi ni facts ambazo ziko wazi.
 
Ni kuwahamasisha watu kufanya mazoezi mara kwa mara hiyo mambo sijui ya wazungu na watu weusi haipo wazungu nao wasipofanya mazoezi wanapata haya magonjwa ndio maana wao mazoezi ni sehemu ya maisha yao...
 
Ni kuwahamasisha watu kufanya mazoezi mara kwa mara hiyo mambo sijui ya wazungu na watu weusi haipo wazungu nao wasipofanya mazoezi wanapata haya magonjwa ndio maana wao mazoezi ni sehemu ya maisha yao...
Ila kisayansi ipo hivyo. Mtu mweusi ana hatari zaidi ya kupata kisukari aina ya pili, na high blood pressure. Pia metabolic tlrate yake ipo chini. Wewe na mzungu mkiishi lifestyle sawa, mkila sawa. Wewe utakuwa na hatari kubwa ya kisukari na Pressure kuliko mzungu.
 
Ila kisayansi ipo hivyo. Mtu mweusi ana hatari zaidi ya kupata kisukari aina ya pili, na high blood pressure. Pia metabolic tlrate yake ipo chini. Wewe na mzungu mkiishi lifestyle sawa, mkila sawa. Wewe utakuwa na hatari kubwa ya kisukari na Pressure kuliko mzungu.
Mimi naishi nao nakula vyakula vyao na wao ndio wanapata hiyo aina ya pili ya kisukari vipimo vya kisukari kila nyumba vipo wenzetu wameathirika sana na kisukari kuliko Nchi za Afrika hata wao wanajua hivyo hiyo tafiti yako fanya upya mkuu..
 
Mimi naishi nao nakula vyakula vyao na wao ndio wanapata hiyo aina ya pili ya kisukari vipimo vya kisukari kila nyumba vipo wenzetu wameathirika sana na kisukari kuliko Nchi za Afrika hata wao wanajua hivyo hiyo tafiti yako fanya upya mkuu..
Mkuu. Tafiti zimefanyika na zinafundishwa shuleni. Hili si suala la kufanyia tafiti tena. Limejulikana siku nyingi.
 
Ila kisayansi ipo hivyo. Mtu mweusi ana hatari zaidi ya kupata kisukari aina ya pili, na high blood pressure. Pia metabolic tlrate yake ipo chini. Wewe na mzungu mkiishi lifestyle sawa, mkila sawa. Wewe utakuwa na hatari kubwa ya kisukari na Pressure kuliko mzungu.
Mmmh! Mbona siyo sawa kabisa, tofauti iliyo ni elimu juu ya lishe, umasikini wa kipato kuweza kupata kilichobora, ujinga wa kutokujua mwili unafanyaje kazi na unahitaji nini katika lishe ya Kila yaani Yale makundi ya chakula, kwasababu ya huo ujinga wetu wa kutokujua imepelekea kulishwa au kula vitu visivyo na afya kwa miili yetu yaani kula makapi na vile virutubisho kuuzwa nje au kwa gharama kubwa au kufichwa kabisa na vingine havitengenezwi kabisa nchini, mfano sukari guru ndo lishe Bora kwaajili ya kuupa mwili sukari itayoleta nguvu na sukari ya kawaida inapaswa kunywewa kwa kiasi kidogo kama Kuna ulivyosema hizo soft drinks zinyewe kwa uchache maana sukari yake inakwenda moja kwa moja kwenye damu na kuweka sukari iwe juu kadiri unavyokunywa nyingi hivyo kunywa kiasi siyo vibaya ila kunywa nyingi na hiyo sukari guru iliyo Bora ndo haipatikani kabisa Wala nguvu ya kuitanganza itengenezwe haipo tofauti na wenzetu wanakamua miwa nyumbani na kutengeneza ngazi ya familia na vifaa wanavyo, tuje kwenye mafuta tunaambiwa mafuta siyo mazuri wakati bado mafuta yanahitajika mwilini na kula chukuchuku siyo kwamba ndiyo afya Bali Yale mafuta yanaharibu mishipa ya damu ndo mabaya yatumike kidogo na mafuta kama butter, jibini na gee ndo vizuri kwa afya na wenzetu wanatumia muda wote kama protini ya mwili huku sisi tukishindilia blue band kama mbadala wa butter, njoo kwenye wanga kwa vile wanga hautakiwi sana kwenye mwili unapaswa kuliwa kwa kufanya kazi ngumu basi wameweka uliwe mchana au Asubuhi na mtu afanye kazi utumike alafu usiku kiliwe chakula laini au position ndogo sana ya huo wanga na kubaki bila kushiba Ili usiku mwili usipate shida kuchakata vitu vizito, hivyo metabolic ipo sawa tatizo ni elimu ya afya ya miili yetu na elimu ya kutokula makapi yanayotesa mwili na mwisho kabisa mazingira mabaya ya jikoni yanayoleta uvivu wa kupika chakula kizuri tena kwa haraka maana wenzetu jiko limezungukwa na vifaa vyote vya muhimu Kila mtu kwenye familia anaweza kujipikia chakula chenye afya akala.
 
Hizi habari za soft drinks na juisi tumeiga tu kwa wazungu lakini watu weusi hazitufai kabisa.

Kwanza metabolic rate ya mzungu ipo juu kuliko ya mtu mweusi. Pengine sababu ni wao kuishi maeneo ya baridi. Hivyo mzungu anachakata chakula haraka kuliko mtu mweusi.

Pili magonjwa yatokanayo na ulaji m-baya na maisha ya bila mazoezi huwaathiri sana watu weusi kuliko wazungu. Hatari ya muafrika kupata kisukari aina ya pili ni mara mbili ya mzungu. Pia magonjwa kama High blood pressure yanawapata sana watu weusi kuliko wazungu. Na hata madhara yake huwa makubwa zaidi kwa weusi kuliko wazungu.

Sasa, pamoja na hatari hii, bado tunakula vitu sawa. Coca cola zile zile, pepsi zilezile, juisi na vyakula vingine, kitimoto na nyama ya kopo, na siagi na mikate vilevile. Hii ni kujihatarisha. Fikiria hapo. Hatari ya kupata kisukari aina ya pili kwa mtu mweusi ni mara mbili ya mzungu.

Kihistoria, inaonyesha binadamu tunapenda sana vyakula vya sukari na mafuta sababu vilikuwa adimu sana miaka hiyo tunakimbiza wanyama porini. Hatukuumbwa kula sukari na mafuta mengi kama tunayokula leo.

Napendekeza kuwe na onyo kwenye juisi na softdrinks zote. Zikisema unywaji kupita kiasi ni hatari kwa afya. Hata vyakula vya mafuta mengi viwekewe maonyo hayo. Tusiige ulaji wa wazungu, tupo tofauti kulingana na mazingira yetu. Tunachofanya kwenye chakula, ni sawa na mzungu amuige mtu mweusi kujianika juani.
Khatari kweli
 
Back
Top Bottom