Soka la Serie A kushuka ubora

Smt016

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2016
Posts
3,012
Reaction score
4,300
Soka la Italy lilitawala sana barani Ulaya, lakini kuanzia kuporomoka kwa timu ya Ac Milan baada ya msimu wa 2007 kutokana na sababu mbali mbali ikiwepo za uchumi, kisiasa na mipango mibovu ya kutowaanda vijana. Ndipo ikawa mwisho wa utawala wa Serie A kwenye michuano ya UEFA.

Kuna wakati wakapoteza hadi nafasi ya kutoa wakilishi wanne kwenye champions league. Timu za Italy zimekuwa na muendelezo wa kuwa viwango vya chini sana kwa sasa, yaani siyo Italy ya kipindi kile. Leo hii Juventus wakufungwa na Maccabi Haifa, Ac Milan imepoteza ubora kabisa, wamekuwa wabovu kupindukia.

Intermilan nayo tia maji tia maji. Msimu huu kidogo Napoli kaonesha ushindani japo haijulikani safari yao itaishia wapi.

Kushuka kwa soka la Italy shida ni nini wadau?
 
Ila ninachowakubali hawa wenzetu wanakuwaga na mipango mkakati ya muda mrefu
Wanapotea kwa muda ila baadae wanarudi kwa kishindo
 
Ila ninachowakubali hawa wenzetu wanakuwaga na mipango mkakati ya muda mrefu
Wanapotea kwa muda ila baadae wanarudi kwa kishindo

Wao hawakuoni wewe kama mwenzao.
 
Mpira ni fedha, AC Milan ya miaka ya 90' Ili sheheni Nyota wote wa ulimwengu huu. Wakina Zvonimir Boban, Lui Costa, George weah, Marco VanBastern, Roberto Baggio, Franco Bares, Paulo Maldin, Marcel Desaily, Roberto Donadon, Allesandro costarcurta, Dicanio Paulo n.k ilikua kama Madrid ya Italy.
Sasa uchumi umeyumba sana Kwa wataliano,ukijumlisha na corona ilivyo wamaliza watachukua muda ku Recover.
 
Ila jamaa wanajua kutengeneza makocha napia wanawathamini sana makocha wao. Timu kubwa zote ukiondoa roma zinafundishwa na wazawa. Kwa hilo mie nawakubali wataliano.
 
Juve,Inter,Ac Milan wanakandwa popote pale iwe home au away tena wanakandwa na timu za kawaida sana.Napoli nawaona wanakuja moto sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…