Pana msemo usemao 'mkulima mvivu haishi kulilalamikia jembe kuwa halilimi vizuri'. Nimekuwa najifikiria sana hasa timu ya soka kama Yanga na Simba inaposhindwa katika mechi viongozi, makocha na mashabiki wao huanza kujenga hoja za kulaumu waamuzi kwa kushindwa kuchezesha vizuri. Mie hujiuliza kama timu hizo zenye tabia/utamaduni wa kuwalalamikia waamuzi zingejenga misingi imara ya wachezaji wao kimchezo na kisaikolojia waamuzi wasingepata taabu ya kutoa maamuzi sahihi.