mkuki wa maisha
Member
- Sep 26, 2017
- 22
- 17
Habari ya muda huu wadau wa michezo,
Niende moja kwa moja kwenye mada husika,mchezo wa mpira wa miguu nchini Tanzania umekua na unazidi kukua kwa kasi na kupendwa kwa rika zote,pamoja na jinsia zote,hivyo imefanya hata baba wa mpira (Tff) kuwekeza nguvu kwa upande wa wanawake,hongera kwa hilo.Watanzania ni watu wanao penda sanaa huu mchezo kiasi kwamba imekua kama ni sehemu ya maisha yao,na ndio inayo watofautisha na wana Africa mashariki wengi,hasa kwa kupenda ligi ya nyumbani na kuhudhuria viwanjani kwa kiasi fulani cha kuridhisha.
Pamoja na kuwa na mapenzi ya dhati ya huu mchezo miundo mbinu panapochezewa ndio kizungu mkuti,
Umekua wimbo wa miaka nenda rudi kutoka kwa wadau wa huu mchezo kuhusu viwanja ,
Ukiachilia viwanja vichache vilivyo chini ya harmashauri na vile vya baadhi vinavyo milikiwa na chama tawala (ccm) vinahali ya kuridhisha,
Viwanja vingi hasa vinavyo milikiwa na chama tawala (ccm) vimetelekezwa hasa sehemu ya kuchezea imekua kituko kama mazizi ya ngamia au mashamba ya mpunga.ifike mahala hawa wamiliki wajitathimini,kusu utunzaji wa miundo mbinu hii kwa manufaa ya maendeleo ya michezo, kama wameshindwa basi watafute angalau wawekezaji kuviboresha,
Pia maoni yangu kwa Tff wakae chini na hawa wamiliki japo wakodi sehemu za kuchezea (pitch) na wazifanyie marekebisho kama itawezekana,
Mfano viwanjana kama Sokoine ,Nangwanda,majimaji,Mkwakwani,Namfua vipo taabani kwelikweli.
Miundo mbinu iboreshwe kuendana na kasi ya maendeleo ya mchezo wenyewe.
Niende moja kwa moja kwenye mada husika,mchezo wa mpira wa miguu nchini Tanzania umekua na unazidi kukua kwa kasi na kupendwa kwa rika zote,pamoja na jinsia zote,hivyo imefanya hata baba wa mpira (Tff) kuwekeza nguvu kwa upande wa wanawake,hongera kwa hilo.Watanzania ni watu wanao penda sanaa huu mchezo kiasi kwamba imekua kama ni sehemu ya maisha yao,na ndio inayo watofautisha na wana Africa mashariki wengi,hasa kwa kupenda ligi ya nyumbani na kuhudhuria viwanjani kwa kiasi fulani cha kuridhisha.
Pamoja na kuwa na mapenzi ya dhati ya huu mchezo miundo mbinu panapochezewa ndio kizungu mkuti,
Umekua wimbo wa miaka nenda rudi kutoka kwa wadau wa huu mchezo kuhusu viwanja ,
Ukiachilia viwanja vichache vilivyo chini ya harmashauri na vile vya baadhi vinavyo milikiwa na chama tawala (ccm) vinahali ya kuridhisha,
Viwanja vingi hasa vinavyo milikiwa na chama tawala (ccm) vimetelekezwa hasa sehemu ya kuchezea imekua kituko kama mazizi ya ngamia au mashamba ya mpunga.ifike mahala hawa wamiliki wajitathimini,kusu utunzaji wa miundo mbinu hii kwa manufaa ya maendeleo ya michezo, kama wameshindwa basi watafute angalau wawekezaji kuviboresha,
Pia maoni yangu kwa Tff wakae chini na hawa wamiliki japo wakodi sehemu za kuchezea (pitch) na wazifanyie marekebisho kama itawezekana,
Mfano viwanjana kama Sokoine ,Nangwanda,majimaji,Mkwakwani,Namfua vipo taabani kwelikweli.
Miundo mbinu iboreshwe kuendana na kasi ya maendeleo ya mchezo wenyewe.