Katika likizo yangu ya hivi karibuni nikiwa Mwanza, nilitembelea Soko la Kayenze maarufu kwa jina la "Soko la Wakulima," lililopo Wilaya ya Magu, nilishangazwa na hali mbaya ya uchafu iliyokithiri sokoni humo.
Soko hilo ambalo linahifadhi meza takriban 2,000 za Wafanyabiashara, limegeuka kuwa kama dampo la taka. Uchafu kutoka kwenye migahawa ya vyakula, hoteli za jirani, na biashara za ndani ya soko unatupwa kiholela sehemu maalum iliyotengwa na wafanyabiashara baada ya kukosa dampo rasmi.
Harufu mbaya isiyovumilika imetawala soko, hali inayowatia hofu Wafanyabiashara na wateja kuhusu afya zao.
Ahadi Zisizotimia na Kodi Zinazokusanywa
Wafanyabiashara wa Kayenze wanahisi kusalitiwa, wanadai walihamishwa kutoka maeneo yasiyo rasmi kwa ahadi za kupewa miundombinu bora, lakini hali iliyo mbele yao ni tofauti kabisa.
Walipopewa eneo hili miaka miwili iliyopita, walihakikishiwa kuwa wangefanya biashara katika mazingira bora na salama. Hata hivyo, hali ya sasa inaonyesha wazi kwamba ahadi hizi zilikuwa hewa.
Inaelezwa kuwa kila siku wanalipa ushuru wa shilingi 200 kwa kila meza, huku wauza ndizi wakitozwa shilingi 10,000 kwa mwezi kwa usafi na ulinzi.
Licha ya makusanyo haya, soko limeendelea kuwa kwenye hali mbaya ya uchafu. Kama ushuru unakusanywa kila siku, pesa zinaenda wapi? Mbona hatuoni matokeo yoyote?
Kibaya zaidi, Wafanyabiashara wanasema walipewa eneo tu, lakini mabanda walijenga wenyewe kwa gharama zao, hii imeibua maswali miongoni mwao, wakidai wanatozwa ushuru kwa mabanda waliyoyajenga wao wenyewe.
“Hivi, ushuru ni wa mabati, mbao, au mazingira machafu? Serikali ituambie ili tujue” hizo ni baadhi ya kauli za Wanafanyabiashara wa hapo.
Magonjwa ya Mlipuko na Hali Mbaya ya Afya
Soko hili limekuwa chanzo cha magonjwa ya mlipuko. Mwaka 2023, inadaiwa watu wawili walifariki kutokana na ugonjwa wa Kipindupindu, huku wengine wakikumbwa na magonjwa ya kuhara.
Uchafuzi wa mazingira na ukosefu wa miundombinu ya usafi umechangia kwa kiasi kikubwa hali hii mbaya.
Wafanyabiashara wanasema kuwa magonjwa haya yamekuwa sehemu ya maisha yao. "Tunaugua mara kwa mara, lakini hatuwezi kusimamisha biashara zetu. Tuna watoto wa kulea, na Serikali haionyeshi nia ya kutatua tatizo hili," alisema mmoja wa wafanyabiashara.
Serikali Imepoteza Dira?
Wafanyabiashara wamekuwa wakitoa kilio chao mara kwa mara kwa viongozi wa soko, halmashauri ya wilaya, hata wenyeviti wa mkoa. Pamoja na yote, majibu wanayopata ni yale-yale: "Tutalishughulikia." Muda unazidi kusonga, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.
Badala ya kuwasaidia, baadhi ya viongozi huwatishia wafanyabiashara wanaolalamika. "Ukiongea sana, wanakuambia utafute soko jingine. Lakini huu ni mtego, kwa sababu hakuna mahali pengine pa kwenda," alisema mfanyabiashara mmoja kwa masikitiko.
Uoga Unatamalaki
Licha ya hali mbaya sokoni, wafanyabiashara wengi wameamua kukubali hali hiyo kutokana na hofu ya kufungiwa meza zao. "Tulijaribu kugoma mara moja, lakini tulionywa kuwa meza zetu zingebomolewa. Tumeamua kunyamaza tu na kuendelea na biashara," alisema mmoja wao.
Hali hii ya kukosa matumaini imewafanya wafanyabiashara wengi kuendelea kufanya biashara katika mazingira haya machafu. Uchafu unazidi kuongezeka, na harufu mbaya imekuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku.
Suluhisho Lazima Lipatikane
Hali ya Soko la Kayenze inahitaji hatua za haraka, Wafanyabiashara hawa siyo tu wanastahili mazingira safi na salama, lakini pia wanapaswa kuona thamani ya ushuru wanaolipa.
Serikali ya Wilaya ya Magu inapaswa kuwajibika kwa kuhakikisha dampo linahama, mtaro wa maji machafu unatengenezwa, na mazingira ya soko yanaboreshwa kwa ustawi wa wajasiriamali na wateja.
Soko hili ni mfano halisi wa kushindwa kwa mifumo ya usimamizi wa biashara ndogo ndogo nchini.
Je, tunasubiri mlipuko mkubwa wa magonjwa ili hatua zichukuliwe? Serikali inapaswa kusikili
za kilio cha wafanyabiashara wa Kayenze sasa.
Harufu mbaya isiyovumilika imetawala soko, hali inayowatia hofu Wafanyabiashara na wateja kuhusu afya zao.
Wafanyabiashara wa Kayenze wanahisi kusalitiwa, wanadai walihamishwa kutoka maeneo yasiyo rasmi kwa ahadi za kupewa miundombinu bora, lakini hali iliyo mbele yao ni tofauti kabisa.
Inaelezwa kuwa kila siku wanalipa ushuru wa shilingi 200 kwa kila meza, huku wauza ndizi wakitozwa shilingi 10,000 kwa mwezi kwa usafi na ulinzi.
Kibaya zaidi, Wafanyabiashara wanasema walipewa eneo tu, lakini mabanda walijenga wenyewe kwa gharama zao, hii imeibua maswali miongoni mwao, wakidai wanatozwa ushuru kwa mabanda waliyoyajenga wao wenyewe.
“Hivi, ushuru ni wa mabati, mbao, au mazingira machafu? Serikali ituambie ili tujue” hizo ni baadhi ya kauli za Wanafanyabiashara wa hapo.
Soko hili limekuwa chanzo cha magonjwa ya mlipuko. Mwaka 2023, inadaiwa watu wawili walifariki kutokana na ugonjwa wa Kipindupindu, huku wengine wakikumbwa na magonjwa ya kuhara.
Uchafuzi wa mazingira na ukosefu wa miundombinu ya usafi umechangia kwa kiasi kikubwa hali hii mbaya.
Wafanyabiashara wanasema kuwa magonjwa haya yamekuwa sehemu ya maisha yao. "Tunaugua mara kwa mara, lakini hatuwezi kusimamisha biashara zetu. Tuna watoto wa kulea, na Serikali haionyeshi nia ya kutatua tatizo hili," alisema mmoja wa wafanyabiashara.
Wafanyabiashara wamekuwa wakitoa kilio chao mara kwa mara kwa viongozi wa soko, halmashauri ya wilaya, hata wenyeviti wa mkoa. Pamoja na yote, majibu wanayopata ni yale-yale: "Tutalishughulikia." Muda unazidi kusonga, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.
Badala ya kuwasaidia, baadhi ya viongozi huwatishia wafanyabiashara wanaolalamika. "Ukiongea sana, wanakuambia utafute soko jingine. Lakini huu ni mtego, kwa sababu hakuna mahali pengine pa kwenda," alisema mfanyabiashara mmoja kwa masikitiko.
Uoga Unatamalaki
Licha ya hali mbaya sokoni, wafanyabiashara wengi wameamua kukubali hali hiyo kutokana na hofu ya kufungiwa meza zao. "Tulijaribu kugoma mara moja, lakini tulionywa kuwa meza zetu zingebomolewa. Tumeamua kunyamaza tu na kuendelea na biashara," alisema mmoja wao.
Hali hii ya kukosa matumaini imewafanya wafanyabiashara wengi kuendelea kufanya biashara katika mazingira haya machafu. Uchafu unazidi kuongezeka, na harufu mbaya imekuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku.
Suluhisho Lazima Lipatikane
Hali ya Soko la Kayenze inahitaji hatua za haraka, Wafanyabiashara hawa siyo tu wanastahili mazingira safi na salama, lakini pia wanapaswa kuona thamani ya ushuru wanaolipa.
Soko hili ni mfano halisi wa kushindwa kwa mifumo ya usimamizi wa biashara ndogo ndogo nchini.
Je, tunasubiri mlipuko mkubwa wa magonjwa ili hatua zichukuliwe? Serikali inapaswa kusikili
za kilio cha wafanyabiashara wa Kayenze sasa.