Soko la waliosoma sheria (LLB)


kwanini ukwenda USTAWI (ISW)-Kijitonyama ukapiga Industrial Relations!!!! Hii kozi ni balaa, vijana waliosoma hiyo kozi asilimia kubwa wako mzigoni: ukitaka kujua kiundani umuhimu wa hii kozi mtafute Pro. Msoke, Prof. Baregu, Prof Issa Shivji, mtaalamu mwenyewe Mwinula au yeyote aliyeitimu Ustawi 2008 kurudi nyuma.
 
Tuliomaliza LLB MZUMBE 2011 hatufiki hata 200 mkuu na hapakuwa na graduates wa LLB Mzumbe maon campus wote waliokuwa mbeya campus na ndio hao below 200, acha kumislead watu!
 

UDOM watu wa LAW bado hawajaanza ku graduate, nadhani ndo kwanza wapo mwaka wa TATU..
 
bado watoto wa rev.dr kitima saut mwanza hujawajumuisha
 
Tuliomaliza LLB MZUMBE 2011 hatufiki hata 200 mkuu na hapakuwa na graduates wa LLB Mzumbe maon campus wote waliokuwa mbeya campus na ndio hao below 200, acha kumislead watu!

Kwa hiyo unataka kusema kuwa kwa sababu mlikuwa below 200 kazi zitapatikana? Kilichokuwa kinaelezwa hapa ni kuwa graduates wa sheria Tanzania in a year hawawezi kuwa absolved na demand.
 
Kijana nenda kasome kila kitu kinapangwa na mungu maana unaweza kumaliza siku hiyo hiyo ukapata kazi na unaweza kumaliza ukakaa mwaka hadi miaka hujapata kazi na siku ukiipata unasahau yote yaliyokupata huko nyuma.
 
sheria ni course nzuri sana, ila unaweza kuchelewa kupata kazi, kama unataka kuajiriwa, au kama unajiajiri mwanzoni lazima usote, lakini cha kufurahia, ukishatoka, ndo umetoka, unaweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sana, na the more unavyoendelea kuishi unapata experience ya kupractice kila iitwapo leo na ndivyo utakavyopata sana hela...sheria ina pesa sana lakini inahitaji uvumulivu hapa mwanzoni kama hauja ji establish, ukishajiestablish tu, umeshatoka kimaisha, pesa zitakufuata. kazi kwako ni kusoma sana judgement na sheria ili uwe mzuri kisheria.....mimi ni mwanasheria, mwanzoni nilipata shida sana, nakwambia miaka ya mwanzoni tangu nimalize udsm, miaka mitatu ya mwanzoni nilipata shida hadi nililaani kusoma sheria, nilipokuja kusettle, nafurahia sheria vibaya mno na ninapata pesa nyingi ajabu. mambo yote ni revision tu kwangu, ninachofanya ni kusoma vitu vipya na kuendelea kujikumbusha ili nikitokea mahakamani nipractice vizuri....sheria ina pesa sana sana....hakuna mwanasheria anayefikia umri wa miaka 50 hana maisha mazuri...akiwa na miaka chini ya thelathini na tano etc anaweza akawa bado lakini akifikia umri ule wa kustaafu hakika yake fanya utafiti karibia wote huwa wanastaafu wamejijenga sana sana, tofauti na course zingine...nakushauru usome LLB lakini uwe na uvumilivu mwanzoni kabla haujajiimarisha, kama huna uvumilivu, basi nenda kasome sociology ili uajiriwe ustawi wa jamii upate laki mbili na nusu kwa mwezi 250,000/=...au nenda kawe ticha.
 
amini usiamini, nilipokuwa nafanya kazi kama state attorney, kabla sijajitoa na kuwa mwanasheria wa kujitegemea, mwaka mzima nilikuwa situmii/sigusi kabisa mshahara wangu. mshahara hauguswi, napata pesa tu zinakuja ndo za kutumia. nikienda mahakamani asubuhi, lazima nirudi na pesa...si lazima rushwa, wakati mwingine mtu tu umeamua kumwachia labda kwasababu umeona hakuna ushahidi kwenye kesi yake, kesho yake unashangaa anakuletea laki mbili za shukrani, anakushukuru wala hujaomba....cha muhimu ni kukaa vizuri na watu. achilia mbali hizo traffick case, dhamana etc, kuna mianya mingi ya kupata pesa, ambapo hata kama wewe si mla rushwa kama mimi, ukimfanyia mtu fadhila, lazima anaenda kurudi...nilijikuta naishi bila kugusa mshahara wangu....nilisomesha watoto, nilifanya mengi, nje ya mshahara.....chukulia mfano, mwanasheria wa serikali grade ya kwanza au ya pili kwasasa anapata si chini ya laki nane kwa mwezi, lakini hiyo laki nane nakwambia haigusi, kuna pesa nyingine nyingi zinazunguka ofisini kila mwezi, akisafiri kidogo tu analipwa perdiem,

akipanda kidogo tu akapata kuwa senior state attorney, analipwa milioni, akifika principle state attorney analipwa milioni na nusu au zaidi...sasa hizo ni mishahara ya serikali,cha ajabu ni kwamba, unapata hela nyingi zaidi nje ya mshahara, ukijaunganisha, unashangaa karibia mara tatu ya mshahara wako kwa kwezi......ukishapata experience, ndo unajiondoa kama sisi, unaunda lawfirm yako ya kawaida, mtu kumsimamia tu kesi zilizo nyingi anatakiwa aje na milioni na nusu au zaidi....hapo kumsaidia, milioni mbili, tatu, nne hadi ishirini kutegemeana na kesi...cha ajabu, kwasababu mimi nimefanya kazi hiyo mda mrefu, kile kitu ambacho mimi naona rahisi kupita vyote, mwenzangu ananipa pesa ili nikamsimamie, hivyo pale naenda kama marejeo tu ili kukamilisha nipate ile pesa kwasababu karibia kesi nyingi ninazosimamia, kipindi cha nyumba niliwasahi kutana nazo na kusolve tatizo hilo zaidi ya mara hamsini...

kuwa layman/kutojua sheria ni mzigo mzito usiobebeka...nawahona huruma...yaani kile wewe unachoogopa sana kwenda hata mahakamani, kuongea mahakamani, kujitetea au vile usivyojua sheria,,,,mimi mwenzio naona ni kutu rahisi kupindukia....kwenda mahakamani ni sawa tu nawewe unavyoenda kwa kuchez a pool pale kwenye bar ya masawe.....hahaha.
 
we dogo tulu kweli,sheria huwezi lala njaa utawakimbia wateja ila si ya kitoto lazima ukomae course unit 9,6 n.k
 

Hivi wewe una akili timamu?? Hao wanafunzi 50 waliomaliza sheria SEKUCo umewadahili, kuwafundisha na kuwapa hzo degree wewe?? SEKUCo hawatoi sheria halafu wewe unasema wametoa wahtimu 50 wa sheria??
Data unazotoa nazitilia mashaka sana.. Zote znaishia na '00, hakuna namba mchanganyiko kama kawaida, au ume round off
 
Course Yeboyebo usisome hiyo.

chukua watu mia moja waliosoma course yako, linganisha na wale miamoja walisoma sheria, wawe na miaka kuanzia hamsinina kwenda juu, halafu linganisha kipato chao kilivyo kwa sasa. cha muhimu ni kwamba, sheria inahitaji watu wenye akili,ndio maana wasiosoma sheria huwa tunawaita laymen...hawajui lolote....ukiwa na akili na kama unapenda kusomasoma, utafanikiwa ktk sheria, kama we mzembe kama wanaosoma sociology kama wewe, hakika sheria uikimbie...
 
Nimemaliza Ruaha university college, hatujamaliza 200 bali 170 pekee na hakuna chuo kinaitwa Ruaha university Mwanza bali ni St.Augustine University of Tanzania, chuo pekee cha Wakatoliki nchini ambacho kina matawi zaidi ya kumi nchi nzima mojawapo ni Ruaha university college, tawi pekee linalotoa shahada ya sheria.Lakini pamoja na hayo hiyo haiondoi ukweli kuwa waliohitimu law ni wengi kwakweli, isipokuwa tu mwanasheria anaweza kufanya mambo mengi sana.So nilitaka kuweka records vizuri hapo.
 
The country produce too many "white collar" graduates that does not tally with economy demand! together with mathematical and science subject cancer diease!!! We have long way to go!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…