Sokolov baada ya kufufuka asema hakuna kilichotokea

Sokolov baada ya kufufuka asema hakuna kilichotokea

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Kama ilivyowahi kusemwa kuwa mafanikio ya kivita ya Ukraine kati yake na Urusi kuwa namba zake huenda hazipigwi kwa base ten kwani daima huwa ni makubwa mno kuliko uhalisia unaonekana.

Wiki iliyopita Ukraine ilitangaza kupiga makao makuu ya jeshi la majini la Urusi kwenye bandari ya Sevastopot yaliyopo bahari nyeusi.Kituo hicho ni muhimu sana kwa Urusi na ni moja ya lengo kuu la Ukraine kuidhoofisha Urusi.

Katika tangazo lake hilo Ukraine ilisema ilifanikiwa kusambaratisha makao makuu ya jeshi hilo na kuu makamanda 34 miongoni mwao akiwa ni mkuu wa jeshi hilo la Urusi Admiral Viktor Sokolov.

Baada ya kutangazwa mafanikio hayo ya Ukraine ambayo yalikuwa yakirudiwa kila saa, Urusi kwa upande wake haikujibu chochote, Siku tano mbele yake Viktor akaonekana kwenye video akishiriki katika mkutano na waziri wa ulinzi wa Urusi.

Picha hiyo iliwatia kizaazaa kikubwa viongozi wa kijeshi wa Ukraine waliotoa matangazo hayo waliyosema wameyathibitisha kuhusu vifo hivyo.Hilo liliwafanya waanze kujifariji na kujitoa kimaso maso kwa kusema aliyeonekana kwenye video hiyo ni yeye kamanda Sokolov lakini huenda ni picha ya zamani na kama ni ya karibuni basi ilikuwa ya maiti yake au akiwa kitandani hospitali.Dalili walizotoa za kuaminisha hilo ni kwa vile kwanza admiral Sokolov katika video hiyo hakuwa akisema, macho hayafumbi na kufumbua na nyuma yake alikuwa amewekewa mito.

Muda huo waziri wa ulinzi wa Ukraine alihojiwa kwamba mbona kuna tetesi kuwa kiongozi wa jeshi la maji la Urusi yuko hai na jee ana kipi cha kusema.Akajibu kwamba ikiwa amekufa itakuwa ni bora zaidi.

Siku ya pili yake admiral Sokolov akatokea mwenyewe wote mzima kwenye mkutano na waandishi wa habari na alipotakiwa aeleze chochote kuhusiana na shambulio la Urusi kwenye ofisi zake za Sevastopol, akuliza kwani kulitokea nini.Hakumbuki kilichotokea.

Baadhi ya vyombo vya habari vimempatia jina la kamanda wa vita aliyefufuka.

Russia’s Back-From-the-Dead Admiral Insists ‘Nothing Happened’


1695875049694.png
 
hakuna funzo lolote, ukraini alitaka tuhadaa, sema russia akaamua kumtoa kamanda dunia ujue ni porojo

na porojo zitaendelea tena na tena
Kama umekubali hayo yalitokea.Yaani Ukraine ilitaka kutuhadaa kwa ambacho hakikutokea na Urusi ikajibu kivitendo bila maneno.Porojo iko wapi hapo.Chukua mafunzo tu uondoke.
 
Vita havipiganiwi ground pekee ,nyanja ni nyingi misinformation pia ni mojawapo .Kuna mengi ya kujifunza hapo na unauhakika gani kuwa hyo aliyetokea ni sokolov mwenyewe ; technology ilivyo kwa ss hata sishangai kuwa yule ni double agent
Warusi hawafanyi ujinga huo.Na haiwezekani wafanye kwa kamanda mkubwa kama huyo.
 
Vita havipiganiwi ground pekee ,nyanja ni nyingi misinformation pia ni mojawapo .Kuna mengi ya kujifunza hapo na unauhakika gani kuwa hyo aliyetokea ni sokolov mwenyewe ; technology ilivyo kwa ss hata sishangai kuwa yule ni double agent
Umepita mlemle,check aljazeela walivyoandika kuhusu hayo madai ya urusi
Screenshot_20230928-100611.jpg


Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Umepita mlemle,check aljazeela walivyoandika kuhusu hayo madai ya urusi View attachment 2764805

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
Hizo ni za zamani .Msikilize huyu hapa
 
Russia anajaribu kujipoza mumivu




[emoji298]Washington, DC-based think tank, the Institute for the Study of War (ISW), said on Wednesday that while Russian media were at pains to “publish inconclusive ‘proof’” that the Black Sea fleet commander is still alive, the institute would reserve judgement until more is known.


“ISW is unprepared at this time to make an assessment about the authenticity of the footage or the date of its filming,” the think tank said.

“The Kremlin and Russian Ministry of Defense have been notably silent on the matter and have not directly confirmed that Sokolov is alive,” it added.

Ukraine’s Special Operation Forces posted a statement on Tuesday saying its sources had claimed that Sokolov was among the dead from the missile strike and that it was trying to verify those reports after the video of Sokolov surfaced.
Black Sea Fleet leadership, reportedly killing many officers at their HQ.


Russian Black Sea commander seen in video after Ukraine said it killed him
Viktor Solokov, Moscow’s top admiral in Crimea, was shown in a Russian defence ministry video conference.





Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Russia anajaribu kujipoza mumivu




[emoji298]Washington, DC-based think tank, the Institute for the Study of War (ISW), said on Wednesday that while Russian media were at pains to “publish inconclusive ‘proof’” that the Black Sea fleet commander is still alive, the institute would reserve judgement until more is known.


“ISW is unprepared at this time to make an assessment about the authenticity of the footage or the date of its filming,” the think tank said.

“The Kremlin and Russian Ministry of Defense have been notably silent on the matter and have not directly confirmed that Sokolov is alive,” it added.

Ukraine’s Special Operation Forces posted a statement on Tuesday saying its sources had claimed that Sokolov was among the dead from the missile strike and that it was trying to verify those reports after the video of Sokolov surfaced.
Black Sea Fleet leadership, reportedly killing many officers at their HQ.


Russian Black Sea commander seen in video after Ukraine said it killed him
Viktor Solokov, Moscow’s top admiral in Crimea, was shown in a Russian defence ministry video conference.





Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
Sasa nini wamesema hapo.
Haingii akilini katika kipindi hiki cha vita kwamba makamanda wakuu wa kikosi cha majini cha Urusi kilikuwa kipo kwenye majengo hayo ya ghorofa tena wamejikushanya pamoja kiasi kwamba storm shadow ikawalipua wote kwa pamoja.
 
Back
Top Bottom