Solutions to albinos' situation

Solutions to albinos' situation

Nkamangi

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
641
Reaction score
32
It's been yet another sad year for albinos in Tanzania. As if the wrath of ultra violet rays on their skin was not enough to keep them worried about their lives, now they are being hunted like endangered animals who hold a secret to success... I urge you to come up with ideas as to what can be done in this coming year to help our brethren. Practical things that can be applied on the ground. I've noticed there's an excellent variety of creative minds in this forum
 
Mama mbaroni kwa kutaka kumuuza mwanawe albino
• Bei yake ilikuwa milioni 15/-

na Julieth Mkireri, Pwani




JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani limewakamata Mwajabu Said (66) na mama na mtoto wake, Said Omary (40), kwa tuhuma za kula njama za kutaka kumuuza binti wa mama huyo aliyetajwa kwa jina la Kabuyu Dalili (22), mwenye ulemavu wa ngozi (albino ) kwa sh milioni 15.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Absalom Mwakyoma, jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa, mama na mtoto wake wanadaiwa kula njama za kuandaa mpango huo na mtu ambaye aliahidi kuwalipa kiasi hicho cha fedha.

Alisema, uchunguzi wa polisi umebaini kuwa biashara hiyo ilipangwa kufanyika Desemba 26, siku moja baada ya Sikukuu ya Krismasi.

Kamanda huyo alisema binti huyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kwamba anakusudia kuuzwa kwa kitita hicho cha fedha alikimbilia katika kituo cha polisi kwa ajili ya usalama wake.

Kwamba baada ya polisi kupewa taarifa hizo, walimtaka binti huyo kubaki kituoni hapo na wao walikwenda kijijini Fukayosi alikokuwa akiishi na kuwakamata watuhumiwa.

Alisema uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea ili kuwatia mbaroni wahusika waliotaka kumnunua albino huyo.

Je kwa hali hii tutafiaka??
 
Back
Top Bottom