The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Takribani watu 24 wamefariki dunia baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba raia wa Somalia kupinduka katika pwani ya Madagascar.
Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia zinasema juhudi zinaendelea kuhakikisha kuwa manusura wanaokolewa wakiwa salama.
Boti hizo mbili zilikuwa zimebeba abiria 70 ziligunduliwa zikiwa karibu na pwani ya kaskazini mwa Madagascar Novemba 23, 2024 katika Bahari ya Hindi hata hivyo Inadaiwa sababu ya boti hizo kupinduka ni injini kufeli.
Walionusurika wanasema walikuwa safarini kwenda kisiwa cha Ufaransa cha Mayotte kwa wahamiaji wa Kisomali wanaotafuta hifadhi.
Madagascar imetoa onyo kali kuhusu uhamiaji haramu na kusema waathirika wa janga hilo walikuwa wahamiaji.
Sma pia: Warembo wawili wa Brazil wafariki baada ya kukataa kuvaa Jaketi za Kuokoa Maisha ili kupiga Selfies katika ajali ya Boti
Chanzo: Mwananchi
Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia zinasema juhudi zinaendelea kuhakikisha kuwa manusura wanaokolewa wakiwa salama.
Boti hizo mbili zilikuwa zimebeba abiria 70 ziligunduliwa zikiwa karibu na pwani ya kaskazini mwa Madagascar Novemba 23, 2024 katika Bahari ya Hindi hata hivyo Inadaiwa sababu ya boti hizo kupinduka ni injini kufeli.
Walionusurika wanasema walikuwa safarini kwenda kisiwa cha Ufaransa cha Mayotte kwa wahamiaji wa Kisomali wanaotafuta hifadhi.
Madagascar imetoa onyo kali kuhusu uhamiaji haramu na kusema waathirika wa janga hilo walikuwa wahamiaji.
Sma pia: Warembo wawili wa Brazil wafariki baada ya kukataa kuvaa Jaketi za Kuokoa Maisha ili kupiga Selfies katika ajali ya Boti
Chanzo: Mwananchi