Somo la Kujitambua: Mara nyingi watu hupigana na kuuana kwa mambo ya kufikirika (People often fight and kill each other over imaginary things)

Somo la Kujitambua: Mara nyingi watu hupigana na kuuana kwa mambo ya kufikirika (People often fight and kill each other over imaginary things)

Venus Star

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2018
Posts
26,519
Reaction score
78,311

MAMBO YA KUFIKRIKA YALIYOPO DUNIANI NI YAPI?​

Kuna mambo mengi sana ya kufikirika yameundwa na kupewa uhai ambayo yanaleta ugomvi mwingi kwa watu hapa duniani. Katika masomo yangu haya niliyoyaanzisha ya kujitambua, kuna watu watajifunza na kufunguliwa nafsi zao na kuwa huru.

Baadhi ya mambo ya Kufikirika Ni kama ifuatavyo:-
  • Mungu
  • Shetani
  • Vyama vya Siasa
  • Demokrasia
  • Timu za mpira
  • Mapenzi
  • Nchi
  • Kabila
Nk...
Vitu hivi ni vya kufikirika havipo. Vimetengenezwa ndani ya ubongo tu.

Ili kuweza kujitambua, ni vyema kujua kuwa hayo mambo na mengine yafananayo na hayo ni vitu vya dhahania tu. Havina uwezo wa kujitetea maana havipo.

TUFANYEJE KUONDOKANA NA UTUMWA HUU WA KIFIRA​

Ni muhimu sana kujenga tabia ya kujitazama kwenye kioo na kupata muda wa kukaa pekee yako. Kupata muda wa kuweza kufanya Meditation. Kufanya hivyo utaanza kujitambua wewe ni nani na uwezo wako upo namna gani.

Baada ya kufunguliwa kutoka kwenye utumwa wa fikira utaanza kuwapenda binadamu wenzako. Hutaendeshwa na vitu vya kufikirika. Utaelewa wewe ni nani na lengo lako la kuwepo hapa ni nini.
 
Tuambie kwanza kama Venus star it's really or it's just imaginary!.
 

Kwanini Mwanamke unayesema unampenda akifanya mapenzi na mtu mwingine unaumia?​

Kama ninavyoendelea kufundisha. Mtu yupo katika sehemu mbili:
  • Ulimwengu wa Roho
  • Ulimwengu wa Mwili

Ulimwengu wa Roho upo katika sehemu mbili:-
  • Roho
  • Nafsi

Nafsi ipo katika sehemu kuu tatu:-
  • Ufahamu
  • Hisia
  • Utashi

Ufahamu unaweza kujazwa vitu ambavyo ni imaginary na kuweza kuathili Utashi na Hisia. Kwa kuwa mwili upo connected direct na nafsi mambo yaliyoingizwa kwenye nafsi yanaweza kuleta impact kwenye mwili.

Ili kuweza kuleta taarifa nzuri kwenye nafsi na kuleta mpact kwenye mwili ni muhimu kuanza kujifunza kupata taarifa kutoka rohoni. Maana huko rohoni ndio asili yetu.
 
Back
Top Bottom