Songa ndiye emcee bora tamaduni music

One de incredible namwelewa san huyu mnyama
Nipo Boooth...natema flow kama tupa, mashairi yana rukaruka kama kuku mwenye mzuka, kapuku ukilaza buti tunakunoa kama tupa na kamwe siishiwi chenji kama biashara ya sambusa.

Mi ndio INCREDIBLE MOKO YA MIUJIZA na kwa ya kiume Vocal ka ya Jesus, madha kanifunza nisiwe mchoyo wa maarifa, nibakie msiri asiye na dhambi kama choo cha KANISA....aaaa

.....mi koboko we kibisa, mi ni soko wewe ni hisa, shika namba niite MOko chagua mbili mpaka tisa.....

Mautundu yasiyo jificha kama mtutu wa jambazi, nipo huku toka yankee dungu mpaka panki nina mudu kila mdundo toka dufu mpaka dansi

...nitafute kama hunioni basi jua nipo juu naning'ing'inia kama tone la kamasi

Tamaduni MUSIC

[emoji767] Mchwa Shababi
 
one the incridible pia ni graduate udsm b.of math's

Punguzeni kuwapa watu sifa ambazo hawana.One Incredible (Harry Kaale) alifeli form 4 then aje ku-graduate UDSM tena Bachelor of Mathematics ?

Nafikiri kuna kipindi alikuwa anasoma UCC,
ROMA ndio graduate wa UDSM Computer Science
 
Ahahaaaaah...
Umetisha mkuu...
Natamani JF ingekua na uwezo wa kutuma na kupokea voice note...
Hapo wale wagumu wa kuelewa wangetuelewa vizuri...!
 

Na nipo haire kama group la maras....mautundu yasiyojificha kama mtutu wa jambazi
 
Punguzeni kuwapa watu sifa ambazo hawana.One Incredible (Harry Kaale) alifeli form 4 then aje ku-graduate UDSM tena Bachelor of Mathematics ?

Nafikiri kuna kipindi alikuwa anasoma UCC,
Sasa wewe ndo unazingua...
One the Incredible anaitwa HARRY KAALE...?
Kapekue tena mafaili yako vizuri mkuu..!
 
Sasa wewe ndo unazingua...
One the Incredible anaitwa HARRY KAALE...?
Kapekue tena mafaili yako vizuri mkuu..!

Tuambie anaitwa nani na miaka aliyosoma hapo UDSM ?

FYI
Nawajua vizuri sana Stereo,Mbishi,Incredible,Zaidi na producer wao Duke
 
Punguzeni kuwapa watu sifa ambazo hawana.One Incredible (Harry Kaale) alifeli form 4 then aje ku-graduate UDSM tena Bachelor of Mathematics ?

Nafikiri kuna kipindi alikuwa anasoma UCC,
ROMA ndio graduate wa UDSM Computer Science
Sorry mkuu...
Naona mim ndo nimejichanganya...
Me hadi Leo jina halisi la one incredible nilikua nikijua ni RASHIDI..!
 
acha nikeshe booth
Kicheche akeshe uchi
Usiku apewe ngoma na
Kesho asepe bush

Sina ustaa kivipi
Niupende uzushi
Navyoinukisha mitaa
utadhani Nina genge la uzushi

Shtuka mmbongo
kua na ubongo wa future
wangapi wanatoa hongo
na kwenye mchongo wanashushwa

Ukweli unaishi
uongo unakufa maneno
hujengwa na maandishi
Kwa kua udongo una nyufa

Songa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…