Songwe: DC Farida Mgomi asema “Tumieni mikopo ya 10% kwa matumizi lengwa ili mpate marejesho”

Songwe: DC Farida Mgomi asema “Tumieni mikopo ya 10% kwa matumizi lengwa ili mpate marejesho”

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.55.19_860b5e2f.jpg
Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mkoani Songwe, Farida Mgomi ametoa rai kwa vikundi vya maendeleo vilivyonufaika na mikopo ya Asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kuitumia mikopo hiyo kwa matumizi lengwa sambamba na kukumbuka kuirudisha ili kutoa nafasi kwa vikundi vingine kupata nafasi ya kukopa.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa utoaji wa Mikopo ya Asilimia Kumi kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na wenye Ulemavu iliyofanyika katika ukumbi wa Community Center uliopo wilayani hapo, Novemba 20, 2024, DC Mgomi amevipongeza vikundi vya maendeleo vilivyopata mkopo huo sambamba na kuvihimiza kuwekeza katika shughuli lengwa ili kupata faida pamoja na kurudisha marejesho ya mkopo huo.

DC Mgomi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kujali masilahi ya wananchi wa Wilaya ya Ileje kupitia mikopo hiyo inayolenga kuimarisha hali ya kiuchumi ya vikundi vya maendeleo.
WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.55.20_450a4042.jpg

WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.55.20_1e0545d6.jpg

Aidha, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya yetu, Nuru Waziri Kindamba kwa kusimamia na kuhakikisha zoezi la utoaji wa mikopo linakwenda vizuri.

WhatsApp Image 2024-11-21 at 09.55.21_35f76969.jpg
 
Back
Top Bottom