Mfano mzuri wa changamoto ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe ni Idara ya Macho ambayo kiukweli haina utulivu kabisa. Mgonjwa anaambiwa aje Saa 2:00 Asubuhi kwa ajili ya operation, analazimika kusubiri kwa zaidi ya Saa 6 huku akiwa hajui kinachoendelea.
Akiingia chumba cha upasuaji, kelele za daktari zinaanza. Mara tuliza macho, mara hutoi ushirikiano. Kwani hivi hakuna vifaa na dawa za ganzi maalum ili jicho litulie? Jicho halitulizwi kwa kukemewa, bali kwa dawa.
Tunajua hospitali yetu ni changa na labda vifaa havitoshelezi sasa kama ni hivyo kulikuwa na ulazima wa kuanzisha idara bila kijipanga?
Kama sio dhambi, hawa Watumishi wapelekwe hata pale CCBRT ili wajifunze utendaji kazi wa Idara ya Macho unavyyofanyika.
Akiingia chumba cha upasuaji, kelele za daktari zinaanza. Mara tuliza macho, mara hutoi ushirikiano. Kwani hivi hakuna vifaa na dawa za ganzi maalum ili jicho litulie? Jicho halitulizwi kwa kukemewa, bali kwa dawa.
Tunajua hospitali yetu ni changa na labda vifaa havitoshelezi sasa kama ni hivyo kulikuwa na ulazima wa kuanzisha idara bila kijipanga?
Kama sio dhambi, hawa Watumishi wapelekwe hata pale CCBRT ili wajifunze utendaji kazi wa Idara ya Macho unavyyofanyika.